Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Sunday, July 15

MWANAMKE-USHINDI ULIOFICHIKA

MWANAMKE HUSIKIA MLIO WA UA HATA UPITAPO UPEPO

 Lengo langu katika makala hii si kufananisha(kulinganisha )kati ya mwanamke na mwanamme,hii ni kwa sababu hakuna kilicho bora kuliko kingine....kila kitu kipo vile kilivyo na ubora huja na kukamilika pale mtu anapotumia uhuru wake wa kuchagua,kuchagua anavyotaka awe,aishi....na kila achaguapo huwa.

Lengo langu ni kutaka kufunua yale yaliyofichika kuhusu mwanamke......ni baada ya kujifunza kupitia wanawake wengi......nikapata hisia za kuandika kuhusu kiumbe hiki kilicho bora,ishara ya upendo,uaminifu,huruma na chemchem ionekanayo ya ubinadamu na uwezo wa Mungu kwa mwanadamu....hisia zinanituma kumuona mwanamke kuwa ni ukamilifu aliouumba Mungu baada ya mwanaume kuwa na mapungufu mengi.(nieleweke kuwa simaanishi mwanaume si bora)(kwa Mungu kila kitu ni bora kadiri alivyokiumba)...

yapo mambo mengi ambayo mwanaume alikuwa ameyakosa kuitimiliza dunia.....hivyo mwanamke akaumbwa akikamilisha yale ambayo yalikuwa ni muhimu(alikamilika yeye kama mwanamke katika dunia timilifu na si kwamba anautimiliza ukamilifu wa mwanaume,mwanaume anabaki kuwa bora jinsi alivyoumbwa,na mwanamke anabaki na ubora wake, wote wakiuishi utimilifu wao kwa ushirika wao
 .
 Maisha yetu huwa yapo katika mzunguko...yanaanza na maisha fulani,yakimalizika,huanza mengine,mfano tupo hapa duniani,baada ya kumaliza maisha yetu hapa,huenda kuanza maisha mengine mapya,kadiri tunavyochagua.......anayefahamu hili anathawabika kwa ufahamu wake...lakini anayeliishi...ana hekima na hufanikiwa...
 mwanamke huishi kwa kufuata mfumo huu....hata pasipo kutambua.,.mwanamke hukubali haraka maisha anayoyaishi..akiyaishi pasipo kuigiza...akitenda upendo...akiishi huruma,akiishi ubinadamu,akiishi kwa kila matarajio ya maisha ya baadae.....

Mwanamke huyaishi maisha yake kwa unyoofu wake...pale anapoamua kuishi kwa dhati,huishi kwa dhati..hulea kwa dhati,hukarimu kwa dhati,hufungua moyo wake kwa wengine kwa dhati....hushiriki na wengine katika kila jambo linalohitaji ushirikiano....huuguza kwa dhati,huvisha kwa dhati...na hii ni ishara ya kila mafanikio katika maisha...yaani kulichagua jambo na kulifanya kwa dhati...wanaume wachache huweza kuamua hivyo...wanaume hugusa hiki na kile,hufanya kwa muda tu,hutamani dunia bandia,huchelewa kukubali maisha yaliyo halisia.....

MWANAMKE ,UPENDO,UVUMILIVU ULIOTUKUKA....HATA PALE ANAPOONEKANA KUSHINDWA..HUSIMAMA-HUJITOLEA KWA DHATI HATA KATIKA NYAKATI AMBAZO YEYE HUHITAJI ZAID   
 Mwanamke huuona upendo usioonekana,hutambua wakati wa kulia,wa kucheka,anatambua wakati wa kulishika jambo (na kulishika kwa moyo wake wote,) na anafahamu wakati wa kuachana na jambo linalomuumiza na kuanza upya maisha.....huu ni mfano bora wa mafanikio katika maisha..................yaani kulishika jambo kwa dhati....na kuyaacha yale yanayoturudisha nyuma,kwani mara nyingi tunashindwa kwenda mbele kwa sababu tunashikilia mambo ambayo yanatuumiza na kutufanya tuhindwe kwenda mbele......mwanamke huweza kuyatambua mambo haya vema..........hata akitelekezwa,husimama na kuanza upya maisha...ishara ya uvumilivu na ishara ya kujikubali na kujiamini na kwenda mbele hata pale ambapo wale wanaomzunguka hawaamini ya kuwa....ATASIMAMA TENA
kwa mwanamke majaribu kwake ni mtaji wa ushindi
 Kwa mwanamke majaribu kwake ni mtaji wa ushindi......anapoonekana kuwa hatatoka,amechimbiwa.......yeye kwake ni sehemu anayejipika,anayojiandaa kunyanyuka na kupaa juu...huyu ni mwanamke ambaye jamii imemfanya aonekane dhaifu,tegemezi....lakini hakika mwanamke akijitambua na KUSIMAMA......ushindi kwake ni lazima
MWANAMKE HUFURAHIA MAISHA,NA KWENDA NA MDUNDO WA MAISHA
 MWANAMKE HUFURAHIA MAISHA,NA KWENDA NA MDUNDO WA MAISHA,AKIJALI,AKIISHI KWA UPENDO,AKIHUDUMIA NA KUAMSHA ARI YA KUANZA UPYA MAISHA KWA WALE WALIOKATA TAMAA

