Tamu, Chungu kutafuta wenza mtandaoni
1 week ago
HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH
![]() |
| Binadamu anayejitambua hutazama kila jambo kama fursa |
![]() |
| Binadamu anayejitambua huyajenga na kuyatunza mazingira yanayomzunguka |


Hofu,adui wa upendo(picha kwa hisani ya mtanzdao)Tumezaliwa tukiwa na upendo,lakini mitazamo yetu ya kifikra imefanya tuweke matabaka katika upendo,na hivyo hofu imetawala upendo,na kufanya hofu kuwa adui mkubwa wa upendo.
Kila unapofikiri kuhusu mwenzi wako,umefikiri kuhusu wewe,unapomtendea mwenzi wako unajitendea wewe,unapomjali mwenzi wako umejipenda mwenyewe,unapomfanya mwenzi wako afurahi umejitendea wewe,upendo hutoka ndani ya moyo wako mwenyewe...pale unapovutiwa na mwingine...pasipo shinikizo litokalo nje ya moyo wako...ukamchagua na kuonesha nguvu hii ya asili kwake,ukishirikiana nae kukua na kuyafikia matarajio ya kila mmoja wenu,hii huitwa ndoa.Ndoa si kupata mwenza ambaye atakufanya uwe kamili(kwa kuwa kila mmoja amekamilika vile alivyo), ni urafiki na upendo uendao mbele ya maumbile.Ndoa ni muumngano wa wawili kila mmoja kwa ukamilifu wake,kwa ajili ya kufanya nuru ya Mungu ambayo ipo kwa kila mmoja,ing'ae kwa kila mmoja ili kuwafanya wawili hao na wale wanaowazunguka waujue utukufu wa MunguNimetazama ndani yangu na kuuona ukamilifu wangu,nami naungana nawe ili mimi nawe tushirikiane ukamilifu wetu(tafakari kwa kina)
muhimu:wengi hufikiri kuwa hawajakamilika,wamekosa kitu fulani,na hivyo huingia kwenye ndoa wakitazamia kukipata kitu fulani toka kwa wenzi wao,baadae hugundua kuwa wanachokitafuta hakipo kwa wenzi wao,hapo ndipo matatizo huanza kutokea kwenye ndoa....baada ya changamoto nyingi ,wengine huomba Mungu awabadili wenzi wao,hawatambui kuwa ni fikra zao ndio adui wa ndoa yao(fikra huleta hofu)-(kama wangetambua wangemuomba Mungu abadili fikra zao.-hata ndoa kuvunjika,hutambua kuwa kumbe furaha,amani,upendo,kujali..kunaanza ndani mwao.sisi twapendana kwa dhati.....kwetu thamani si magari,fedha,ufahari,umaarufu....sisi huvumilia,upendo hushinda yote
Ndoa ni mungano ambao kila mmoja katika wenza huhakikisha anatumia kila alichonacho kuhakikisha kuwa mwenzi wake anakua na kutimiza yale aliyoyakusudia katka maisha yake.Ni mahali ambapo chemchem ya amani ilipo,ndoa si kifungo...ndoa ni chimbuko la uhuru ,ndoa si hofu,bali ni chemchem ya upendo,umoja na amani,ni mbegu iletayo matunda bora,ndoa ni ishara ya kukubali majukumu,ni chimbuko la kuifanya dunia kuwa sehemu bora
Kinyume chake katika dunia ya sasa,ndo imekuwa ni sehemu ya watu kukimbia majukumu,ni sehemu ya watu kukwepa kufikiri,kuamua na kutenda...ndoa imekuwa ni sehemu ya mmoja kuweka matarajio dhidi ya mwenzi wake......tamaa ya kupata mali,kupata sifa ndio imekuwa msukumo wa watu kuingia kwenye ndoa...na kwa sababu ya hofu ya kukosa matamanio ama matarajio haya......mwanadamu akabuni sheria mabyo inamuhakikishia kuwa\ anatimiza matamanio yake......na kutengeneza sheria.....ya kwamba kila anayeingia katika ndoa basi huweka kiapo cha lazima(na kuifanya ndoa kuwa shuruti ya kisheria).Swali ni je,upendo (usio na shuruti) unaweza kulindwa kwa shuruti(sheria)?
Kuingizwa kwa sheria(kiapo_katika ndoa ni dalili tosha ya kuwepo kwa hofu kati ya wawili waliopendana.Ni dalili ya kutoamini mioyo yao .Ni matokeo ya kutazama ndoa katikamisukumo ya hali na mali...gari,fedha,nyumba,ardhi,umaarufu...Matokeo yake ni kwamba mmoja kati yawenzi hawa huwa mtumwa na mwingine huwa mtwana...Hofu ndio msingi wa ndoa ya kisheria.....upendo hushinda yote..Mpendwa msomaji,jiulize ni kwa nini,watu wawili waliokutana wao wawili,wakathaminina na kupendana,huweka kiapo na kuandikishana kisheria.....je kiapo hiki huwasaidia kukua na kupendana pamoja?
