Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Monday, December 31

UKWELI KUHUSU WEWE

Wewe ndiye mjenzi na mbomoaji wa maisha yako katika nyanja zote kwa fikra zako kwani fikra ndiyo mbegu ndani yako itoayo matokeo kadiri ya sababisho litokanalo na msukumo wa kimazingira. Hivyo mafanikio yako huja kwa kupanda fikra za mafanikio na kutofanikiwa huja kwa kupanda fikra za kushindwa,uma kwa kujua na kutojua.
Wewe ni msanifu na mjenzi wa maisha yako(picha na cognitivesocialweb.com)




Wewe ndiye unayebomoa na kuangamiza maisha yako kwa fikra zako,kwa kujua ama pasipo kutambua(picha na hot100tips.com)

Kamwe huwezi kufanikiwa kama hujui unachokitaka,huwezi kuona mbele pasipoonekana kama hufahamu uendapo,ni mpaka pale utakapojua unataka kuwa nani,ndipo utakapokuwa.....ni sawa na kwenda safari isiyojulikana hata uelekeo.

Mungu alipokuuumba alikupa nguvu na uwezo,akaifanya dunia na vyote vinavyokuzunguka vitii maagizo yako,hasa yale yanayotokana na msukumo wa moyo wako..hivyo wewe ni kiumbe bora jinsi ulivyoumbwa,wewe ni aidi ya ulivyo,wewe ni upendo,amani,faraja,chuki,visasi,wewe ni mwerevu,na msanifu wa maisha yako mwenyewe,hivyo hupaswi kumlaumu yeyote kuhusiana na jambo lolote linalohusu maisha yako,chukua hatua juu ya maisha yako mwenyewe.

Ndani yako ni chemchemi ya kila hali iletayo matokeo hasi ama chanya,ukifikiri kuhusu upendo utafute ndani yako,ukitaka kujua kuhusu uwezo ulio nao,utafute ndani yako,ukitaka kujua kuhusu mafanikio yako,tafuta ndani mwako...chemchemi yako haileti faida kama hujachukua maamuzi

Huna tofauti na binadamu mwingine kwa maana ya uwezo......anza kwanza kuuchunguza ubora wako uujue,ukiutambua,utambue kuwa wengine ni bora kama wewe,hivyo matendo yako yazingatie matokeo yake,fikra zako ziwe fikra njema juu yako na kwa wengine kwani kila utendalo kwa wengine,umejitendea mwenyewe.Maisha ni uchaguzi wako,na matokeo ya kila unachochagua ni juu yako.

Fikra zitokazo kwako ni sewa na bustani ama shamba,inaitaji kutazamwa na kupaliliwa...kuhakikisha kuwa unapanda mbegu bora,ukipanda mbegu isiyo bora (fikra mbaya dhidi yako na maisha yako) huleta matokeo sawia na mbegu uliyoipanda.

Maisha unayoyaishi hayatokei kwa kiitwacho bahati(nzuri ama mbaya) bali ni matokeo ya uchaguzi wako mwenyewe ama kwa kutambua na kutotambua.Umasikini,utajiri,furaha,huzuni,amani,chuki,upendo vyote ni matokeo ya uchaguzi wa maisha yako.Nguvu na uwezo wa kubadili matokeo hayo hutoka ndani mwako....Ni msukumo utokao ndani mwako pekee ndio utakaobadili maisha yako.

Kamwe wewe huvuti maishani vile vitu unavyovitamani ama maisha unayoyatamani,bali unavuta jinsi ya fikra zako.Fikra a ushindi huleta ushindi,fikra za kushindwa huleta kushindwa.

Mara nyingi unajaribu kubadili hali ama mazingira yanayokuzunguka pasipo kubadili fikra zako juu ya mambo hayo....Jinsi uvitazamavyo vitu huwa...ukilitazama jambo kwa uchanya wake,basi kila hali huwa ni nafasi,kama ni mtazamo hasi,basi matokeo yake huwa hasi na kwako huwa ni maumivu.

NURU NA GIZA

Bila shaka kila mmoja yu na furaha siku ya leo.Karibu tena katika somo jipya leo hii.Somo hili litakufanya utambue jinsi wewe ulivyo muendeshaji wa maisha yko,ni somo litakalokufanya ujue kuwa wewe ndiye mjenzi na ndiye unayebomoa maisha yako mwenyewe,iwe kwa kutambua ama kutotambua.Karibu tujifunze pamoja

Ni mara nyingi tumekuwa tukikumbushana kuwa Mungu ametuumba kwa mfano wake,kwa kutupatia uwezo wa kutenda kama yeye.Naye hujidhihirisha kuwepo kwetu kwa njia ya upendo,ni sawa na kusema upendo ni Mungu ndani yetu.Upendo ni nuru ya Mungu iliyopo ndani yetu.Hivyo kila jambo litendwalo kwa msukumo wa upendo hufanya nuru ya Mungu iliyopo ndani yetu hung'aa.
Upendo ni nuru,kama nilivyoeleza hapo juu.Kinyume chake ni chuki,ama giza. Kila tutendapo jambo kwa chuki,basi nuru huzimika ndani yetu  na linabaki giza


Upendo ni nuru iliyo ndani ya mioyo yetu,kila tutendapo kwa upendo maisha yetu huwa nuru kwa wengine (picha kwa msaada wa mtandao)


 Giza ndani ya mioyo yetu hutokana na kutoweka kwa mwanga,yaani kutenda pasipo upendo.Inamaanisha visasi,migogoro,ugomvi....yote hii huipoteza nuru iliyopo kwako.Ama kwa kutambua na kutotambua,unayajenga maisha yako kwa uchaguzi wako mwenyewe,ambao hutokana na kutenda kwa upendo ama kinyume chake (giza).Ni sawa na kusema tunayafanya maisha yetu kung'ara ama kufifia kwa maamuzi yetu wenyewe.
Atandaye kwa upendo hulipwa upendo.Moyo wake hujawa furaha na hivyo hufungua njia ya mafanikio katika kila jambo alipendalo.Huamsha mwili wenye uchangamfu na uso uliojawa bna furaha na amani.Nuru yake hung'aa daima.Hata siku zake za kuishi hapa duniani zinapokwisha,huenda kwa amani.Nuru yake huendelea kung'aa vizazi hata vizazi.Mifano ipo mingi
Mfano wa kwanza ni ule wa Yesu,Kristu (mnazareti).Huyu alifanya kila jambo kwa kusukumwa na upendo.Alitoa maisha yake kwa ajili ya wengine.Alifundisha upendo kwa kutenda na kuuishi.Akawa faraja kwa wote ambao walikuwa hawathaminiki katika jamii.Hata alipoondoka,wengi wa wafuasi wake na wasio wafuasi wamezidi kumkumbuka,na hata sasa wanaozaliwa baada yake hukumbuka na kumtambua kwa kupitia matokeo ya upendo .Wengine ni wengi ambao tumekuwa tukiwasikia ama kupata kuwaona katika jamii yetu.
Kutenda kwa upendo humaanisha kujali,kuthamini wengine.
Sisi ni wa thamani kwa sababu Mungu yupo ndani yetu.Hivyo kila unapojitazama na kujikumbusha thamani yako,kumbuka ya kuwa kila anayekuzunguka ana thamani sawia na ile uliyonayo,hivyo kila utendalo kwa wengine,umejitendea wewe.Unapotenda kwa upendo kwa wengine,umejitendea wewe,vivyo hivyo,unapotenda kwa wenako kwa chuki,basi umejitendea mwenyewe.
Upendo ndio lugha ya pekee inayounganisha viumbe wote duniani(picha kwa msaada wa mtandao)
 

Hivyo kwa maelezo hayo juu,tunajifunza kuwa sisi tunajenga ama kubomoa maisha wetu wenyewe kwa uchaguzi tunaoufanya wenyewe.Katika kila huduma unayoitoa,iwe ni elimu,biashara..ukitenda kwa upendo unafanikiwa.Ukitoa huduma kwa chuki unadidimiza mafanikio yako mwenyewe,iwe kwa kutambua hilo ama kutotambua.Chukua mfano unafanya biashara;wanapokuja wateja unawachangamkia kwa furaha na upendo..ukiwahudumia vema na kuwapa ushauri mzuri na ukatenda kinyume chake,ni lipi kati ya matendo hayo juu itakuletea mafanikio?

Nuru ya Mungu iliyopo ndani mwetu haifichiki kamwe,viumbe vyote duniani huvutiwa na nuru hiyo
Tunapokianza kipindi kipya katika mpangili wa miaka,tukumbuke kuwa tutahesabu mafanikio ama kutofanikiwa katika malengo yetu kwa  kuchagua wenyewe,nuru ama giza

Kuna furaha kubwa kwa wale wanaouchagua upendo,furaha huwa daima maishani mwao,na daima nuru ya Mungu iliyo ndani mwao hung'aa daima na kuwafanya wengine wajifunze toka kwao.Heri ya maandalizi ya kipindi kipya cha mwaka 2013.


Friday, December 7

Kumbuka wimbo wako




Katika dunia hii ni vema kuyaishi maisha yako pasipo kuigiza,yawe yako halisi..Ukiyaishi kwa juhudi zako,hutapata kuwa na wasiwasi juu ya kifo na matokeo yake...Waheshimu wengine wote,heshimu imani zao,fikra zao na mitazamo yao.Yapende maisha yako,furahia maisha yako,heshimu maamuzi yako katika maisha,sikiliza hisia za moyo wako...Fikiri kuishi maisha marefu yenye thamani kwa wengine.Kila ukutanapo na watu,wafanye watambuae nuru ya Mungu iliyo ndani mwako...ing'ae kwao,nao wajifunze kutoka katika nuru hiyo,na kuwafanya nao pia waishi maisha yao halisi yenye thamani kwa wengine....Wathamini wote,wageni kwa wenyeji...Kila uamkapo tafakari thamani yako na nafasi uliyonayo kutenda makubwa zaidi..shukuru kwa siku mpya,Kama hutaona sababu ya kushukuru,basi ndani yako hujautambua mwanga,na utaidanganya nafsi yako mwenyewe..: Na pale wakati wako wa kuyaendea maisha mengine mapya hutapatwa na woga,wala wasiwasi juu ya yajayo.....usiogope kama wale ambao kifo kikiwajia hujaa hofu na kuomba muda kidogo wa kutekeleza yale ambayo hawakuyatilia maanani pale waliposukumwa na mioyo yao kutenda...Kumbuka wimbo wako...wa kumkaribisha rafiki yako,atakayekupokea katika maisha mapya,kifo...kisha aga dunia kwa furaha,kwa sababu uliishi vema..kishujaa.

