Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Tuesday, December 20

KITABU KITAKACHOKUWEZESHA KUWEKA KUMBUKUMBU YA MAPATO NA NMATUMIZI YAKO

JE WAJUA?: Watanzania wengi hatuweki rekodi ya Mapato na matumizi tunayoyafanya kwa siku,juma ,mwezi na hata mwaka?Je unajua kwamba wengi wetu tunatamani kuwa na kumbukumbu na mwisho wa mwaka kujua tulipata kiasi gani na tulikitumia vipi?Sasa umerahisishiwa.Unaweza kuweka kumbukumbu ya mapato yako kila siku na matumizi.
Nimeandaa kitabu kitakachokurahisishia kuweka kumbukumbu juu ya ulichozalisha(wapi,lini,namna gani,kiasi gani) na hivyo kujua unakitumiaje.
Ni kitabu kidogo chenye kurasa 32 (karatasi 8) kiitwacho BAJETI YAKO MIKONONI MWAKO /YOUR BUDGET ON YOUR HAND.Kipo kwa lugha ya Kiswahili na kiingereza,Ni wewe utachagua unapenda cha lugha gani.

Hauhitaji kuwa na elimu ya uhasibu ama biashara ili kuweza kukitumia,kila kitu kimerahisishwa. Unachohitaji ni kuweka kumbukumbu kwa usahihi kama utakavyokuta kwenye maelezo.Kwa nini unapaswa kuwa na kitabu hiki kabla ya kuanza mwaka
1.Utaweza kujua mapato yako yanatokana vema na nini na namna gani uweke bidi
2.Kitakurahisishia kujua matumizi yasiyokuwa na tija na kuyaepuka.
3.Kitakuwezesha kujua vyanzo vyako vya mapato halisi na vyanzo vya matumizi makubwa
4.Ni rahisi kukitumia,kidogo na rahisi kukibeba.
5.Kitakurahisishia kuweka mikakati ya kimaendeleo na kuweka vipaumbele
6.Kitakurahisishia kujua ulipata kiasi gani kwa wiki,juma,mwezi na hata mwaka na hivyo kujua napopaswa kuongeza bidi na kupunguza /kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima
7.Kitakurahisishia kupanga mipango ijayo kwani utajua mapato yako na matumizi halisi nay ale yanayojitokeza.
8.Ni kizuri kwa watu wote wenye nia ya kupanga mipango ya kiuchumi na kuitekeleza.
9.Unajenga tabia ya kuthamini kidogo ulichonacho
UNAKIPATAJE?
Kitabu kinapatikana kwa bei ya tshs 5,000/= .Wasiliana nami kwa namba 0765046644 ama 0717903089 utaletewa popote ulipo.