Thursday, July 12

DINI NA UUMBAJI WA WAAMINIO.

tazama Mungu umtafutae yupo ndani mwako
TAZAMA MUNGU UMTAFUTAE,YU NDANI MWAKO

Waimbaji huiwakilisha nuru ya Mungu kwa nyimbo.Waandishi pia hutufundisha yatokayo ndani mwao kwa kutumia maneno na kuyaandika.Wahubiri huifundisha nuru ya Mungu kupitia vipawa vya kuzungumza na kwa mifano mbalimbali hukumbusha uwezo wa Mungu ulio ndani mwetu.Mjasiriamali vivyohivyo hutenda kwa kutumia maneno yao ya kibiashara na bidhaa zenye kumjali mnunuzi.

Je wewe binafsi unaufundisha vipi utukufu wa Mungu?

Hakuna aliye hapa kwa bahati mbaya.Tuna sababu ya kuwepo duniani.
Nayo ni kufurahia uumbaji wa Mungu na kuitengeneza dunia bora.
Je,ni jinsi gani dini na imani ndani yake inatujenga kutambua sababu ya sisi kuwepo?

Nianze kwa kukusihi usome kuanzia mwanzo mpaka mwisho,ili uweze kuelewa ni nini nimekusudia kukifikisha kwako.....SI KAWAIDA KWANGU KUTAZAMA JAMBO KATIKA UPANDE HASI,lakini nitajadili upande hasi wa dini kwani ndicho kilichonisukuma kuandika kwa sasa,ninakusihi uchukulie hii kama elimu chanya ili ikusaidie kujadili na kujitambua.

 Dini inamaanisha jumla ya imani ya binadamu kadhaa pamoja na mafundisho wanayotoa kuhusu yale ambayo wanayazingatia ama kuyasadiki, yaani mambo ya roho, kama vile kuhusiana na Mungu, maisha na uumbaji-hii ndiyo maana ya kimtazamo kuhusu dini...Japo kimantiki hii si maana halisi.

Kila anayeingia katika imani hii,ama dini,matazamio yake huwa ni kwamba,dini itakuwa ni suluhisho la kila jambo kwa binadamu.....dini inatazamiwa kuwa ndio amani,ndiyo furaha,ndio umoja,ndio huruma,ndio usawa,ndio kila chimbuko la ubinadamu,na kikubwa kumfanya binadamu ajitambue yeye ni nani,anatoka wapi na anakwenda wapi......

Lakini kwa sasa imekuwa ikiwafanya binadamu kuwa tegemezi,wasio huru katika kila nyanja ikiwemo uhuru wa kufikiri usio na mipaka,uhuru wa kuchagua(simaanishi uchaguzi mbaya). Dini imekuwa kifungo cha kuwafanya wengi wasitumie vipawa walivyonavyo na hata wasisikilize sauti ya Mungu inayowatuma kutenda kwa ajili ya utukufu wake.(Unaweza kuuliza kivipi,jibu ni fupi...imani nyingi katika dini zimeweka mipaka ,inayomfanya muamini asifikiri juu ya hapo)NA KUWAFANYA wawe na maisha yasiyo na mwelekeo wa ushindi na hivyo kuamini kinyume na matarajio ya imani yenyewe.

1.KUMWOGOPA MUNGU
  Dini nyingi zimewafanya waumini wake wamwogope sana Mungu na kumuona kuwa ni adui.Wengi wamekuwa wakimuona Mungu ya kuwa yu mbali sana nao,asiye rahisi kufikika,asiye rahisi kuongea nae.