Tuesday, December 4

IAMBIE NAFSI YAKO

 Tumeumbwa na kupewa mamlaka juu ya maisha yetu na juu ya kila kilicho juu ya nchi,Hivyo tunapaswa kukumbuka kuwa kila kitu tunachokihitaji maishani mwetu kipo katika uwezo wetu tuliopewa na Muumba...mradi tu ulihitaji jambo hilo kwa dhati kabisa toka moyoni mwako....
Kwa kutambua hilo huna sababu ya kuwa na wasiwasi juu ya maisha na juu ya kesho....iambie nafsi yako kwa dhati kabisa toka moyoni yakuwa Unaweza.
Unaweza kuwa imara kuliko hofu uliyonayo,
Unaweza kabisa kuwa na afya bora,furaha na amani,
Unaweza pia kuwa sababu ya vyote hivyo kwa wengine,
Unaweza kuwafanya wengine watambue kuwa wao ni nuru,nao wanapaswa kuifanya nuru hiyo iangaze wengine
Kuafanya wayatazame maisha katika upande wa mwangaza

Iambie nafsi yako kuwa,
Unaweza kubadili maisha yako na kuyafanya kuwa nuru,
Unaweza kufikiri chanya na kutenda kwa uwezo wako wote
Kuwa chachu ya mabadiliko chanya duniani,na kuwa mfano wa kuigwa

Iambie nafsi yako yakuwa unaweza kusahau yaliyopita,
ambayo yalikusababishia maumivu,na kuishi maisha yenye furaha na matumaini,ukianza upya bila woga,
Unaweza kuwapenda na kuwajali wengine pasipo kutazama maumivu ama mabaya waliyokutendea
Unaweza kusimama imara hata katika nyakati za magumu mengi
        furaha ni pale unapotumia maisha yako kuwa furaha kwa wengine-unaweza kuwa chachu ya upendo na anani


Sema kwa nafsi yako kuwa unaweza
Kuishi bila kusengenya na kuwanenea wengine kwa ubaya,bali unaweza kuwa faraja kwa watu wote,
Iambie nafsi yako kuwa wewe ,ukiwa kama nafsi huru,
Una jukumu la kutenda hapa duniani,
Iambie nafsi yako itazame kwa kina,
Ichunguze umuhimu wa maisha yako hapa duniani
Na kisha kuamua kufanya dunia kuwa sehemu ya upendo

Wednesday, October 31

JIFUNZE KUFANYA MAAMUZI MAGUMU

Kuna faida kubbwa sana kwa mtu kujitambua.Utafahamu ni jinsi gani unaweza kuchukua maamuzi ya kugeuza maisha ambayo huyapendi na kuishi maisha mapya,n ndipo utakapokuwa tayari kuchukua hatua ya kufanya maamuzi magumu maishani...amua,kaa na kuandika kila jambo unalhitaji ulifanye kwa mwaka mzima,andika kila jamnbo kwa kina...kwa makini tafuta  picha ya jinsi gani unataka maisha yako kuwa...kisha chukua hatua kuanza maisha hay sasa,wakati ni sasa...mwaka wako unaanza sasa...na hakuna mwisho...kila mwisho wa jambo moja utaanzisha jambo jipya..... kumbuka kama huna malengo huwezi kufanya lolote..hivyo weka malengo yako sas..yafanye kuwa dura yako...chukua  hatua hata kama unahisi ni vigumu kusonga mbele...chukua hatua...narudia usiogope kuchukua hatua juu ya maisha yako mwenyewe

ONDOA HOFU KWA WENGINE

 Dunia ina watu wengi ambao daima hukatisha wengine tamaa.,hukatisha tamaa ama kwa maneno yao,vitendo  vyao na kwa njia  nyingine mbalimbali....hawa hiufanya dunia kuwa sehemu ya hofu na mataraji yaliyojaa kukata tamaa....
Ni muhimu tukaitangaza dunia yenye matarajio mema kwa kila mmoja ,tunao uwezo huo,timiza wajibu wako kwa njia yeyote ulionayo iitakayoifanya  dunia kuwa sehemu bora...fanya chochote kitakachoondoa hofu kwa wengine juu ya maisha yao wenyewe kuwafanya wawe jasiri miyoni mwao...washindi na mategemeo makubwa juu ya dunia bora...upendo ndio silaha pekee kufikia hapo.....upendo hushinda yote...........tumeumbwa kufanya maisha ya wengine na yetu kuwa mwanga wa dunia

Monday, October 8

mwanzo wa mafanikio


Pale unapolihitaji jambo lolote kwa moyo wako wote,huwa ndio mwanzo wa mafanikio wa jambo lolote lile.....Msukumo utokao ndani yako ndio mwanzo wa mafanikio yako...kama msukumo ni mdogo utokao ndani mwako ndivyo utoavyo mafanikio madogo...kama ilivyo pia kwamba moto mdogo utoavyo joto dogo pia...Huwezi kupata maendeleo(mafanikio )katika jambo lolote bila kuwa na hamu ya kweli ya kutenda jambo hilo,pasipo mwelekeo(mipango),pasipo kujitolea kwa dhati kulitenda jambo hilo,na wala huwezi kufanikiwa kama jambo ulilosukumwa kulitenda,halijawa sehemu ya fikra na tafakari ya moyo wako kila wakati.Kinachomfanya mtu atambulike ama kufanikiwa si wingi wa mali aliyonayo,bali ni maamuzi ya kweli yatokayo moyoni,ambayo anayehitaji,hujitoa kweli kutimiza lengo(malengo)ALOJIWEKEA.Si idadi ya vyeti alivyonavyo ama elimu aliyonayo...ni kile kilicho ndani mwako...kinachokusukuma kutenda.

Thursday, September 6

ujumbe 2

Ipo siku ambayo hutahesabu tena ni nini unamiliki ama umepoteza.......
chuki,hasira na majaribu yote hayatakuwepo
Haitajalisha kuwa ulikuwa na sura nzuri ya mvuto ama ulionekana wa sura mbaya
wala ngozi,wala jina halitahesabika
Ni NINI KITAHESABIKA....
KiTAHESAbika ulichotoa kwa wengine na si ulichopokea
Kitahesabika ulichojenga ukiwa duniani,kilichowainua wengine,,,na si kile cha kifahari ulichonunua
Ni kila upole,usawa,utu, na kuwanyanyua wote walio wahitaji,
nI vile ulivyo,wewe halisi,ulivyoyaishi maisha yako kwa ajili ya wengine
Si watu wangapi wanakufhamu,ama umaarufu wako bali ni kiasi gani wengine wataumia pale wanapokukosa
Ni ule umuhimu wako kwa wengine
Si kumbukumbu tu kwamba ulikwepo,bali ni kumbukumbu ya maisha ya wengine uliowabadilisha na kuwasaidia kufikia furaha.
Kitakachohesabika si ni muda gani utakmbukwa,bali ni nani na kwa nini unakumbukwa,ni kwa wema uliotenda
Katika maisha tuishio,ni muhimu kuishi maisha yenye faida kwa wengine....
jiulize ni nini kimekuleta duniani...ishi kilichokuleta

Sunday, September 2

UJUMBE

Wakati mwingine huhisi kuwa niandikayo hapotea tuu,hutazamwa tuu,na hata kutotiliwa maanani...hii hainikatishi tamaa...siuzi ujumbe...hutolewa bure...wakati mwingine nafikiri kurudia na kurudia
Wakati mwingine nasoma kwa kurudia na kurudia,nami hupata faraja.Siandiki tu kujifurahisha....naandika nikilenga kubadili maisha ya wale walio katika huzuni,kuanguka na wote wanaohitaji maneno tu kusimama na kuanza tena maisha yenye mafanikio...naweza nikawa sijaridhisha wengi,lakini ukweli ni kwamba nitaweza kuinua wachache...kwa yule ambaye huguswa na hata machache ,huu ni upendo wangu uende0 kwa wote....naamini siku moja nitakuwa sababu ya furaha kwa wengi...Ni tamaa yangu kuona ujumbe unafika mbali...kuwaamsha wengi....naamini ipo siku mlango mkubwa utafunguka...kwa ajili ya wengi..nami nitajitolea daima,kusimama pale Mungu atakaponituma.

Saturday, September 1

YALIYOPITA YAMEPITA...SONGA MBELE

Wapo wanaotazama mambo ya jana,juzi na yote waliyoyapitia na kukata tamaa,Wakisikia jinsi marafiki wao wanavyowanenea mabaya,wakitazama kila pande na kuhisi hakuna anayewajali,wakiangalia pande zote wasione tumaini,hukata tamaa lakini ukijitambua hutakata tamaa kamwe,kwani utatambua kuwa ni Mungu na wewe ndiye uliyetumaini juu ya yote...Hutaweka matumaini kwa wengine tu,bali utajifunza kuwa wewe ndiye unayepaswa kuchukua hatua juu ya maisha yako.
Maumivu tuliyopitia hutupatia juhudi mpya na uwezo mpya.Yote wanayokunenea wengine hayatakufanya uwe vile wanavyotaka ama kudhani kuwa utakuwa hivyo,bali uamuzi wako utayainua ama kudidimiza maisha yako mwenyewe.Utaacha aibu na woga wa kufanya jambo kwa kuogopa kuwa wengine watakucheka ama kusema vibaya juu yako.Jibu kwao ni mafanikio utakayoyapata,ambayo yatawafunza wao pia.Hutajiona kuwa hustahili kuwa unavyopenda,bali sasa utaamua na kujipenda,ukiishi kwa ajili ya wengine pia
Kila jambo huwa na sababu ya kutokea,ukitazama yaliyopita kwa moyo mweupe,utafurahi kupita huko,kwani ndiko kunliko kuinua na kukufanya uwe imara zaidi..Ndipo sasa utakapoanza kujitazama upya na kujipenda jinsi ulivyo,jinsi ulivyoumbwa,na si jinsi wengine wanavyotaka uonekane....usiwaache wengine wakuchagulie maisha yako...usiache yaliyopita yakakuchagulia jinsi utakavyokua.
Tazama ulivoshinda vikwazo,kisha chukua nguvu ya ushindi wako na songa mbele.Unaweza na maisha yanaendelea.Amka...songa mbele

AHSANTE WOTE


Rafiki wa kweli ni yule ambaye unaweza kumwamini,ni yule ambaye unaweza kumshirikisha furaha,huzuni na kila tamanio la moyo wako,ni yule ambaye hakuhukumu kwa kufikiri tu,ama kusikia toka kwa wengine,ni yule anayekubali na kuheshimu maamuzi yako,uchaguzi wako na uhuru wako,ni yule ambaye yupo tayari kutumia alichonacho kwa ajili yako,ni yule anayeweza kukukosoa na kukufanya utambue njia bora na kukua ukiendelea mbele daima,hutambua umuhimu wako na kukupa moyo,kukuamsha uwe bora zaidi na kufikia mafanikio,Hukusikiliza na kukushauri pale panapostahili na unapohitaji...daima huwa kwa ajili yako..rafiki wa kweli hawezi kuwa na ajenda za siri,hawezi kukuzunguka n A KUKUSALITI...rafiki wa kweli hufurahi pale unapofanikiwa na si kuweka kinyongo na kuumia pale unapofanikiwa,daima huwa pamoja nawe......na ni furaha kubwa pale unapogundua kuwa rafiki yako mkuu ni wewe mwenyewe....furaha pia ni kumpata rafiki wa kweli ..ni wachache....daima nafurahi kupata marafiki wa namna hii..nitakuwa sina fadhila kama sitasema ahsante itokayo katika furaha ya moyo wangu

Tuesday, August 28

TUNAENDELEA MBELE

KATIKA MAISHA TUNAPITIA MAGUMU.....tunapitia kuanguka mara nyingi...tunapitia kukatishwa tamaa,kusengenywa,kutengwa na hata kudaharauliwa.....tunapitiwa kuumizwa katika mahusiano,kuachwa,kudhulumiwa nk...haya yote hayana budi kutokea,jambo la muhimu ni kuwa tunavumilia yote na licha yakuwa tumeanguka mara nyingi,lakini pia tumesimama mara nyingi zaidi...na ndio maana tunaendelea na maisha kama ili

vyo kawaida,tunaendelea kuandika,kuwaelimisha wengine,kuwaburudisha wengine na kuwafariji wengi....tunayafahamu maisha,tunajua kuwa kama tutakata tamaa tutakuwa tumejidharau wenyewe,tumejiangusha wenyewe,tumejisengenya wenyewe na tumejidhulumu wenyewe.....
Hatukati tamaa kamwe
“Tunasikiliza mioyo yetu,kwa sababu hutupatia mwongozo wa maisha kila kukicha,hutukumbusha kuwa haklisi...hutukumbusha kuwa tupo kwa ajili ya wengine....hutukumbusha kuwa dunia inatuhitaji....hutukumbusha kuwa sisi ni zaidi ya tujifikiriavyo...sisi ni bora kama tulivyoumbwa

