Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Wednesday, October 31

JIFUNZE KUFANYA MAAMUZI MAGUMU

Kuna faida kubbwa sana kwa mtu kujitambua.Utafahamu ni jinsi gani unaweza kuchukua maamuzi ya kugeuza maisha ambayo huyapendi na kuishi maisha mapya,n ndipo utakapokuwa tayari kuchukua hatua ya kufanya maamuzi magumu maishani...amua,kaa na kuandika kila jambo unalhitaji ulifanye kwa mwaka mzima,andika kila jamnbo kwa kina...kwa makini tafuta  picha ya jinsi gani unataka maisha yako kuwa...kisha chukua hatua kuanza maisha hay sasa,wakati ni sasa...mwaka wako unaanza sasa...na hakuna mwisho...kila mwisho wa jambo moja utaanzisha jambo jipya..... kumbuka kama huna malengo huwezi kufanya lolote..hivyo weka malengo yako sas..yafanye kuwa dura yako...chukua  hatua hata kama unahisi ni vigumu kusonga mbele...chukua hatua...narudia usiogope kuchukua hatua juu ya maisha yako mwenyewe

ONDOA HOFU KWA WENGINE

 Dunia ina watu wengi ambao daima hukatisha wengine tamaa.,hukatisha tamaa ama kwa maneno yao,vitendo  vyao na kwa njia  nyingine mbalimbali....hawa hiufanya dunia kuwa sehemu ya hofu na mataraji yaliyojaa kukata tamaa....
Ni muhimu tukaitangaza dunia yenye matarajio mema kwa kila mmoja ,tunao uwezo huo,timiza wajibu wako kwa njia yeyote ulionayo iitakayoifanya  dunia kuwa sehemu bora...fanya chochote kitakachoondoa hofu kwa wengine juu ya maisha yao wenyewe kuwafanya wawe jasiri miyoni mwao...washindi na mategemeo makubwa juu ya dunia bora...upendo ndio silaha pekee kufikia hapo.....upendo hushinda yote...........tumeumbwa kufanya maisha ya wengine na yetu kuwa mwanga wa dunia

Monday, October 8

mwanzo wa mafanikio


Pale unapolihitaji jambo lolote kwa moyo wako wote,huwa ndio mwanzo wa mafanikio wa jambo lolote lile.....Msukumo utokao ndani yako ndio mwanzo wa mafanikio yako...kama msukumo ni mdogo utokao ndani mwako ndivyo utoavyo mafanikio madogo...kama ilivyo pia kwamba moto mdogo utoavyo joto dogo pia...Huwezi kupata maendeleo(mafanikio )katika jambo lolote bila kuwa na hamu ya kweli ya kutenda jambo hilo,pasipo mwelekeo(mipango),pasipo kujitolea kwa dhati kulitenda jambo hilo,na wala huwezi kufanikiwa kama jambo ulilosukumwa kulitenda,halijawa sehemu ya fikra na tafakari ya moyo wako kila wakati.Kinachomfanya mtu atambulike ama kufanikiwa si wingi wa mali aliyonayo,bali ni maamuzi ya kweli yatokayo moyoni,ambayo anayehitaji,hujitoa kweli kutimiza lengo(malengo)ALOJIWEKEA.Si idadi ya vyeti alivyonavyo ama elimu aliyonayo...ni kile kilicho ndani mwako...kinachokusukuma kutenda.