Wanasahau ya kuwa Mungu wamtafutao na kumwogopa yupo ndani mwao..Nae ni sauti iliyo kubwa kuliko utashi wa mtu mwenyewe,kuliko awazaye mtu,.Wanasahaulika ya kuwa yeye huzungumza na yeyote yule ,kwa wakati wowote pale kila mmoja awaye tayari kumsikiliza.

NAYE NI RAFIKI MKUBWA WA NAFSI YA KILA MMOJA WETU, Mungu ni mpole,mwenye huruma,asiyetazama tutazamavyo sisi,bali hutazama mawazo ya mioyo yetu,naye hujibu maombi ya mioyo yetu,na si maneno yatokayo kwa mtu..

 Hivyo kwa matokeo hayo dini hujenga jamii ya watu wenye kujiogopa wenyewe,wakimwogopa Mungu aliye rafiki mkuu,wakiishi maisha bandia ya kujionesha kwa wengine hasa wale wanaowaongoza,wawaone ya kuwa wamejaa nguvu za Mungu na matendo yaliyotukuka,huku wakifanya kinyume kwa siri(siri kwa binadamu wenzao,lakini Mungu ambaye tupo nae nafsini mwetu anatutazama kwa ubandia wetu)

2.KUISHI MAISHA YA WENGINE 
Dini zimekuwa zikiwafundisha na kuwafanya watu waishi maisha ya wengine na kuchagua maisha ya wengine waliopita na kuyaacha yetu yale tuliyoitiwa ili nuru yetu ing'ae kwa wengine....Hapa naomba nieleweke vizuri kuwa viongozi wengi wa dini wamekuwa wakiwafundisha watu kuishi kama fulani aliyepita(wapo wanaowaita watakatifu,wengine viongozi wao waliopita....)wakijitesa,wakijinyima pasipo sababu ya msingi,(SABABU ISIYO MSUKUMO WA MHUSIKA BALI MSUKUMO WA NJE}na matokeo yake kuishi maisha yasiyo ya furaha kwani mwisho hugundua ya kuwa furaha huja pale unapoishi maisha uliyoitiwa wewe mwenyewe,
Ukiyaishi kwa kujitolea si kwa ajili ya kuneemeka,bali ili wengine waitambue nuru ya Mungu aliyo ndani ya kila mmoja,na wale wasioamini ,wajitambue na kuiishi.

Dini zitakufundisha kuishi maisha ya wengine na matokeo ya wengine lakini ROHO WA MUNGU aliye ndani mwetu hutufundisha kuishi maisha yetu halisi ili tufikie katika matokeo mapya,yamtangazaye Mungu na utukufu wake.
Wengi wameingia kwenye mkumbo kwa kufuata tu imani ,kwa sababu ni za wazazi wao

3.DINI NA WATEULE

Dini hutoa picha ya matabaka,ya walio wakuu kuliko wengine,na wale wanyonge(watawaliwa) wanaosubiri pia kupewa ukuu na Mungu.inatokeaje? Viongozi wengi wa dini wamekuwa wakijipa ukuu na kuwaaminisha wengine kuwa ukuu huo umetoka kwa Mungu.Viongozi hawa wamejitangazia utawala,wakichuma kutoka kwa wengine ambao daima huwaogopa na kuhisi labda,Mungu kateua baadhi,na kwamba wao si wateule.

UKWELI NI KWAMBA,KILA MMOJA YU SAWIA KWA 
MUNGU,Yu bora akiwa na uwezo na nguvu za kuponya,kuamsha upya ari ya kila kitu,kulea,kuwanyanyua wanyonge badala ya kuwakandamiza,na ukweli ni kwamba,kwa sababu tuu mfano wa Mungu(tukifanana katika nguvu )tunauwezo wa kufanya chochote kile,kuyafikia mafanikio makubwa,kuvumbua vitu vipya,mradi tu tumetambua uwezo huu na kuchagua kuutumia  

aliye mkuu yu ndani mwetu,sote tu bora
kila mmoja akitumia kipawa chake vyema,basi huwa mkuu..tukumbuke aliye mkuu ni yule atendaye yote kwa ajili ya wengine pasipo kutegemea malipo,aliye tayari kuona wengine wakinyanyuka na kuendelea mbele,asiyetengeneza matabaka,ambaye kwake kila mmoja ni sawa,na katika yote,upendo humsukuma kutenda