Monday, August 27

NAFASI YAKO HAPA DUNIANI NI YA MUHIMU SANA

Kwa sababu kila mmoja wetu anahitaji kuthaminiwa,kuheshimiwa na kila mmoja anahitaji kuona wengine wanamjali....mioyo yetu haiwezi kuwa na furaha ya kweli kama hatutakuwa sauti kwa wale ambao wanataka kusema lkn hawapati japo nafasi....kuwa faraja kwa wale wenye machozi,kuwa mwangaza kwa wale wanaohitaji nuru ya kuamsha mioyo yao na ari ya kuyaishi maisha yao....tutakapokuwa nguvu kwa wanyonge,na zaidi..kuishi kwa ajili ya wengine

Haujatokea duniani kama bahati mbaya,ama pasipo lengo,lipo lengo....nalo ni kuishi lengo hilo ili nuru ya Mungu iliyopo ndani mwako ionekane ,Bila wewe kuwepo na kuishi maisha yako,lipo jambo ambalo halitakuwa vile linatakiwa liwe,upo kwa ajili ya kuiangaza dunia...wewe ni mwanga...wewe ni chachu ya maendeleo ya dunia hii....si nyota,wala jua,wala miti,wala majani ,wanyama kila uoto ambao unakukosa pale unapokuwa upo duniani pasipo kutenda jambo lililokuleta.....nafasi yako wewe haijazwi na mtu yeyote mwingine,ndio maana umeletwa hapa duniani....amua kutimiza lengo lililo kuleta,viumbe wote wanakuhitaji....ishi kwa ajili ya wengine,wauone upendo,waione amani,waijue faraja,wafahamu kujitolea...na haya yote yanatoka kwako wewe..wewe ni wa pekee


 

Saturday, August 25

WEKA JUHUDI KUJITAMBUA WEWE KWANZA

Wapo watu wanaofikiri kwamba yupo mtu ambaye anahusika juu ya uchaguzi wa wanataka kuwa nani,na kuishi maisha ya namna gani...Wapo wanaofikiri kuwa wenzao ni bora kuliko wao...Wapo wanaofikiri kuwa upo wakati utafika watabadilika tu katika kufikiri,kutafakari na kufanya maamuzi pasipo kuweka juhudi binafsi.Nikupe siri moja katika kutafuta mafanikio,jiulize unataka maisha ya namna gani,uishi vipi maishani....jiulize kila mara kabla ya kulala,na baada ya kuamka,jikumbushe ....kila siku mpaka pale moyo wako na nafsi yako itakapofanya kuwa kanuni ya msingi,kisha chukua hatua pasipo kutazama pembeni ama wanaokutazama....Acha uiga wengine...wewe ni wa pekee na nafsi yako...maisha ni mwanga,fuata mwanga wako..acha uoga...chagua ujasiri ....amka ,chimba ndani ya moyo wako,chimba ujitambue wewe ni nani.

Wednesday, August 22

TUNAPATA KILE TUTOACHO

Nakusihi usome kwa makini makala yenye kichwa cha habari.JINSI GANI TUNAPATA TUWAZACHO hapa http://pongujoseph.blogspot.com/2012/07/ni-jinsi-gani-tunapata-tuwazacho.html   kabla ya kusoma makala hii..
   Kabla ya kueleza kanuni hii...nitoe mifano miwili

          Kwanza kabisa...tafakari pale unapokuwa na rafiki yako...unapomtendea jambo la kumuudhi....hukasirika,akasirikapo huchukia ,na chuki aliyonayo huweza kumfanya akakutendea pia jambo mfano neno baya ,na kisasi.....kifuatacho ni kwamba wote huwa mnakuwa katika hali ya kutokuwa na furaha,.Hata kama yule umtendeaye ubaya atanyamaza pasipo kukutenda lolote....wewe utabaki na wasiwasi na huzuni
         Pili,upo na mwenzako,katika hali ya kawaida....ukamchekesha....kitendo cha kumchekesha husababisha atabasamu ,kutabasamu huamsha furaha katika moyo wake.....nawe uliyechekesha utacheka na kuamsha furaha moyoni mwako.....
   Ni sawa na pale mtu anapopiga miayo....unapomtazama nawe pasipo shuruti unapiga miayo

unapotoa upendo,unapata upendo uleule ulioutoa
                   

                  Mifano hiyo hapo juu inatueleza jinsi gani pale tunaposababisha jambo fulani kwa wengine,basi jambo hilo huturudia sisi wenyewe.Sisi ni matokeo ya nguvu,sisi ni nguvu..kila tunachokitoa ndani mwetu ni nguvu...upendo ni nguvu,chuki ni nguvu,mawazo ni nguvu ,furaha ni nguvu....Ipo kanuni ambayo ilitolewa na mwanasayansi mkongwe,Isaack Newton,inayosema..kwa kiingereza, to every action there is equal and opposite reaction---kwa tafsiri isiyo rasmi ,kwa kila tendo /jambo litokealo/lisababishwalo...basi huwa na kinyume chake kilicho sawia na jambo /tukio/tendo hilo.
                       Hivyo kila tunachokiwaza,tunachokitenda dhidi ya wengine...basi hutokea kwetu wenyewe...ukiwafanyia wanaokuzunguka kwa upendo,nawe upendo utakurudia,ukitoa pasipo vikwazo nawe pia utapata pasipo vikwazo...ukifurahi na kutamani wengine wafanikiwe kupitia wewe basi,mafanikio unayoyatoa kwa wengine huja kwako.......
                Hivyo basi,hapa tunapatas kanuni ya pekee ambayo inatusaidia kufanikiwa katika maisha tunayoyaishi,ya kwamba...mafanikio huja pale unapokuwa sababu ya wengine kufanikiwa,unapofanya juhudi maishani mwako kuwainua wengine,ndivyo nawe unapoinuliwa,ndivyo unavyofungua milango ya mafanikio kwako.Ukifanya chuki,chuki hukurudia siku moja......majuto huwa ni sehemu ya maisha yako

   

Saturday, August 18

simama kwa ajili ya wengine

Kila mmoja anacho kipaji chake...haijalishi mzee ama kijana...simama kwa ajili ya wengine..wapo wahitaji,wanyonge,walioshuka moyo..wapo waliokata tamaa,simama kwa ajili yao...unaweza kuhisi kuwa wewe si lolote ..lakini ukisimama kwa ajili ya wahitaji.....utapata furaha isiyo kifani.....natamani sana kuona maisha ya wengi ya kibadilika...ninaweza kuwa sina fedha lakini daima nitakuwa chanzo cha wengine kuamka na kusimama...wewe unajisikiaje?

 Ninaishi maisha yangu,lakini nikiwatazama walionizunguka,moyo wangu unapata faraja kuwaona wakifanikiwa....nipo kama mimi,lakini nikisimama kwa ajili ya wengine.......nimesimama nikiwa peke yangu lakini kwa kujitolea kwa wengine nasimama kwa mamiolioni...tujitolee maisha yetu kwa ajili ya wengine

Friday, August 17

THAMINI WANAOKUZUNGUKA.

    Nimefanya utafiti na kupata matokeo kwamba katika Jamii nyingi za waafrika,wengi huwa hawapendi kuona wenzao wakifanikiwa..Mtu huchukia kuona mwenzake kaanzisha biashara,kapata ajira,kagundua kitu kipya,yaani kwa kifupi wengi huingiwa na chuki kuona wengine wakinyanyuka.Mfano,mpogoro yupo radhi kumfanyia fitina mpogoro mwenzake asiendelee,Mbena atamfanyia fitina mbena mwenzake asiendelee....msukuma atafanya kila awezalo kumrudisha nyuma msukuma mwenzake.
     Katika utafiti huu,nilipata maoni tofauti pamoja na mifano lukuki ya jinsi jamii ya kiafrika tunavyofanyiana fitina sisi kwa sisi(roho mbaya).Mzee  Mkiki ,anasema ameshuhudia chuki na visa vingi alipoanza kujenga nyumba ya kisasa (ya bati),wapo ambao waliapa kuwa watahakikisha kabla hajahamia katika nyumba ile basi atakuwa amedondoka....kwa hofu yake aliamua kusitisha ujenzi.....Rafiki yangu mmoja niliyesoma nae shule Mazengo,alinisimulia jinsi ambavyo wale aliokuwa akidhani ni marafiki wake wakubwa ,walipooneshwa kutofurahi pale alipofanikiwa kusimama mwenyewe katika biashana na hata kuanza kujenga....anasimulia kisa hiki ambacho kiliambatana na marafiki wake kumsengenya na hata kushirikiana na wahalifu kumuibia,ili mradi tu arudi nyuma....bila shaka hata wewe unao ushuhuda
     Sababu kubwa ya roho mbaya hii ni elimu duni...hasa ya kutojitambua..Hatutambui kuwa kila mmoja wetu analo jukumu la kutimiza hapa duniani...Na kila tukifanyacho huwa eitha kinaweza kubomoa ama kuwajenga wengine,kulingana na uchaguzi wetu,......Tupo kwa ajili ya wengine....kila mmoja anamtegemea mwingine katika kuifanya dunia hii kuwa sehemu bora...
      Sisi hatuwatazami wengine,tunatazama tu nafsi zetu,.Hatujui kuwa maendeleo ya wale wanaokuzungiuka ni maendeleo yako,hatutambui kuwa chuki hufunga milango ya mafanikio yetu wenyewe.
   Hatupo tayari kujua wala kujifunza ushirikiano,hatupo tayari kujifunza wengine wamefanikiwaje!hatupo tayari kubadili maisha yetu....tumekuwa tukiendeleza chuki badala ya upendo,tukiendekeza majivuno,visasi na choyo..hatuwathamini wanaogusa maisha yetu..hatuwathamini wanaotuzunguka,hatuthamini michango ya wale waliothubutu kusimama licha ya vikwazo,hatuthamini mawazo mapya,hatuthamini chemichemi za fikra,hatuthamini wazalendo wa dunia hii....hatuthamini wanaojitolea kwa ajili yetu
    Tujiulize,unapoteza nini pale mwenzako anapoushinda umasikini...unapoteza nini pale unapowainua wengine....unapoteza nini unaposimama kwa ajili ya wanyonge.....ni wakati sasa wa kujifunza kuwa mafanikio ya mwenzako ni mafanikio yako......kwangu mimi ninapata faraja ninapoona kuwa ninagusa maisha ya wengine....ninawathamini kila anayenizunguka

Monday, August 13

KUMRADHI

 Karibuni nyote mnaofuatilia blog hii.
 Kwa siku kadhaa nilipata shida kuweza kuandika katika blog hii kutokana na tatizo la kiufundi,akaunti yangu ilipata hitilafu na kuingiliwa,nikapata changamoto katika kuandika......nilikuwa nikiumia kwa kuwa furaha yangu ni kuona kuwa kila mara tunajifunza jambo jipya,ni kuona waliokuwa wanakata tamaa wanaamka upya..ni kuona kuwa wewe na mimi tunakua na kuyafikia mafanikio...
 Changamoto zilizotokea zimenifanya niongeze bidii,bila shaka tutafika pale tunapokusudia kufika

Tuesday, August 7

MWALIMU BORA

Wale waliopitia ugumu ,milima na mabonde katika maisha yao ni walimu bora,kwa sababu wanajua maana ya kila jambo walilolipitia,wanajua jinsi gani ya kubomoa ukuta wa mipaka ya kufikiri,wanajua kuumizwa,wanajua faraja,wanajua chuki,wanajua amani,wanajua upendo,wanajua kila jambo walilolipitioa si kwa kusoma nukuu tu,bali kwa kuishi na kupambana na vikwazo...wanatambua kuwa hakuna njia ya kupambana na woga zaidi ya kuamua kutenda unachokiogopa,wanatambua jinsi ya kufungua minyororo inayotuzuia kuyafikia mafanikio,hawa maisha yamewapa changamoto,maisha pia yamewapatia baraka tele...wamepata majaribu,wakayapita,wamepata maumivu,wakaendelea kusimama imara ,watu waliwakejeli,waliwaumiza na wengine waliwapa faraja...waliamua kuacha yaliyopita na kusimama tena kwa ushindi,wakachagua kuwa washindi,wakaishi maisha yao kwa ajili ya wengine pia,woga wao ni kuogopa kutenda wanapotakiwa kutenda..wamekuwa mifano bora katika jamii,wanatambua kujitolea ,hawa ni mashujaa ambao nuru ya maisha yao itaishi milele.Ni wakati sasa wa sisis kutoogopa kushindwa na kuamua kudiriki kutenda.

