Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Friday, July 6

YOU ARE ALREADY PERFECT

are already perfect — you just need to realize it. You don’t need anything to solve this problem — you already have it. You just need to practice, like it’s the most important thing in your life, because in many ways, it is. ‘You yourself, as much as anybody in the entire universe, deserve your love and affection.’ ~Buddha

Thursday, July 5

FURAHIA MAISHA,FURAHIA JINSI ULIVYO

furahia maisha,furahia jinsi ulivyo
MAISHA HUTUMA CHANGAMOTO,MAISHA PIA HUTUPA MATUNDA NA NEEMA TELE,UTAPATA MAJARIBU,NA PIA MAISHA YATAKUPA MATOKEO MEMA,TUNAPATA MACHUNGU,LAKINI TUNAPATA MATOKEO YA FARAJA NA FURAHA,WENGI WATAKUJA NA KUWA FARAJA,WENGINE KUWA MWIBA,WENGINE WATAKUONESHA CHUKI,LAKINI YOTE YAKUPA WAKATI KUJIFUNZA NA KUKUA KUTOKANA NA CHANGAMOTO HIZO,MUDA UTAKWENDA...YALIYOPITA YANAKUWA FUNZO KWAKO....KUNA SABABU YA KILA JAMBO KUTOKEA...NA JINSI UNAVYOCHUKULIA KILA JAMBO,NALO HUKUPA MATOKEO YALEYALE...HIVYO NI VEMA TUKALICHUKUA KILA JAMBO KATIKA MFUMO CHANYA,YAANI KILA CHANGAMOTO IWE NI NJIA YA WEWE KUKUA NA KWENDA MBELE ZAIDI,,MAISHA YATAKUFUNZA KUCHAGUA...WAWEZA KUCHAGUA KWENDA MBELE KWA FARAJA AMA KUTAZAMA KILA JAMBO KWA WOGA NA KUANGUKA BILA KUSIMAMA...KILA MMOJA ANA UCHAGUZI...NI VEMA KUCHAGUA KWENDA MBELE NA MAISHA....TUNAWEZA KUYAISHI VYEMA MAISHA KWA KUCHAGUA KUWA BORA ZAIDI NA KUWA MIFANO BORA...KUFURAHIA MAISHA NA KUYAISHI BILKA KUOGOPA AMA KUTAZAMA KWA HUZUNI NA WOGA...HAYA YOTE TUTAYASHINDA KWA KUFANYA BIDII NA KWA KUJITOLEA KWA MOYO WOTE...KUWA MMOJA WA MJENZI WA DUNIA BORA...JUHUDI NA KUTOKATA TAMAA(UVUMILIVU)YATATUPATIA MATOKEO BORA...PALE TUNAPOCHAGUA KUWA MWONGOZO WETU....JIAMINI,...FUNGUA MOYO WAKO..SIKILIZA SAUTI YA MOYO WAKO....TIMIZA NDOTO YAKO.........ISHI NA KUYAFURAHIA MAISHA

Wednesday, July 4

upendo ni lugha ya moyoni,ni lugha ambayo kila kabila,kila taifa na kila kiumbe huitambua,imepita maneno na maandishi,juu ya ubaguzi,juu ya dini juu ya siasa....na kila atoaye hupendo,hulipwa upendo

YASHINDE YOTE

Umeumbwa ukiwa mshindi....wewe ni mshindi....tambua ya kuwa wewe ni mzaliwa wa ukoo wa ushindi toka hapo awali....lakini kushinda yote yapasa kwanza kujitolea kwa moyo wote na nguvu zote kutekeleza yale ambayo umedhamiria kuyafanya...tekeleza majukumu yote kwa uaminifu na bila shuruti..jiamini katika K ila ukifanyacho binafsi na katika maamuzi ya jumuia..kuwa na moyo wa imani kuwa unao uwezo wa kufanya kitu kipya chochote unachokidhamiria hata kama wapo wameamini ya kuwa haiwezekani...kwani tumezungukwa na wale ambao kwao vingi haviwezekani...kwao wao ,wapo wateule ambao wamepewa uwezo fulani(jambo ambalo si sahihi)kuwa na tumaini moyoni mwako hasa pale ambapo tumaini huwa ni hitaji(wakati wa changamoto ) na kuwa kioo kwa wote wanaokuzunguka..(kuwa kioo haimaanishi kutafuta umaarufu ama kutenda ili ujulikane na kujipatia chochote,bali ni kutenda kwa bidii yako yote...na mafanikio yako yanakuwa ni mfano kwa wengine)uwe na moyo wa kujitolea kila wakati...tena kujitolea pasipo tegemeo la kupewa chochote(unconditional giving)kupenda na kuwajali wote na kwa maana hiyo kuufundisha upendo kwa wengine...jiamini na kupigania imani yako hasa pale ambapo wengine wote huona ama hudhani kuwa hauko sahihi(mradi tu wewe unaongozwa na visheni yako)uwe tayari kutenda kwa wema kwa wengine,na kujifunza kutoa kwa wale wenye mahitaji...jitoe(jitolee) kwao pasipo fikira na malengo ya kujipatia ama sifa ama zawadi yeyote.jiamini na kutenda na kufikiri kwa mfano wako wa kipekee bila kufuata fikra na njia za watu(simaanishi usifuate ushauri wa wengine,bali kwa mwenye visheni yake..huongozwa na mwongozo wa visheni yake na sio mitazamo ya wengine),kwani naamini njia za wengine zitakupeleka ktk matokeo yao,bali isikilize sauti iliyo moyoni mwako ili maisha yako yawe ya mfano kwa watu wote,na kwa kufanya hivi utawafundisha wengine kujitambua na kuishi maisha yao yasiyo ya bandia...ukumbuke ya kuwa Ipo sauti inayokutuma kutenda jambo moyoni mwako...hii ni sauti iliyo moyoni mwako na mwisho...usikate tamaa.

