Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Wednesday, April 4

SAFARI YA KUTAMBUA KWA NINI UPO DUNIANI.


Mwalimu wa kweli wa kiroho hana maneno ya kukufundisha jambo jipya usilolifahamu, habari mpya taarifa mpya,sheria mpya ama imani mpya.
Kazi pekee ya mwalimu wa kiroho ni kukusaidia na kukuongoza kuondoa giza linalokutenganisha wewe kutoka kwenye ukweli wa kwa nini Mungu alikuumba na undani wa sababu ya kwa nini upo hapa duniani.
Kazi yake ni kukufunulia ujue ukweli unaokuunganisha kwa kina wewe na Muumba wako.
Tumemaliza mfululizo wa siku 40 katika kuweka tafakari ya kina juu ya sababu ya sisi kuwepo hapa duniani kwa njia ya mfungo wa siku 40.
Kwa nini upo duniani? Nimevutiwa kutumia ujuzi nilioupata kushirikiana nawe kwa mfululizo wa siku 40 kutafakari upya kwa pamoja. Ni katika mfululizo wa makala kujikumbusha kwa nini tupo hapa katika dunia hii.
Bila shaka mfululizo huu utakuwa ni njia ya kukufumbua  kuhusu swali hili ambalo wengi hujiuliza ‘’Kwa nini nipo duniani? Nina jukumu gani katika dunia hii’’?
Ni imani yangu kwamba mwisho wa mfululizo hu utakuwa na picha kubwa ya namna ulivyokuwa ukijitazama,na upya baada ya mfululizo huu.
SIKU 40 ZIJAZO
Takwimu mbalimbali zinaonesha kuwa umri wa mwanadamu kuishi unafikia wastani wa miaka 70.Unaonaje kama utafanya maamuzi ya kutumia siku 40 tu kutafakari ni kwa nini Mungu alituleta hapa duniani?
Kwa wale wakristu mtakumbuka jinsi biblia inavyoeleza umuhimu wa siku 40. Mungu alipotaka kumwandaa mtu kwa makusudi Fulani,alitumia siku 40.
·       Maisha ya Nuhu yalibadilishwa kwa siku 40 zaa kunyesha mvua
·       Musa alibadilishwa kwa siku 40 katika mlima wa Sinai
·       Daudi akipambana na Goliath katika siku 40 alishinda na kubadilishwa katika imani.
·       Eliya alibadilishwa pale Mungu alipompa nguvu ya kuishi kwa siku 40 kwa mlo mmoja tu
·       Mji wote wa Ninawi ulibadilika baada ya Mungu kuwapa siku 40 za mabadiliko
·       Yesu aliinuliwa baada ya kufunga na kuomba kwa siku 40 nyikani
·       Mitume wa Yesu walibadilishwa kwa siku 40 baada ya ufufuko.
Bila shaka siku 40 zijazo zitabadili maisha yako
Tutakuwa na mada zilizogawanywa kwa siku 40. Ruhusu mabadiliko katika maisha yako kwa kubadili mtazamo wako katika tafakari ya siku 40. Ni muhimu kushiriki kwa kina katika kusoma makala hizi kwa siku 40 zijazo, ukitafakari na kujadiliana kwa kina.Usikimbilie kusoma tu,tafakari, hata katika mafunzo ya mwalimu mbovu, lipo la kujifunza.
Muombe Mungu akujalie tafakari ya kina, kudadisi na kupata faida inayokusudiwa katika mfululizo huu. Washirikishe na wengine,na shirikiana nao katika kujadili mada kwa kila siku .Ushirikiano wa wawili ni bora kuliko mmoja.Mmoja atashika hili na mwingine lile,kushirikiana kunajenga zaidi.
Nakutakia ushiriki mwema

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

1 Comments:

  1. Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

    Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

    Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

    Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

    Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

    Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159

    dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete

maoni yako hapa