Sunday, August 5

KILA JAMBO LITOKEALO LINA SABABU, KILA JAMBO HUTUFUNZA

     Ni  kweli kwamba kila changamoto itupatayo huwa na sababu...na huwa ni wakati wetu kujifunza mbinu mpya za kufikia pale tunapohitaji kufika...wakati mwingine tunajifunza kutoshikilia sana mambo ambayo yanatuchelewesha kufika tuendako....wakati mwingine tunakumbushwa kuwa kila mlango mmoja ufungwapo,basi hutoa nafasi kwa milango mingine mingi na madirisha kufunguliwa ,na hivyo,waweza kukata tamaa,kwa kutokewa na changamoto,kumbe changamoto hiyo ndiyo inayokupa njia mpya
    Si lengo langu kuandika mambo yanayonihusu mimi,ama watu fulani...kama ilivyo ada,blog hii ni mahali pa kukufanya ujitambue wewe ni nani,uweze kufungua minyororo ambayo inakuzuia kuyafikia mafanikio
    Wikiendi nilikutana na rafiki yangu ambaye ameumizwa sana katika masuala ya mahusiano...kuumizwa huko kumemfanya ajihisi kuwa hana thamani,ana matatizo.....hajiamini tena na daima anashuka moyo,amekata tamaa na kuapa kuwa hatapenda tena...baada ya kuongea naye sana,alitokea kukubali kuwa hayo yalitokea,yamebaki historia.....anasimama tena na kusamehe,akianza maisha mapya.Amekubali kuwa aliumizwa,lakini yote hayo hayatamfanya ashindwe kuishi maisha mapya,amaetambua kuwa yeye ana jukumu juu ya maisha yake,hakuna anayeweza kumpangia maisha yake yajayo,bali ni yeye,yaliyopita yamempa nguvu ya kusimama na kukimbia kwa kasi zaidi




  CHANGAMOTO ZINATUKUMBUSHA KUWA NI VEMA KUTAZAMA KILA JAMBO  KUWA NI KUFUNZI
    Lipo somo kubwa tunajifunza hapa......nakusihi usome kwa makini maneno haya chini,ambayo rafiki yangu huyo,aliyaandika baada ya kujitambua,toa pia maoni


Kuachana nawe kumenifunza jinsi ya kuwathamini watu wengine,kuwapenda hata pale panapoonekana ni vigumu, kumenifanya nijifunze kuwa mimi sipo tu kwa ajili yang u,bali kwa ajili ya wengi,hivyo,maisha yangu yana sababu kubwa hapa duniani,nimejifunza kuwajibika na kujitolea kwa wale wote ambao jamii haiwathamini—wafungwa,yatima,wajane na wote ambao hawana tumaini la kusimama tena,nimetambua kuwa sisi sote ni wamoja,uadui huletwa na wale wasiojitambua,wanaofikiri kuwa dunia
hii ni sehemu ya ushindani badala ya ushirikiano,wanaodhani kuwa wao ni bora kuliko wengine...nimejifunza kuwa ni furaha katika kutoa kuliko kupokea,nimejifunza kuwa hata kama binadamu atakuwa amekosa viungo vya mwili,sura nzuri,mavazi,fedha ama umaarufu,lakini bado ni binadamu mwenye thamani kubwa,kwani thamani ya binadamu ni zaidi ya sura,umbo,mali,umaarufu,hivyo nitawatazama binadamu wote kwa usawa na kujitolea kwao kwa usawa,nimejifunza kuwa sipaswi kutazama changamoto kwa upande hasi,bali nitazame daima kwa mtazamo chanya,na mwisho,nimejifunza kusimama mwenyewe,na kumshukuru Mungu,nikimsihi anitumie daima kwa ajili ya  w engine…Amina (Pongu)

  

Saturday, August 4

TUJIKUMBUSHE SISI NI NANI.


     Kwa kipindi hiki cha mwisho wa wiki,ningependa tujikumbushe sisi ni nani,anza na wewe,
 Kaa sehemu tulivu,kisha funga macho,vuta pumzi taratibu ,sikiliza na kufuatilia mapigo ya moyo wako,kisha jiuliza maswali yafuatayo
  1.  mimi ni nani?
  2. kwa nini nipo hapa duniani
  3. je ni kwa kiasi gani nimetimiza jukumu langu la kuwepo hapa duniani?
  4. je ninajipenda na kujithamini kwa jinsi nilivyoumbwa?
  5. je,nitakapokuwa tayari kumaliza maisha yangua hapa duniani,ni jambo gani la msingi litakalo nipa furaha na kumbukumbu kwa wengne?
  6. je nimekuwa faida gani katika dunia hii?
  7. kama bado sijafanya chochote,ama siridhiki na maisha niyaishiyo,ntabadilika?lini?kama sio sasa,ni nini inanifanya nisiamue?
  8. je maisha ninayoyaishi si ya bandia?



Tuesday, July 31

UPENDO,NDOA NA SHERIA

Mwisho wa makala hii utapata kujifunza mambo yafuatayo
  1. ni nini na jinsi gani upendo wa dhati
  2. HOFU-ADUI MKUBWA WA UPENDO
  3. ndoa,furaha,na huzuni katika ndoa-sababu
  4. sheria katika upendo na kushindwa kwa sheria kulinda ndoa
  5. jinsi gani utaishi maisha ya furaha katika ndoa
  6. nafasi yako katika upendo,ndoa.
  7. jinsi ya kuifanya ndoa yako idumu na kuwa na mafanikio kila kukicha
  8. jinsi ya kutazama kila jambo katika mfumo chanya na kubadili maisha yako

                                  UPENDO
 


     Upendo ni mvuto wa asili(nguvu ya asili) usio na shuruti kati ya mtu mmoja na mwingine.Ni lugha ya pekeee ambayo kiziwi,kipofu,mtoto,mzee, na kila kabila huisikia.Ni lugha ya moyoni..Ni NGUVU PEKEE INAYOTIBU,INAYOWEZA KUAMSHA WASIO NA TUMAINI,INAYOONDOA CHUKI,(UPENDO HUSHINDA YOTE).Upendo ndio ishara kuu ya Mungu(MUUMBA-ASILI YA VIUMBE VYOTE),,ni faraja,amani,ni tumaini...Ndio maana katika maandiko toka katika biblia tunaelezwa ya kuwa Mungu ni upendo
       Mara nyingi tumekuwa tukigawa aina mbalimbali kutokana na mazingira yetu na fikra zetu na kupata upendo wa dhati,upendo wa kawaida,lakini ukweli ni kwamba upendo unabaki kuwa ni upendo(unapopungua huo si upendo) na kinyume chake (chuki) inabaki kuwa chuki.Huwezi kusema kuwa unao upendo pasipo kuuishi/kutenda mambo yanayodhihirisha upendo.Upendo ni kutazama kwa huruma,upendo ni kuinua walkio chini,upendo ni kujitolea pasipo kuhitaji malipo,upendo hushinda yote.  
       Kama tulivyyoona hapo juu,upendo ni msukumo wa kiasili kabisa.Hutokana na mvuto wa asili utokao moyoni kwa mtu,na ndio maana nikauita upendo kuwa ni lugha ya moyoni.Kwa sababu ni mvuto wa kiasili,upendo haujengwi wala kulindwa na vitu visivyo vya asili.Fikra zetu zimejengwa kuutazama upendo katika mtazamo wa vitu ama mali.Mvuto huu wa asili huwa haujali rangi,dini,tofauti ya kimawazo ama mtazamo,haujali tofauti za taifa,ukanda ama lugha,kabila,haujali mali wala hali.Ni ukweli usiopingika kuwa kila mtu huweza kumpenda ama kuvutiwa na mwingine si kwa sababu ya dini,ama rangi,ama kabila,ama utaifa fulani,ama mali.....fikra za dini,mali,kabila,taifa huja kwa msukumo wa fikra(zenye athari ya kimazingira) na tamaa.
      Kwa maana hiyo,sitakuwa nakosea nikisema kuwa,upendo (mvuto wa asili) kwa sababu ni asili ya moyo,basi ukitazamwa kwa mtazamo wa vitu visivyo asili(vitokanavyo na fikra za kimazingira) basi huwa si upendo tena bali huwa ni tamaa na udanganyifu.Upendo hauwezi kulindwa kwa sheria,hakuna sheria itakayotungwa kuulinda upendo kati ya watu wawili,na sheria hiyo ikashinda isipokuwa tu,upendo wa dhati hutoka moyoni mwa kila mmoja,nao hudumu na kutukuka toka moyoni mwa wawili hao na ndio maana,tutaona hapo mbele ya kuwa sheria imeshindwa kulinda ndoa na badala yake baada ya sheria kuwa ndio mlinzi wa upendo,ndoa nyingi zimekuwa zikivunjika(zipo sababu nyingine ndogo)
  Tumezaliwa tukiwa na upendo,lakini mitazamo yetu ya kifikra imefanya tuweke matabaka katika upendo,na hivyo hofu imetawala upendo,na kufanya hofu kuwa adui mkubwa wa upendo.
                                                Hofu,adui wa upendo(picha kwa hisani ya mtanzdao)
    Ni hofu ndiyo inayoleta chuki,hofu humfanya mtu kutojiamini na kuhisi wanaomzunguka ni maadui...Ni hofu ndiyo iliyosababisha viongozi wang'ang'anie madaraka,kufanya mauaji,kubagua..Ni hofu ndiyo  inayojenga uhasama.
                              