Tunaweza kuyaona matokeo ya dini,ni jinsi gani inaumba mustakabali wa waamini wake dini zimekuwa ni chanzo kikuu cha matabaka na ubaguzi duniani hasa kutoka kwenye imani na mafundisho ya msingi ya imani husika,dini moja hujiona ni bora kuliko nyingine...tena zinawafanya baadhi kujiona wao ni wateule na kutengeneza tabaka la wanyonge tofautti kabisa na makusudio ya MUngu.mf. mkatoliki anajiona ni bora na ni mteule ukijilinganisha ma mlutheri,mkristo anajitazama kama ni mteule akijilinganisha na mwislamu.mlokole anajipa sifa ya kuwa mteule pekee wa mungu akijilinganisha na wengine...hili ni kinyume kabisa na malengo ya Muumba ya kumuumba kila binadamu na kumfanya kuwa sawa na mwingine..dini zimeleta imani iliyopelekea matabaka..choyo,majivuno,utengano na hata kutowasaidia wengine kwa kuwaona si wa darajasawia... tukirejea vita na vurugu nyingi ni zile ziletwazo na dini...rejea ireland,nigeria,sudan,uturuki zamani.....tena hizi ni vita kati ya dini kubwa zinazofundisha usawa na upendo lkn zikishindwa kuonesha matokeo bora... dini pia zimekuwa ni chanzo cha kumfanya binadamu kuwa mtumwa wa mawazo yake naa mazingira yake...zinafundisha kinyume cha makusudio ya MUumba ya kumfanya binadamu kuwa huru na kuyatawala mazingira yake...zinafundisha utegemezi huku viongozi wakuu wakiwatumia waumini wao kama daraja la kujipatia utajiri na utawala...

Mbele za Mungu hakuna aliye mkuu na wala mtawala...kila mmoja amepewa nguvu na uwezo na anapaswa kuzitumia kama nuru ya utukufu wake MUNGU hapa duniani... Ni WAKATI SASA KUTAMBUA YA KUWA DINI ya kweli ya kila mmoja,ipo ndani mwake...na kuwa ukitambua hilo,utakuwa huru,mawazo huru yasiyo na mipaka,kila jambo litawezekana na li ndani ya uwezo wako kwani Mungu aliye suluhisho la yoote,yu ndani mwako.

Lengo langu si kupinga uwepo wa dini,lengo langu ni kukufanya ujitambue na unyanyuke,uwe na hofu ya kweli,hofu ya kuona unamaliza uwepo wako hapa duniani pasipo kuifanya nuru ya Mungu iliyo ndani mako,ing'ae......hofu ambayo itakufanya utumie maisha yako yote kuwainua wengine.....walio wahitaji,walio wanyonge,walio wafungwa na kila mmoja ambaye upendo tu,huwaamsha

Wednesday, July 11

MAFANIKIO HUANZA NA FUKUTO NDANI MWAKO

KIFARANGA KUTOKA NJE YA YAI(kutotolewa),HUTOKANA NA YEYE MWENYEWE KIFARANGA
KIFARANGA KUTOKA NJE YA YAI(kutotolewa),HUTOKANA NA YEYE MWENYEWE KIFARANGA, KUANZISHA KISHA KUPASUA KIWAMBO CHA NJE
MUASISI WA HATUA ZOTE ZA KUTOKA TUMBONI KWA MAMA HADI KUZALIWA HUANZA KWA MTOTO MWENYEWE

MUASISI WA HATUA ZOTE ZA KUTOKA TUMBONI KWA MAMA HADI KUZALIWA HUANZA KWA MTOTO MWENYEWE NA KISHA TAARIFA HUPELEKWA KWA MAMA NA NDIPO KICHOCHEO CHA UCHUNGU HUTOLEWA

Juu ni mifano inayokupa picha kuwa,tangu hatua ya kuzaliwa msukumo hutolewa na anayezaliwa mwenyewe na si anayezaa....hii ni sawa na kusema mtoto ndio aanzishaye hatua za yeye kuzaliwa.Kwa wale waliopata kujifunza zaidi somo la baiolojia,warejee na watakubaliana nami kwamba msukumo wa awali wa kiumbe kuzaliwa huanza kwa kiumbe anayezaliwa,,yaani,msukumo unaofanikisha hutoka ndani.....hivyo kwa kifupi ni kuwa ,msukumo utuleteayo matokeo yetu chanya ama hasi hutoka ndani mwetu wenyewe
 KUCHANUA KWA UA NI MATOKEO YA MSUKUMO UTOKAO NDANI YA UA LENYEWE
KUCHANUA KWA UA NI MATOKEO YA MSUKUMO UTOKAO NDANI YA UA LENYEWE
 Vivyo hivyo,msukumo unapotoka nje(external forces) matokeo yake huwa ni kuharibu,mfano msukumo utokao nje kwenda kwa mtoto husababisha mimba(kiumbe) kuharibika ama kufa,vivyo hivyo msukumo utokao nje kwenye yai hulipasua na kuliharibu....mfano huu huwa sawia pale ua linapopigwa sana na jua(msukumo wa nje) nalo hulazimishwa kuchanua na matokeo yake hunyauka
msukumo wa nje huharibu