Tuesday, July 3

may motivate yu

The CREDIT belongs to the man who is actually in the ARENA, whose face is marred by DUST and sweat and blood, who STRIVES valiantly, who errs and comes up short again and again, because there is NO EFFORT WITHOUT ERROR or shortcoming, but who knows the great enthusiasms, the great devotions, who spends himself for a worthy cause; who, at the best, knows, in the end, the triumph of high achievement, and who, at the worst, if he fails, at least he fails while daring greatly, so that his place shall never be with those cold and timid souls who knew neither victory nor defeat."-- Theodore Roosevelt (26th President of the United States of America|September 14, 1901-March 3, 1909) in his speech titled "Citizenship in a Republic," at the Sorbonne, Paris-France on April 23, 1910 Any fool can criticize, it is one of the EASIEST thing to do. There is a difference between a FEEDBACK and mindless CRITICISM. Of more use is a CONSTRUCTIVE criticism.

ELIMU ILIYO BORA

hakuna elimu iliyo bora kama elimu imfanyayo mtu kujitambua yeye ni nani,anatoka wapi na anakwenda wapi....tofauti na elimu zingine zinazofanya BINADAMU akariri mambo waliyoyafanya wengine,nakumfanya aishie pale walipoishia hao(kwa maneno mengine kupita katika njia ileile walopita hao waliotangulia),elimu hii humfanya mtu awe na uhuru wa kufikiri usio na kikomo....na kumfanya binadamu kufanya mambo makubwa na yasiyo na ukomo,ili nuru iliyo ndani mwake,ionekane kwa wengine,ili nao wajitambue......elimu hii ipo ndani mwa kila mmoja pale anapopiga hatua moja na kuamua kuishi maisha yake halisi..kutimiza yale ambayo moyo wake unamtuma...akipanda milima,mabonde,tambarare,katika nyakati za kuumia,kuanguka na kuamka.....na mwisho kujitambua ya kuwa hakuna uchawi wala ujanja.,..bali kila kitu ki ndani mwake.....kwa wale wanaomfahamu Yesu ama kusoma habari zake(yesu kristo wa nazareti),ambaye alichukua hatua...akaishi maisha yake ...pasipo ubandia...akaipanda milima,mabonde,magumu,akababa kila lawama....lakini alitaka kufundisha jinsi ya kufanya maamuzi ambayo hutufanya tujitambue....hii ndio elimu kubwa aliyotaka tuifahamu

TUPO KWA AJILI YA WENGINE

tupo hapa duniani kwa ajili ya wengine,si kwa ajili yetu tu.....tuwatazame wengine kwa upendo,kama tunavyojipenda sisi.....huwezi kusema una upendo kama hujafanya matendo yanayouonesha upendo,huwezi kusema una utu kama matendo yako si ya utu...wala huwezi kusema kuwa wewe ni wa thamani kwa wengine kama hutendi kwa thamani kwao wakati wote...ni vema upendo uwe ni mwongozo wetu ili nuru ya maisha yetu ing'ae.maisha ya yeyote anayejitambua ni kutenda kwa ajili ya wengine..ka anayetambua,katika macho ya ndani,basi vitu vidogo ni vikubwa na kila kimoja huhesabiwa na kurudisha kadiri utoavyo,kutambua ni kujielewa..unaweza kufanya chochote pale upatapo moyo wa kufanya hivyo.....nawe unapata moyo wa kuendelea mbele..ni ukweli kwamba huwa tunafanya uchaguzi usio na manufaa kwa wengine na kwetu wenyewe,na hivyo ndovyo tunavyojifunza....hizi ni changamoto....nuru tulionayo ...ni dawa tosha kwa wengine...hasa pale upendo unapokuwa ndio msukumo wa awali...tazama kila tunapohitaji kunyanyuka tuangukapo,twatazama ile nuru......na kumbe hiyo nuru ndiyo ile waitazamiayo wengine...kumbe tumeunganishwa.....kila mmoja wetu kwa upendo..binafsi ... mimi si wa tofauti,nawe huna tofauti nami...wote tu wamoja...kila mmoja akiitazamia nuru ...nuru iliyo ndani ya kila mmoja...kila mmoja wetu..na tazama kila nijitoleapo kwa wengine...moyo wangu hujazwa furaha isiyo kifani....na ndipo sauti iliyo juu ya upeo wangu inapozidi kuniamsha na kunifundisha mengi.....na kuzidi kunifanya nitambue ya kuwa nipo ka ajili ya wengine.nawe kumbka ya kuwa upo kwa ajili ya wengine.la sivyo maisha yako yasingekuwa katika dunia hii ya kutegemeana kwa vipawa vyetu