               NDOA
        Kila unapofikiri kuhusu mwenzi wako,umefikiri kuhusu wewe,unapomtendea mwenzi wako unajitendea wewe,unapomjali mwenzi wako umejipenda mwenyewe,unapomfanya mwenzi wako afurahi umejitendea wewe,upendo hutoka ndani ya moyo wako mwenyewe...pale unapovutiwa na mwingine...pasipo shinikizo litokalo nje ya moyo wako...ukamchagua na kuonesha nguvu hii ya asili kwake,ukishirikiana nae kukua na kuyafikia matarajio ya kila mmoja wenu,hii huitwa ndoa.Ndoa si kupata mwenza ambaye atakufanya uwe kamili(kwa kuwa kila mmoja amekamilika vile alivyo), ni urafiki na upendo uendao mbele ya maumbile.Ndoa ni muumngano wa wawili kila mmoja kwa ukamilifu wake,kwa ajili ya kufanya nuru ya Mungu ambayo ipo kwa kila mmoja,ing'ae kwa kila mmoja ili kuwafanya wawili hao na wale wanaowazunguka waujue utukufu wa Mungu
 Nimetazama ndani yangu na kuuona ukamilifu wangu,nami naungana nawe ili mimi nawe tushirikiane ukamilifu wetu(tafakari kwa kina)
            muhimu:wengi hufikiri kuwa hawajakamilika,wamekosa kitu fulani,na hivyo huingia kwenye ndoa wakitazamia kukipata kitu fulani toka kwa wenzi wao,baadae hugundua kuwa wanachokitafuta hakipo kwa wenzi wao,hapo ndipo matatizo huanza kutokea kwenye ndoa....baada ya changamoto nyingi ,wengine huomba Mungu awabadili wenzi wao,hawatambui kuwa ni fikra zao ndio adui wa ndoa yao(fikra huleta hofu)-(kama wangetambua wangemuomba Mungu abadili fikra zao.-hata ndoa kuvunjika,hutambua kuwa kumbe furaha,amani,upendo,kujali..kunaanza ndani mwao.
               Ndoa ni mungano ambao kila mmoja katika wenza huhakikisha anatumia kila alichonacho kuhakikisha kuwa mwenzi wake anakua na kutimiza yale aliyoyakusudia katka maisha yake.Ni mahali ambapo chemchem ya amani ilipo,ndoa si kifungo...ndoa ni chimbuko la uhuru ,ndoa si hofu,bali ni chemchem ya upendo,umoja na amani,ni mbegu iletayo matunda bora,ndoa ni ishara ya kukubali majukumu,ni chimbuko la kuifanya dunia kuwa sehemu bora
              Kinyume chake katika dunia ya sasa,ndo imekuwa ni sehemu ya watu kukimbia majukumu,ni sehemu ya watu kukwepa kufikiri,kuamua na kutenda...ndoa imekuwa ni sehemu ya mmoja kuweka matarajio dhidi ya mwenzi wake......tamaa ya kupata mali,kupata sifa ndio imekuwa msukumo wa watu kuingia kwenye ndoa...na kwa sababu ya hofu ya kukosa matamanio ama matarajio haya......mwanadamu akabuni sheria mabyo inamuhakikishia kuwa\ anatimiza matamanio yake......na kutengeneza sheria.....ya kwamba kila anayeingia katika ndoa basi huweka kiapo cha lazima(na kuifanya ndoa kuwa shuruti ya kisheria).Swali ni je,upendo (usio na shuruti) unaweza kulindwa kwa shuruti(sheria)?
               Kuingizwa kwa sheria(kiapo_katika ndoa ni dalili tosha ya kuwepo kwa hofu kati ya wawili waliopendana.Ni dalili ya kutoamini mioyo yao .Ni matokeo ya kutazama ndoa katikamisukumo ya hali na mali...gari,fedha,nyumba,ardhi,umaarufu...Matokeo yake ni kwamba mmoja kati yawenzi hawa huwa mtumwa na mwingine huwa mtwana...Hofu ndio msingi wa ndoa ya kisheria.....upendo hushinda yote..Mpendwa msomaji,jiulize ni kwa nini,watu wawili waliokutana wao wawili,wakathaminina na kupendana,huweka kiapo na kuandikishana kisheria.....je kiapo hiki huwasaidia kukua na kupendana pamoja? 
               Hivi majuzi nimesoma ripoti moja kuhusu ndoa duniani,ikionesha kuwa kuvunjika ndoa kumeongezeka sana toka katika karne ya kumi na tisa na sasa kasi ni kubwa sana..Sababu si ugumu wa maisha,sababu si utandawazi...sababu nimekwisha ieleza,ni fikra zetu na msukumo wa kuingia katka ndo kwa msukumo wa mali na hali,kwa matazamio ya kupata kuliko kutoa,sheria ikiwa ndio chimbuko lake
               KWA mtazamo wangu mimi upendo ,ni mvuto asilia...huvumilia,hujali,huthamini..na ndoa iliyojengwa katika upendo,hukua,tena pasipo kiapo kanisani ,msikitini,ama kwa mkuu wa wilaya,kila mmoja huishi kwa furaha ndani ya ndoa hii,kila mmoja huona fahari kuona mwenzi wake akikua nakutimiza ndoto zake....lakini ndoa itokanayo na msukumo wa kisheria...hujengwa katika tamaa,majivuno,hofu,kisasi...na kila mmoja hujitazama yeye anapata nini,mmoja huwa mtumwa na mwingine huwa mfalme.Hawa kinachowaunganisha ni sheria,(hofu) bali waliopendana kwa dhati upendo huwaunganisha.
 sisi twapendana kwa dhati.....kwetu thamani si magari,fedha,ufahari,umaarufu....sisi huvumilia,upendo hushinda yote
          Hivyo ,ni wazi kuwa ili uishi maisha ya furaha katika ndoa, unapaswa kufanya mabo yafuatayo
  1. Kubadili fikra zako,ya kuweka mategemeo ya kupata kitu fulani toka kwa mwenzi wako,kisha anza kutazama kwa mtazamo chanya,jitolee,timiza jukumu lako,daima kumbuka kuwa wewe una jukumu la kumfanya mwenzi wako akue na kutimiza malengo yake maishani,hivyo ni wakati wa kuacha kuomba tu Mungu ambadili mwenzi wako,bali muombe abadili fikra zako.
  2. Ondoa hofu,toa hofu juu ya mwenzi wako kuwa atakusaliti,atakuumiza,..anza kumtazama kwa wema,mfanye aamke na kutambua wajibu wake,hofu hupelekea kujaa wasiwasi na kufanya maamuzi yasiyo na manufaa.
  3. Zipo nyakati mbalimbali katika maisha,kuna wakati wa shida,raha......uvumilivu utokanao na upendo hurejesha matumaini..hivyo jipende wewe,kisha jifunze kumpenda mwenzi wako kama unavyojipenda wewe
  4. Tumezungukwa na jamii yenye maoni tofauti,sikiliza sauti ya moyo wako.....kama unaingia katika mahusiano kwa kusikiliza ushauri ama maoni tu ya wenginme pasipo kuchunguza na kusikia moyo wako,unatengeneza njia ya maangamizi yako mwenyewe,kama utambagua mytu kwa sura,umbo,rangi,kabila ama hali,basi umejibagua mwenyewe toka moyoni mwako
  5.  
       
      unapomsikiliza,kumthamini na kumjali mwenzi wako licha ya mapungufu ya kimaamuzi,hujenga ndoa imara na yenye furaha
     upendo hautazami nini mimi ninapata,bali mwenzangu anafanikiwa vipi kwa uwepo wangu



  Kuna rafiki  yangu alikataliwa kuoa kwa sababu ya kabila lake,akiambiwa kuwa 'mtoto wetu hawezi kuolewa na kakabila hako,labda ungekuwa umesoma sana maana sisi kabila letu ni wasomi,yupo ambaye aliwekewa pingamizi eti kwa sababu ya tofauti ya dini,....waliofanya hivi husukumwa na mali na hali.....upendo haujali dini,kabila wala hali........Kama hatujajitambua,basi migogoro katika ndoa haitakwisha kabisa....tafakari njema
 
     
   
      

DUNIA INAKUHITAJI

 dunia inakuhitaji uwatazame wenzako kwa huruma,ukijali mahitaji yao,ukiwainua na kuwafanya wajitambue na kujikwamua(picha kwa hisani ya www.viewtz.com)
DUNIA HAIITAJI WATU WENYE FEDHA NYINGI,MAGARI,NYUMBA,NGUO NYINGI AMA WENYE UMAARUFU MKUBWA..DUNIA INAHITAJI WATU WENYE KUJITOLEA KWA WENGINE,WENYE UTAJIRI WA UPENDO,WENYE KUUGUZA,KUPONYA,KUAMSHA MATUMAINI YA WALIOKATA TAMAA,WENYE KUSAMEHE NA KUTAZAMA UPYA KWA UPENDO,WENYE KUPIGANIA UHURU ,WENYE KUJALI NA KUTETEA WENGINE.,WENYE KUTENDA YALE YANAYOONEKANA HAYAWEZEKANI,..DUNIA INAKUHITAJI WEWE KWA YOTE HAYA.CHUKUA HATUA
 tunapaswa kuwapenda wengine ,kuthamini changamoto zao na kuthamini mawazo yao ,kuwa tayari kujitolea pasipo kujali rangi,kabila,dini,taifa.picha kwa hisani ya helped by animals
 

SONGA MBELE.







 KAMA HUWEZI KUPAA,USILALAMIKE,...KIMBIA,  KAMA HUWEZI KUKIMBIE USIKATE TAMAA,TEMBEA......KAMA HUWEZI KUTEMBEA USIBAKI TU UNALALAMA, TAMBAA,ILI MRADI TU KILA SIKU UNASONGA MBELE

Saturday, July 28

AMUA KUBADILIKA AMA KUBAKI ULIVYO


 ni wewe unaeweza kuamua juu ya kubadilikakuyaendea mafanikio AMA kutobadilika na kubaki ulivyo(picha kwa hisani ya mtandao)
           
          Ni wazi kuwa unatambua kwamba nazungumzia kuhusu kufanya mabadilko ili kuyafikia mafanikio uliyoyakusudia.Mafanikio kwangu nina maana ya kutimiza jambo lolote lile ambalo umepanga kulifanya maishani mwako,ambalo linakuletea furaha moyoni mwak Kila mara tumekua tukisubiri kuchukua hatua ya kubadilika,tumekuwa tukitarajia tutabadilika baadae,kesho,wiki ijayo,mwezi ujao ama mwakani,lakini hakuna wakati zaidi ya sasa,yaani wakati uliopo.Usisubiri kesho ama mwakani,kila jambo lipo mikononi mwako,ni wewe tu kuamua.Na pale tu utakapotambua sababu ya wewe kuishi,ndipo utakapoanza hatua kubwa kuelekea mafanikio.
            Tunao pia uwezo wa kuamua kutofanya chochote,kuamua kubaki tulivyo,kubaki na umasikini wetu,kubaki na malalamiko yetu,kubaki na huzuni zetu...tunao uwezo huu.Tunaweza pia kujifanya tumeamua kubadilika,hasa pale ambapo hatujitambui...tutajifanya tumebadilika ili kuwafurahisha watu fulani,kwa uoga wetu...Tunaweza kuamua hili.Tunaweza kuamua kukaa tu pasipo kazi,tunaweza kuamua kuchagua ujinga badala ya kuelimika, tunaweza kuchagua kuamini uzushi  dhidi ya ukweli,,kuchagua woga dhidi ya kujiamini,yoote haya ni uchaguzi wetu.......Tunaweza kujikumbusha toka kwa Shakespear,ambaye alisema(kwa tafsiri isiyo rasmi)kwamba 'suluhisho la matatizo ytu na maamuzi yetu halipatikani juu,kwenye nyota,bali ndani yetu wenyewe 
          Tunayo jukumu na maamuzi juu ya uchaguzi wa maisha yetu wenyewe,ili kuandaa maisha bora kwa ajili yetu kesho na kwa ajili ya wengine.....na maamuzi haya yanaanza sasa.Anayetafuta mafanikio hatafuta miujiza wala maneno mengi,bali ni msukumo wa maamuzi unaotoka moyoni,kutenda kwa ukweli na kwa bidii,Anayehitaji mafanikio hatazami nyuma na kukata ytamaa,bali hutazama mbele kwa matumaini,akijitolea nafsi yake yote kutenda.Anatambua kuwa hakuna muda wa kujadili afanye nini,wa kujadili mambo yaliyopita,bali kwake,hutazama kufanya tofauti na mawazo ya wasio liona tumaini jipya,wasiouona ushindi mbele...
                  Kwa yeyote anayehitaji mabadiliko katika maisha yake,kama unaona unachokifanya hakibadili maisha yako,badlika ukitazama malengo yako...wewe si jiwe,una akili na uwezo,amua kubadilika sasa.