Ukitaka mafanikio maishani,ukitaka furaha,ukitaka amani,nk hivi vyote haviletwi kwako na mtu mwingine,wala hakuna kitu nje yako kitakachokuletea,wala haitokei kama bahati..bali hutoka kutoka kwenye fukuto litokalo ndani ya chemchem isiyokauka,toka moyoni mwako .
 FURAHA YA KWELI HUTOKA NDANI MWAKO Wengi tumekuwa tukifikiri kwamba furaha yetu hutoka nje yetu, Mafanikio yetu yataletwa na wengine pasipo sisi kuyatamani kwa dhati,tumekuwa tukilaumu wengine kwa mambo yanayotuhusu sisi wenyewe,na kumbe sisi ndio tunaohusika na maisha yetu na uchaguzi wetu tunaoufanya...

Utakapotambua hili ya kuwa wewe ndio chemchem ya matokeo na matazamio yote maishani,utaanza kuchukua hatua ukitafakari kwa kina bila ukomo,ukichuja na kuchagua yenye manufaa na kuyasimamia kwa dhati .
furaha huanzia ndani
.



NDANI MWAKO NDIMO PALIPO NA CHEMCHEM YA KILA JAMBO
 Mifano hiyo yote juu inatufunza jambo moja la muhimu sana....ya kwamba kila jambo ambalo hufanyika pasipo manung;uniko na hatimae kufanikiwa ama kuleta matokeo yaliyokusudiwa,huanza ndani (hutoka ndani mwa alifanyaye...Aliyefanya ugunduzi wa ndege,roketi,bastola,komputa,simu...nk.wote hawa msukumo wa kufika walipofika ulitoka ndani mwao...


 NDANI MWAKO NDIMO PALIPO NA CHEMCHEM YA KILA JAMBO....ULIFIKIRIALO HUTOKEA..HIVYO UNAPASWA KUCHAGUA KIPI UKITOE,KIPI UKITUMIE,KIPI KIKUONGOZE..... TAZAMA,WEWE NI JINSI UWAZAVYO,WEWE NI FUKUTO LA KILA JAMBO


ULIFIKIRIALO HUTOKEA.
WEWE NI JINSI UWAZAVYO



 Hivyo,wewe ni fukuto la mafanikio unayoyatarajia,mafanikio katika kila nyanja hayaji kwa kusema tu,ama kwa kusoma tu,bali huja pale unapoweka nia,na kuhakikisha unasimamia wazo unaloliwaza pasipo ukomo mpaka pale unapofikia.....ukisema huwezi,umeshindwa,ukisema unaweza bila kuchukua hatua,wewe si shujaa,kwani daima shujaa anapotambua jukumu lake hulifanya na kuliishi..... Ahsante ,nategemea maoni,maswali na ushauri

Monday, July 9

NITAYASHINDA YOTE

nitapanda milima na mabonde,nikiyaishi vyema maisha niliyoyachagua,nitashinda
Nitapanda milima na mabonde,nikiyaishi vyema ambayo ni uchaguzi wa moyo wangu,nitashinda .
Sauti zote zinazonikatisha tamaa zitashindwa .
 Nitayashinda yote na kuvunja imani zote na kauli zote zinazoaminisha kushindwa,na kunifananisha mimi na wengine ambao wanaamini katika kushindwa, ama kushinda kwa kutazama mifano ya wachache na wengi walioshindwa.....Nitashinda kwa sababu katika kupambana kwangu....nautambua mwisho,ya kuwa  nitashinda licha ya changamoto zote,

Nitashinda....ninaongozwa na visheni ionayo mbali,isiyotazama tu hatua chache,bali itokanayo na uhuru usio na mipaka wa tafakari,na uhuru usio na mipaka wa kuchagua,,,,,Sitakuwa na chochote cha kupoteza hata nikipoteza maisha,kwani kuishi maisha yasiyo na mtazamo wala matokeo ya kuifanya dunia kuwa sehemu bora,kwangu ni hasara kubwa......sitajutia uamuzi wangu,kwani kwangu majuto ni kutofanya jambo kwa kuamini kuwa haliwezekani, Na kisha mwingine akalifanya... 