Hivi majuzi nimesoma ripoti moja kuhusu ndoa duniani,ikionesha kuwa kuvunjika ndoa kumeongezeka sana toka katika karne ya kumi na tisa na sasa kasi ni kubwa sana..Sababu si ugumu wa maisha,sababu si utandawazi...sababu nimekwisha ieleza,ni fikra zetu na msukumo wa kuingia katka ndo kwa msukumo wa mali na hali,kwa matazamio ya kupata kuliko kutoa,sheria ikiwa ndio chimbuko lake
KWA mtazamo wangu mimi upendo ,ni mvuto asilia...huvumilia,hujali,huthamini..na ndoa iliyojengwa katika upendo,hukua,tena pasipo kiapo kanisani ,msikitini,ama kwa mkuu wa wilaya,kila mmoja huishi kwa furaha ndani ya ndoa hii,kila mmoja huona fahari kuona mwenzi wake akikua nakutimiza ndoto zake....lakini ndoa itokanayo na msukumo wa kisheria...hujengwa katika tamaa,majivuno,hofu,kisasi...na kila mmoja hujitazama yeye anapata nini,mmoja huwa mtumwa na mwingine huwa mfalme.Hawa kinachowaunganisha ni sheria,(hofu) bali waliopendana kwa dhati upendo huwaunganisha.
sihesabu mafanikio katika maisha yangu kwa kuhesabu idadi ya namba za wale wanaonipigia simu,ama wale nliopata kuwa nao,nisiokuwa nao na nilio nao,sihesabu ni fedha kiasi gani nlichonacho,ama mimi ni wa daraja lipi,sihesabu nguo nlizonazo,ama ni vyuo gani na vingapi nimesoma....sihesabu ni marafiki wangapi ninao,ama kama nipo pekee,,,,,,,.nahesabu mimi ninawapenda wengine kiasi gani,na ni kiasi gani nawaumiza wengine,na mimi mwenyewe kwa chuki....nnahesabu,mimi ni nani na najitambua kiasi gani,,nahesabu heshima,usawa ,furaha,ubinadamu,amani..nahesabu ni namna gani nimeleta upendo palipo na chuki,,najifunza kutojisifu wala kutafuta sifa...nahesabu kutazama mbele na kuwa na imani na hakika ya ushindi,nahesabu ni maneno gani ninayasema na yana maana gani,yanawajenga vipi wengine.Kwangu maisha ya mafanikio ni kuwakubali wengine jinsi walivyo na si kwa kutazama mali wanazomiliki,Zaidi ya yote,kwangu maisha ni kuishi kwa kusikiliza moyo wangu,kwa dhati,na kuifanya nuru ya maisha yangu iwaguse wengine ,ili nao wanapochagua kuishi maisha yao kwa dhati-Pongu Joseph-0717903089
![]() |
| moyo wako ni chemchem ya uwezo wa ki Mungu |
![]() |
| SAUTI KUU IKUONGOZAYE KWENYE USHINDI IPO NDANI MWAKO |
Shukrani ziende kwa familia yangu,kwa wote waliokuwa tayari kujitolea ili blog hii ifanikishe lengo lake..Ahsante Mtaki R Muyenjwa Gamba kwa ushauri wa kiufundi nilipohitaji,Lazaro Mafie,Faith Kassano,na wote walioshiriki kwa kila namna.Natambua ya kuwa mimi na wewe tunayo sababu ya kuwepo hapa duniani,nikitambua hilo,nitaishi kwa upendo,nitafundisha upendo na kuufundisha kwawengine si kwa kuusema tu bali kwa kuuishi.Nitajiamini na kutenda kwa upendo..nikijitolea kwa ajili ya wengine pasipo kujali malipo ,ama dharau na kejeli.,kwa sababu hivi havitabadili ukweli ya kuwa mimi ni nani ....nitajitolea na kushiriki kuwaamsha waale wote walio wahitaji..nimejifunza kuwa mimi si chochote pasipo wengine,hivyo matendo yangu na majitoleo yangu yatatazama furaha ya wengine,nikiwapenda na kuwajali kama ninavyoitendea nafsi yangu....nina imani ya kuwa nitakua na kufikia mafanikio hata pale panapoonekana kuwa hapawezekani...kwa pamoja tutaweza
binadamu tumeumbwa tukiwa na uwezo mkubwa...uwezo wa kimungu ndani yetu.....kabla ya hapo tulikuwa katika maisha mengine....tukapewa mwili ...kuja hapa duniani kuonesha utukufu wa Mungu ulio ndani mwetu...hivyo ni jukumu la kila mmoja wetu kujitambua na kuitikia wito alioitwa ,na kuutimiza kwa nguvu zote,moyo wote,ili utukufu/nuru ya Mungu iliyo ndani mwetu ionekane kwa wengine..ili nao waiishi na kuonesha nuru hiyo pale watakapojifunza toka kwetu na kufanya uchaguzi kadiri ya mguso wa moyo ambako ndiko ile nuru huishi
Copyright © 2013 KWA MWANANGU MPENDWA.