 ni maamuzi yako kuchukua hatua ama kubaki ulivyo(picha kwa hisani ya the rhododendron  walk,George Mark)
     
     Kama utazidi kuzamisha kichwa chako ndani ya maji,ukiwa huna kifaa chochote,basi tambua kuwa huwezi kutambua upo sehemu gani,unakwenda wapi na umefika hatua gani,mpaka pale utakapoamua kunyanyua kichwa na kutazama,..tunafundishwa kuchukua hatua juu ya kubadili maisha yetu wenyewe.Tambua kuwa ili kubadili maisha yetu ,tambua unataka kuwa nani,weka maleno,chukua hatua kutekeleza malengo,amini uwezo wakop na kuutumia,vumilia mpaka mwisho,...wale wote waliofanikiwa walifanya maamuzi,wakachukua hatua kuyatekeleza.Ukiamua,zipo nafasi zisizo na ukomo..chukua hatua ........kila ukitakacho kitakuwa chako.siku njema

Friday, July 27

UTAMBUE UHURU WA KUCHAGUA USIO NA MIPAKA


 BINADAMU TUMEPEWA UHURU WA KUCHAGUA NA UHURU WA MAWAZO USIO NA MIPAKA
                      Kama  unaishi maisha ambayo ni matokeo ya kuchaguliwa na mtu,basi wewe si huru.Kama unafanya jambo mfano biashara ama kazi yeyote kwa sababu tu wengine wanafanya basi haupo huru,unaishi maisha ya utumwa ,ni mtumwa wa maamuzi ya wengine.Je unaishi na kutenda mambo ambayo eitha mama ama baba yako anakusukuma utende?(Sizungumzii kuwa unapaswa kukataa ushauri wa wazazi ama marafiki,namaanisha ujifunze kuamua na kutenda kadiri moyo wako unavyokutuma na si kuishi maisha ambayo unachaguliwa).unapaswa kuwa halisi,kuchagua unachokipenda,unachokikusudia na kuishi maisha yenye sababu itokayo moyoni mwako.Je umeeza kuamua kuwa huru katika fikra zako na kuwa huru katika kuchagua maisha uliyoyakusudia?
          
                  Tumepewa uhuru mkubwa wa kuchagua kila kitu.Mungu aliyetuumba ametupa wa  kuchagua kila jambo pasipo mipaka.....ametupa pia uwezo wa kufikiri pasipo mipaka..na kutafuta suluhisho la matatizo yanayotukabili pasipo  mipaka.Ni fikra zetu wenyewe ndizo huweka mipaka katika uhuru huu wa kuchagua na kufikiri na hivyo tunafikiri kuwa Muumba wetu ametuwekea sheria na mipaka katika kuwaza na kufikiri.(Ni sawa na kusema fikra zetu ndio mpaka(ukomo) katika kuwaza na kuchagua).Tunafikiri kuwa kufikiri  pasipo mipaka ni dhambi,hivyo tunapofikia ugumu katika kutatua matatizo yetu wenyewe na kuchagua,huwa tunaogopa na kudai kuwa 'tunamwachia Mungu' ama' Mungu  ndo anayejua.'
   
                Unapofika hapa duniani unakuwa huru kabisa katika kuchagua.Fikiri kama tungekuwa tuna mipaka,ugunduzi unaofanya tuyatawale mazingira yetu ungepatikanaje?Uhuru wa kuchagua na kufikiri tuliopewa si sawa na uhuru tunaoutengeneza sisi katika maisha yetu ya kila siku wenye vigezo na masharti,uhuru usio kamili.Uhuru huu ni ule ambao wewe binafsi ni mwamuzi wa kila jambo.Nayo nchi hutekeleza yale unayoyaamuru. Muumba anakuwa mtazamaji tu katika kila uchaguzi unaoufanya (na si mwamuzi katika uchaguzi unaoufanya).Kwake kila jambo ni jema(simaanishi utende kinyume na jinsi sauti ya moyo wako inavyokutuma ambako huleta majuto).Hakusukumi wala kukuzuia kuchagua jambo lolote ama katika kuwaza pasipo mipaka.Anataka wewe uchague utakuwa  nani,anataka wewe uchague kile kilicho ndoto yako(chaguo la moyo wako),anataka uwe na uhuru katika kuwaza na kuchagua kutatua ugumu wowote wa kimazingira ili uweze kuitawala dunia na kuifanya kuwa sehemu bora kabisa.Anataka uchague jambo ambalo kila ukiamka  unakua namsukumo wa kulitenda kwa ajili ya utukufu wake  na  kwa ajili ya kila binadamu.Haingilii uchaguzi wowote,hata ule ambao unauchagua na unakuletea matokeo yasiyo mazuri.Huu tunauita kuwa ni uhuru usio na mipaka wa kuchagua na kuwaza.
                
                     Kwa kutambua hili kuwa Muumba wetu katupatia uhuru,wa kuchagua na kuwaza,usio kuwa na mipaka yeyote,ni wazi kwamba mafanikio ama kutofanikiwa kupo ndani yako,furaha ama huzuni ni uchaguzi wako,usawa ama matabaka yanatoka kwako,upendo ama chuki unatoka kwako,kuanguka mna kusimama kunatoka kwako,kuishi  maisha ya furaha ama yasiyo na furaha ni uchaguzi wako,na tukumbuke kuwa kwa kuwa uchaguzi ni uhuru wa kila mmoja,hivyo anayehusika na uchaguzi wako ni wewe mwenyewe.
                   
                  Kama nilivyoeleza hapo awali,fikra zetu wenyewe ndizo zinazoleta mipaka katika kuchagua na kutafuta suluhisho la matatizo yetu wenyewe.Natoa mfano,majuzi nilikuwa nikijadiliana na rafiki yangu ambae tumekua pamoja na kusoma pamoja.Tulikuwa tukizungumza kuhusu suala la ajira,yeye aliniambia kuwa amekuwa akitafuta kazi kwa muda mrefu  sana,na hata kukata tamaa,katika kujadiliana nikamshauri ni vema akaanza sasa kufikiri kuhusu kujiajiri yeye na kuajiri wengine,badala ya kufikiri kuajiriwa tu.Hapa ndipo  palipokuwa na mjadala mkali,kwamba licha ya kusoma,lakini familia zetu hazina uwezo wa  kutupatia mitaji,mimi nikamueleza kuwa mtaji mkuu kwetu sisi si fedha tuliyonayo,bali ni mawazo tulionayo....wazo hili lilionekana kuwa haliwezekani'haiwezekani kujiajiri kabisa....haiwezekani nikafanya kazi mtaani saa na mtu ambaye hajasoma,na ni mpaka miaka mingapi ntafanikiwa'
             
                      Mawazo ya msomi huyu ndiyo adui mkubwa wa yeye kudhubutu kufanya na kuchagua kufanya kile anachokipenda,elimu aliyoipata ni elimu ambayo inamfanya wakati wote afikiri tu kuajiriwa(inamuwekea ukomo katika kufikiri na kutatua matatizo),elimu tunayoipata katika vyuo vyetu na shule zetu ni elimu ya kikoloni,inayolenga kuwafanya watu wawe wafanya kazi wa wengine(kutumika),wawe tegemezi na kwao kufikiri kujiajiri ni kosa kubwa,..elimu hii inafanya fikra zetu ziwe  na mipaka katika kufikiri na katika kuamua.Inatengeneza ukuta mkubwa kati ya fikra zetu na maamuzi.Tusipogundua hili na kubomoa ukuta huu,mafanikio na kutimiza ndoto (matarajio tuliyoyapangilia)

uhuru usio na mipaka,mafanikio yasiyo na mipaka




  uhuru wa kuwaza usio na mipaka,uhuru wa kuchagua usio na mipaka ndio unaoleta ugunduzi katika dunia hii,ndio unafanya binadamu ayatawale mazingira.

uhuru  wa kuwaza usio na mipaka,unaotoka ndani ya mtu mwenyewe umeondoa ule msamiati wa haiwezekani(imposible)
picha zote kwa hisani ya mtandao na fresh mind matter



                              Kumbuka kutumia uhuru huu usio na mipaka kuchagua maisha yako,sikiliza moyo wako,usisikilize sauti za watu ambazo si halisi kwako.U CHAGUZI WAKO BINAFSI NDIO UCHAGUZI WA MUNGU KWAKO (kila ambacho moyo wako hukusukuma kutenda kikuleteacho furaha na amani moyoni mwako,hutoka kwa Mungu,ndio sauti ya Mungu na uchaguzi wa Mungu kwako).Unaweza kuchagua kuamka na kuanza upya baada ya kuumizwa katika mahusiano,ama kuendelea kulala,unauhuru wa kuchagua kuishi maisha yako mwenyewe kwa kufanya unachokipenda,ama kufanya tu kwa kufuata mkumbo,una uhuru wa kuchagua upendo,ama chuki,una uwezo wa kuchagua  mtumwa ama kuwa huru

  mazingira na athari katika fikra na uhuru wa kuchagua
                     Tumezaliwa katika mazingira tofauti,lakini yote yakiwa na misukumo yenye athari katika fikra zetu.Tumezunguka na mazingira yenye umasikini wa fikra ,na umasikini katika uhuru wa kuchagua.Mazingira yetu yanatufanya tuamini kuwa kuna nguvu ambayo inayo maamuzi juu ya maisha yetu,na ni pale tu nguvu ile itakapoamua kutupa uhuru,wa mawazo na kuchagua basi ndipo  tunapata mafanikio,ama kama nguvu hiyo itachagua kinyume basi hutokea.Kumbe ukweli ni kwamba uhuru wa kuamua maisha yetu yaweje,tuishi vipi upo ndani yetu.
                     Tunaaminishwa kuwa pale fikra za moyo wako zinapokusukuma utende kuwa ni shetani,tunaogopa kutimiza kuishi vile mioyo inatutuma,matokeo yake tunaishi kadiri wazazi ama viongozi wetu wa kiimani wanavyotaka, tunaishi kwa hofu maisha yetu yote--(kiongozi bora si yule anayekufundisha utende anavyotaka yeye,bali anayekupa mwanga wa kutambua maisha yako halisi,kuyasikiliza na kuyaishi,ambaye furaha yake ni wewe kuishi kadiri nuru yako inavyokuongoza na si kadiri ya maamuzi yake)
                       Unaweza ukajiuliza maswali ,kwa nini sisi waafrika hasa,hatufanyi ugunduzi,na wala hatuamini katika mambo yetu tunayopanga kuyafanya,tunaamini katika kila jambo ambalo linasemwa na watu toka ulaya na amerika?Ni kwa nini  kila jambo linapotokea linalohusisha uzembe,uvivu na mapango mibaya tunalichukulia kuwa  ni kazi ya Mungu ama shetani/?
  

     ni fikra zako ndizo zinazokuwekea ukomo wa kuwaza na kutenda

                           Jibu umelipata,licha ya kutojiamini katika tutendacho,hatuamini katika uwezo wetu,na imani zetu zilitwazo na mazingira zimetujengea hofu na mipaka,tunajiogopa wenyewe,tunamuogopa Muumba wetu abaye ni rafiki aliye ndani mwetu,na kisha tunaamini kuwa wapo wengine waliobarikiwa kufanya kila jambo kwa ajili yetu,tukiwaabudu hao.(ukimuogopa Mungu  badala ya kumpenda na kumchukulia kama rafiki ambaye wakati wote upo nae,utaishi kwa woga na hofu maisha yako yote,na wala hutapata kujua dhamira yako kuwepo duniani).
ELIMU YAO WALIOTUJENGEA IMETUFANYA TUWE WATUMWA,tumekuwa wafungwa sio kwa kuwa tupo  jela,bali jela yetu ni fikra zetu wenyewe.Namaliza kwa kusema,Tunahitaji watu wanaoutambua uhuru wa kufikiri na kuchagua maisha ,usio na mipaka na hivyo wanaodhubutu kubadili msamiati wa haiwezekani kuwa inawezekana.Wanaoweza kutafuta mbinu mpya(sio zile tu ambazo tumekariri na kuamini hakuna njia nyingine zaidi ya hiyo(hizo)),pasipo kujali kuwa ni mjini ama kijijini,pasipo kujali kuna vifaa ama hakuna,pasipo kujali tumewezeshwa ama hatujawezeshwa,bali katika kila hali ushindi utapatikana......kama wapo walioweza katika mazingira magumu,kwa nini tusiwe sisi,kwa nini tunaogopa kuchukua hatua..kwa nini tunauogopa uwezo wetu......TUSIMAME TUSEME TUTASHINDA




Tuachane Na Fikra Za Malalamiko, Upanuliwe Wigo Katika Ubunifu




Na: Meshack Maganga, Mjengwablog-Iringa.

Rais wa enzi hizo wa taifa la Marekani Theodore Roosevelt (Oktoba 27, 1858- Januari 6, 1919) alipata kusema, “What we need is more people who specialize in the impossible”, kwa tafsiri isiyo rasmi ya Kiswahili ni kwamba, “Tunachohitaji ni watu wengi zaidi ambao wamebobea katika kufanya mambo yanayoonekana ama kudhaniwa kuwa hayawezekani, (specialists)”.

Kauli ya Roosevelt inanikumbusha habari ya vijana wawili waliohitimu Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam. Vijana hawa walipokuwa chuoni muhula wa pili, mwaka wao wa kwanza wa masomo walibuni biashara ya usafiri wa bajaji. Walichanga shilingi laki nane kutoka fedha ya mkopo wanayopewa na bodi ya mikopo ya elimu ya juu, ndipo wakanunua gari hiyo ya miguu mitatu na kufanya biashara hiyo ambayo iliwasaidia sana kuwakwamua kiuchumi.

Kwa mujibu wa maelezo yao ni kuwa wakati wakitambulisha wazo lao kwa wenzao waliambiwa “hilo haliwezekani!”. Wanasema kuwa katika kauli ambayo hawataisahau ni ile waliyoambiwa hivi, “Hiki kitabu cha UDSM kitawapaje muda wa kusimamia hiyo biashara yenu? Labda kama mpo tayari kwa supp zisizokwisha zitakazofuatiwa na disco”. Maneno hayo hayakuwazuia, walianzisha biashara wakaendeleza na bado walifaulu masomo yao. Wakafanikisha kisichowezekana!

Miaka ya karibuni watanzania tumeshuhudia kuanzishwa kwa utaratibu wa kuchangia gharama katika elimu ya juu. Suala hili ndilo lililopelekea kuundwa kwa bodi ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Bodi hii hutoa mikopo kwa wanafunzi hao; katika viwango tofauti tofauti kutegemea na vigezo ambavyo imeweka kwa mujibu wa sheria na taratibu za uendeshaji wa bodi hiyo.

Mabadiliko ya mifumo ya gharama za elimu ya juu nchini Tanzania yanatupa somo muhimu sana kuhusu alama za nyakati. Ni suala la uhakika kuwa siku zijazo mchango wa moja kwa moja wa serikali katika kusomesha vijana wetu utafutika. Hapa naikumbuka kauli aliyopata kuisema Mkurugenzi wa shule ya Star International ya mjini Iringa, Madam Jessca, namnukuu, “Ninawekeza leo kwa kutoa sadaka na kuimarisha biashara zangu, ili siku Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, itakapokosekana, wanangu wasishindwe kupata elimu ya juu” mwisho wa kunukuu. Hakuna haja ya kupambana na nyakati kwa kuzililia zama za Mwalimu J.K Nyerere ambapo elimu ilitolewa bure, bali tukabili nyakati zilizopo na kujipanga kwa nyakati zijazo

Tangu kuundwa kwa bodi hii kumekuwepo na malalamiko mengi sana kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusiana na mfumo huu wa uchangiaji wa gharama pamoja na utaratibu na utendaji wa bodi hii katika kufanikisha lengo hili.

Kuna wadau ambao kwa asilimia mia moja wanapingana na utaratibu huu wa kuchangia elimu ya juu na kuna kundi ambalo linaunga mkono. Sehemu kubwa ya kundi la pili inakwazwa na namna bodi hii inavyotenda kazi zake na kupelekea, mikopo kuchelewa kuwafikia wanafunzi kwa wakati husika, kukosekana kwa mbinu sahihi katika kubaini wapi wanastahili madaraja gani, pamoja na upendeleo (ama uzembe?) katika kupanga madaraja haya ya mikopo.

Bodi hii hutoa mikopo kwa madaraja kwa upande wa ada, “tuition fees” pamoja na fedha ya mafunzo kwa vitendo. Kuhusu fedha za chakula na malazi wanafunzi hupewa kiwango kinacholingana bila kuzingatia madaraja waliyopata. Hadi wakati huu bodi hii inatoa shilingi, elfu tano kwa siku, ama laki moja na nusu kwa mwezi, kama gharama za chakula na malazi.


Kumekuwa na changamoto zinazobainishwa na wanafunzi hawa kwamba kiwango cha fedha wanazopewa hazitoshi katika kuwawezesha kusoma kwa uzuri. Ingawaje vyuo hivi vipo katika maeneo tofauti tofauti, changamoto zinazowakabili wanafunzi hawa nyingi zinashabihiana.

Wanafunzi wengi wanatoka katika familia za kimasikini ambazo pengine hata 70,000/= ya kulipia ada katika sekondari walizotoka zilikuwa zinawapiga chenga. Sasa chukulia kuwa huyu mwanafunzi anapewa mkopo wa asilimia themanini, na yupo katika chuo ambacho gharama ya shahada ya kwanza kwa mwaka wa masomo ni 1,800,000/= Hii ina maana kuwa bodi ya mikopo itamlipia ada shilingi milioni moja na laki mbili na itampa shilingi milioni moja na laki mbili ya malazi na chakula kwa mwaka.

Katika ada atakuwa anadaiwa shilingi laki sita, (600,000/=). Hizi laki sita anatakiwa azilipe kutoka katika ile fedha ya malazi na chakula. Akilipa hizo ina maana anabakiwa na shilingi laki sita tu kwa mwaka wa masomo. (Isisahaulike kuwa bodi ina ukomo wa viwango vya kuwalipia ada wanafunzi inaowadhamini, ukomo huo ni milioni moja na nusu kwa mwaka wa masomo.) Laki sita kwa miezi nane ya masomo, kulipia pango, kununua chakula na kujipatia mahitaji mengine ya msingi kiuhalisia haitoshi.

Tatizo la mikopo isiyotosha elimu ya juu ni la kimtambuka kwa maana kuwa linahusisha pembe nyingi. Kuna suala la ada kubwa katika baadhi ya vyuo, kiwango kisichotosheleza cha fedha inayotolewa na Bodi ya mikopo kwa siku kwa chakula na mavazi, mfumo wa utoaji wa elimu ya juu nchini pamoja na fikra zilizopo miongoni mwa wanafunzi wengi wanaosoma elimu za juu.

Mwanazuoni mmoja wa nchi za Magharibi, G.K Chesterton amewahi kuelezea shida inayowakumba watu kupata ufumbuzi kwa matatizo yanayowakabili, yeye anasema “It isn’t that they cant see the solution. It is that they can’t see the problem” (Sio kwamba hawaoni ufumbuzi wa tatizo, ila ni kuwa hawalioni tatizo). Kuwa na tatizo ni kitu kimoja na kulielewa tatizo (chanzo cha tatizo, lilipo na madhara yake ikiwa halitatatuliwa) ni kitu cha pili. Tuna tatizo la mikopo isiyotosheleza kwa wanafunzi wa elimu ya juu lakini ufumbuzi wake umeendelea kuwa suala la kufikirika na imebaki kulaumiana.

Wanafunzi wa elimu ya juu na baadhi ya wadau wanadhani kuwa suluhisho la tatizo hili ni kuongezwa kwa kiwango cha mikopo. Serikali inasikia lakini haitendi kwa mujibu wa matakwa haya. Tayari pande mbili husika hazijakubaliana na ufumbuzi wa tatizo hili; ina maana kuwa eidha upande mmoja haujalielewa tatizo vizuri ama pande zote hazijalielewa.

Hata hivyo mwathirika mkubwa ni huyu mwanafunzi anayesomeshwa na bodi ya mikopo katika taasisi hizi.Hakuna namna zaidi ya mwanafunzi huyu kupanua wigo wa fikra zake na kuona ni namna gani ataishinda changamoto hii kwa mbinu na njia zilizo halali. Daima ufahamu uliopanuliwa katika njia mpya za kupata majibu ya changamoto, haurudi kamwe katika mipaka yake ya mwanzo. Zikomeshwe fikra za malalamiko, wigo upanuliwe katika ubunifu, badala ya mawazo ya kuilaani Bodi ya mikopo na serikali kwa mikopo isiyotosheleza ni vema kupanua fikra katika kujitegemea

Huu ni wakati ambao vijana wetu wanatakiwa kushusha chini vidole vyao vilivyoielekea serikali na kutazama ni nini kinaweza kufanyika kujikwamua. Mwanaharakati wa kweli hupambana kwa ajili yake na kwa ajili ya vizazi vyake vijavyo. Tujiulize, maswali yafuatayo. Je, vizazi vijavyo vitaishije pindi mchango wa serikali kwa elimu zao utakapofutika, ikiwa hatuweki misingi ya kujitegemea sasa? Vilio vyetu vimesikilizwa kwa kiasi gani? Je, tuendelee kulia ama tufute machozi, tujifunge mikanda tutazame tatizo kwa namna tofauti?

Hakuna maana ya kuweka nadhiri za chuki zitakazoliangamiza taifa kutokana na yale yanayopitiwa kwa sasa. Nafahamu wapo vijana wetu ambao kutokana na adha wanazozipata katika utaratibu huu wa mikopo, wananadhiri kuja kulipiza kisasi. Nao wanaweka nia za kuja kupukutisha rasilimali za taifa ili kunufaisha matumbo yao na ya ndugu zao. Vijana wetu wa vyuo vikuu lazima watambue jambo hili, ya kuwa uovu wa baadhi ya viongozi waliopo madarakani haupaswi kuhalalisha wengine kutenda maovu. Msomi ni lazima awe na ndoto za kuubadili ulimwengu wake kutoka hatua moja kwenda nyingine iliyobora zaidi.

Ipo haja kubwa sana kwa wanafunzi wa elimu ya juu kujijengea utamaduni wa kijasiriamali ili kwa fedha kidogo wanayokopeshwa waweze kuzalisha na kufidia upungufu unaojitokeza katika gharama za masomo yao. Nikigusia suala la ujasiriamali inawezekana kuwepo na vikwazo vingi, ikiwemo muda na mazingira ya kufanya huo ujasiriamali, ukosefu wa rasilimali (mitaji) na mengine mengi upendayo kuorodhesha. Anayevuka na kutatua vikwazo hivyo, huyo ndiye “specialist” wa yasiyowezekana!

Wanafunzi wengi waliopo katika taasisi zetu si wenye juhudi katika kufikiria, ubunifu na kufanya kazi kwa kujituma. Waangalie wanafunzi hawa jinsi wanavyoutumia muda wa likizo zao ndefu na fupi, mara nyingi hawafanyi kazi eidha za kulipwa ama za kujitolea. Mara nyingi hutoa sababu zinazosema na kuonesha kuwa hakuna kazi. Wananata, hawataki kukaa vijijini hata kama kuna fursa nyingi, wanataka kumalizia likizo zao Dar es Salaam.

Kuna wakati unaweza kudhani kuwa vyuo vya elimu ya juu hupendelea kufanya udahiri wa kimikoa, kwa sababu wengi wanataka kutambulika kama wakazi wa majiji hasa Dar es Salaam. Miezi mitatu ama mine ya likizo mtu yupo jijini kwa mjomba, binamu au kwa wa kutoka kijiji kimoja kule Songea, hana kazi zaidi ya kula, kulala, kuoga na kuangalia TV. Wakati mwingine analala sebuleni, na kulala kwake ni mpaka wote waende kulala! Kama mwanafunzi huyu angeenda hata kijijini kwenye kata ya nyumbani kwao akajitolea kufundisha shule ya kata kwa miezi minne angekuwa amezalisha angalau laki mbili!

Ninao mfano wa rafiki yangu mmoja ambaye ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Mzumbe, ambaye amekuwa mbunifu na alishaupiga teke ulimbukeni wa kujiona kuwa eti “wa elimu ya juu” kuna kazi hatakiwi kuzifanya hata kama zinamwingizia kipato. Huyu kila likizo huwa anarudi kijijini kwao na huko huutumia muda wote katika kufanya biashara ya alizeti. Huzunguka vijiji mbalimbali akikusanya na kisha kusafirisha alizeti hizo kwenda mjini. Katika moja ya likizo yake ya miezi minne, aliingiza mtaji wa shilingi laki tatu (fedha za bodi ya mikopo) na kuzalisha jumla ya shilingi milioni moja na laki sita.

Hawa wanafunzi wa vyuo vya juu, imewapasa kuwa na macho ya ndani yenye uwezo wa kuvumbua na kuzitumia fursa. Kuna kuwekeza kwa aina nyingi ambako wakati mwingine mtu si lazima awepo muda wote katika kusimamia alivyowekeza. Inawezekana kumiliki hisa katika makampuni, kuingia ushirika wa kibiashara (partnership) ama kuitumia jamii ya wanafunzi wanaowazunguka, kubuni biashara ama miradi itakayowaingizia vipato.

Pale juu katika makala haya nilitaja pembe zinazochangia mtambuka wa tatizo hili. Ingawa niliacha pembe zingine tatu, ni dhahiri kuwa zinachangia sana katika kufanikisha ufunguzi wa hizi fikra  za hawa wanafunzi wa elimu ya juu. Nitachambua pembe hizi katika makala mengine, lakini itoshe tu kusema, ukiwa na tatizo ni lazima ujikague na kujirekebisha vizuri kabla hujamvaa anaechangia kukua kwa tatizo lako.

Leo hata kama wanafunzi hawa wakaongezewa fedha na kulipwa 20000/= kwa siku, bado watagundua kuwa fedha hiyo haiwatoshi. Suluhisho sio kuililia serikali pekee wakati tumekaa na kubweteka. Tutalala, tutaamka, tutaandamana na kujikuta bado tuko pale pale. Badala ya kuwaza ukahaba, wizi na ujanja ujanja wa kukopeshana na kudhulumiana hebu wasomi wetu waanze kutumia taalveuma zao kufanya ubunifu na kujikwamua. Hii inawezekana ila kwa wale watakaojitolea ku-specialize katika yasiyowezekana.
 Na kila mwanafunzi wa elimu ya juu anayeguswa na hili analazimika kuwa specialist wa yasiyowezekana!

Thursday, July 26

KUMBUKA YAFUATAYO UNAPOPATA HOFU NA KUVUNJIKA MOYO

 Upo wakati ambapo tumnapita katika magumu ,huwa tunafika wakati tunashindwa kujitambua,na wakati mwingine tunapatwa na msongo mkubwa wa mawazo hata tunakata tamaa.Kila wakati jitazame ndani mwako,usome uwezo wako ulio ndani mwako...utaondoa hofu,woga na kukata tamaa.Jikumbushe ya kuwa wewe u bora vile ulivyoumbwa.....wewe ni bora kwa sababu zifuatazo

   Wewe  ni wa pekee,unaipenda nafsi yako,hivyo unampenda Muumba wako na watu wote   pasipo kujali sura,rangi,kabila,dini , na hivyo upo katika uhuru na usalama pote ulipo

  • Unatambua kuwa furaha,amani havitoki nje yako na kwamba furaha ya kweli huanza ndani yako
  • Wakati wote katika maisha yako unaishi ukithamini wengine na kuhakikisha kuwa wewe ni sababu ya wengine kuamka na kufanikiwa,hivyo unapata marafiki na ndugu kwa maisha yako halisi,hivyo wote anaoutambua mchango wako,wanathamini maisha yako.
  • yote yaliyopita kwako,hayakufanyi uwe mnyonge bali yote hayo yalikuwa ni mwanzo wa wewe kuyaendea mafanikio,na hivyo daima utatazama sasa(wakati uliopo) na kuyaandaa maisha yako yajayo kwa kujali pia maisha ya wengine.
  • unatambua kuwa kuanguka(kushindwa) si mwisho wa maisha ,bali ni mwanzo wa kuuelekea ushindi na kadiri unavyoshindwa mara nyingi,ndivyo unavyokuwa mpya kupambana na huhesabu ni mara ngapi umeanguka,bali ni mara ngapi na namna gani umesimama na kushinda.
  • unatambua ya kuwa katika maisha hakuna jambo lililo baya kama kukata tamaa,hivyo magumu hayatakupoteza katika lengo uliloliweka,bali yatakupa mbinu mpya za kufika uendapo.
  • kwa kuwa kila jambo unalolitenda linasukumwa na upendo,na daima unafurahi kuona wengine wakifurahi,unajitolea,unatazama wengine kwa huruma,unawakumbuka wenye mahitaji,hivyo yote yaliyo mema unaowatendea wengine yatakuja kwako pasipo wewe kutegemea.
  • kwa sababu  unayo imani,unayo matumaini na upendo na daima unaepuka hasira,masengenyo,woga,choyo na visasi.
  • unatambua kuwa kutochukua hatua kwa kuogopa kufa ama kuumia ni usaliti wa nafsi yako mwenyewe.
  • moyo wako unawapenda wale ambao jamii imewasahau,unawatia moyo wale walioshuka moyo na wenye katika hali ya kukata tamaa,wwe ni rafiki wa waliotengwa,na  tumaini jipya kwa wasio na tumaini.
  • Daima upo tayari kusamehe,unatazama mbele kwa tumaini la maisha mapya,unaitika sauti ikuitayo kwa ajili ya yatima,wafungwa,wagonjwa,wajane na daima unasimama upya kuyafikia matazamio yako.
    • unapokuwa msaada kwa wanyonge,watima,wajane,wafungwa,matatizo yako yote hupata suluhisho(picha kwa msaada wa mtandao)
    • kwa kuwa unakiri na kutambua na kutumia nguvu na uwezo,akili na  uwezo usioonekana uliopewa na Muumba(Mungu)  kwa utukufu wa Muumba wako,na yote utayafanya kwa ajili ya binadamu wote,hivyo utaepuka kudhuru,kuumiza wengine.
    • kwa sababu unatambua tu kuwa,ili kuwa mkuu mbele ya wengine...ni lazima uwe mtumwa kwanza

Wednesday, July 25

HEKIMA.

Upo wakati ambao tunawalaumu wengine kwa matatizo yetu wenyewe ,lakini hakika,ukijitambua utajua ya kuwa wewe ni kiongozi wa maisha yako, utatambua kuwa wewe ni chemchem ya kila jambo,utaweza kuchanganua lipi la kushika,lipi la kuachia,utakwenda sambamba na mdundo wa maisha yako. utasimama na daima utakuwa na furaha maishani......

Wakati mwingi maishani,tunatengeneza maadui.tunawachukia wengine kwa kudhani kuwa wao ni sababu ya matatizo yetu,tunadhani ya kuwa wapo watu ambao ni wateule katika kutatua matatizo yetu wenyewe,na wakati mwingine tukiwaogopa na kuwafanya kuwa wakuu,ukweli ni kuwa  fikra zetu ndiye adui mkuu,utambuzi tu humfanya adui huyo mkuu kuwa rafiki mkuu katika kutatua matatizo yetu,kusonga mbele na kuyatawala mazingira yetu,na ndipo tutavitazama vitui katika uhalisia wake..

 Kila jambo lina kinyume chake,kuna upendo na chuki,kuna kishinda na kushindwa,kupanda na kuvuna.....utakapoanza kutazama kila jambo kwa mtazamo mpya,mtazamo chanya,utagundua kuwa kila jambo linapotokea huwa si mwisho,bali huwa ni mwanzo wa jambo lingine......kifo si mwisho wa maisha,ni mwanzo wa maisha mapya,kushindwa ni mwanzo wa ushindi.,dhihaka ni mwanzo wa heshima,chuki ni mwanzo wa upendo,udhalimu ni mwanzo wa ubinadamu......na hivi vyote hutoka ndani yetu wenyewe

 Tunafikiri k uwa nafsi zetu na Muumba wetu ni utengano...kwamba Muumba wetu yupo mbali nasi,kumbe yupo ndani mwetu,ni mawazo yetu tu ndio yanayotutenganisha na asili yetu..

  Shujaa si yule aliye na nguvu nyingi,wala hasira nyingi,wala simwenye umbo la kutisha,ama anayeweza  kuwapiga watu kwa hesabu yake....shujaa wa kweli ni yule ambaye huamini katika ushindi,huamini kuwa anaweza,na akawa tayari kupita magumu yote hata anapofika pale anapopachagua kufika,shujaa wa kweli hutazama kila jambo kama nafasi yakwenda mbele.
  
 Anayekata tamaa hana tofauti na yule ambaye anapoteleza ama kujikwaa na kuanguka hanyanyuki tena akiamini kuwa hawezi tena.
  Kila jambo huwa na mwanzo,anayeanza vibaya na kumaliza vibaya ni yule tu anayeamini kuwa kuna nguvu nje yake ya kubadili kile alichokichagua na kukiishi,naye mwanzo wake na mwisho wake,vyote husababishwa na nguvu hiyo iliyo nje yake,lakini ,yule anayejitambua....husimama na kuanza upya pale anapotambua kuwa nguvu zote za ushindi zipo ndani mwake.

Aibu,hasira,woga,chuki,ubinafsi na kulipiza kisasi(visasi) ni sifa za mtu asiyejitambua,asiyetambua kuwa anapotenda yote hayo kwa wengine anajitendea mwenyewe....anayefikiri kuwa ana akili na uwezo kuliko wengine hushusha uwezo wake wa kutenda na kujenga mambo mapya,anapofika ukomo wa fikra zake....husema kuwa haitawezekana tena na hakuna atakayeweza tena
  
  Anayelitambua jambo  pasipo kulitekeleza ni sawa na chumvi ama sukari isiyofaa...kama unajua kuwa wengine wananyonywa,ukanyamaza,kama unafahamu  hakuna linaloshindikana ,kisha ukaogopa kuchukua hatua,utajilaumu sana wakati wa kuiaga dunia hii,utajilaumu kwa kutokuwa chanzo cha mabadiliko,kuwa chanzo cha upendo,kuwa chanzo cha kuwaamsha wengine..lakini ukitenda lile unaloliamini,unapokuja muda wa wewe kuiaga dunia,utaiaga kwa furaha,nawe utakumbukwa kama ishara ya ushindi na nuru ya Mungu iliyo ndani mwako,,itang,aa daima,naamini,dunia itakulilia utakapoondoka
.