Sitasikiliza sauti zote ambazo zitanikatisha tamaa,zitokao kwa wale wanayoyatazama maisha katika mtazamo hasi,na wote watakao nifanya niishi maisha ya bandia,bali daima nitaisikiliza sauti iliyo moyoni mwangu,ile iliyo kubwa kuliko ile ya mawazo mengi,ile iletayo furaha..kwani natambua kuwa kila mmoja ana jukumu la kusikiliza muito wa moyo wake, .umuitaye kuifanya kazi ambayo hujengwa katika upendo na kuijtolea,ili Nuru ya MUNGU iliyo ndani mwetu ionekane...
natazama mbele daima nikiyafurahia maisha
Nitatumia nguvu zangu, akili zangu na uwezo wangu wote kuisikiliza sauti ya Mungu kutenda kadiri sauti huru ya Mungu initumapo,nikitekeleza kwa upendo,ili alama ya maisha yangu,iandikwe hapa duniani,na siku nitakapo yaanza maisha yangu baada ya maisha katika dunia hii,alama hii iwe ni nuru kwa wengine na kuwa ishara ya umoja,kujitolea,na ushindi dhidi ya wasioamini...

Nitafundisha upendo kwa kuuishi,nikitimiza malengo yangu na ndipo nitakapouvuta upendo wa wengine.
Nitafanya bila kumdhuru yeyote,nikisamehe na kuyakubali maisha na changamoto zake....na ndipo wengine watakapotambua sababu ya wao kuwepo duniani,waamke,wajitambue,watumie vipawa vyao ,wakiifanya dunia kuwa sehemu bora ... kwani kila mmoja anazo nguvu zisizoonekana..lakini zikiwe ni zaidi ya vile kila mmoja ajiwaziaye na kufikiri.....

Licha ya kuwa niendako ni mbali,nitashinda yote
 DUNIA INILILIE PALE NTAKAPOONDOKA NA KUYAENDEA MAISHA MAPYA,SIO TU KWA SABABU YA NILIKUWEPO,BALI KWA SABABU NILIYAISHE VYEMA MAISHA,PASIPO KUOGOPA MACHO YA WENGINE,BALI KWA KUTAMBUA KILE NIKIAMINICHO,AMBACHO HAKUNA AWEZAYE KUKIONA,ISIPOKUWA MWENYE MACHO YAONAYO MBALI,YALE YAUONAO MWISHO KABLA YA KUANZA KWA MWANZO EWE MUUMBA WA VYOTE NISAIDIE...AMINA.

SAMEHE,FUNGUA MILANGO YA FURAHA NA MAFANIKIO

Sote tu binadamu,sote hufanya uchaguzi ambao huweza kuwaumiza wengine na kutuumiza sisi pia. Tunaweza kufanya uchaguzi huo eitha kwa kusudi ama pasipo kusudio.Tunawaumiza wengine na kuumiza mioyo yetu...tufanyapo hivyo tunafunga nafasi ya urafiki,ushirikiano na maelewano....,tunajiwekea mipaka ya kupata nafasi za mshikamano. Tunafunga milango ya mafanikio...tunafunga milango na kuweka mstari mpya wa utengano...chuki,ubaguzi,masengenyo, na kikubwa tunajenga uadui mkubwa ambao hutuumiza mioyo yetu wenyewe....


Kutosamehe ni kukaribisha giza(chuki )mioyoni mwetu
Wengi hufikiri tu kwamba kutosamehe ni kuwakomoa wengine,ni kuwafungia milango..kumbe kutosamehe kunafunga milango yako mwenyewe.....Pia wengi hufikiri tu kuwa tunapaswa kusamehe wengine...pasipo kutibu majeraha ya kuumia katika mioyo yetu pale tunapoamua kufanya uchaguzi ambao hutubomoa...Tunafika wakati tunakuwa  na  aibu, na kukata tamaa kutokana na kutosamehe........

 Kutosamehe kunafunga milango yote ya mafanikio...Ni  kuonesha udhaifu mkubwa...kutosamehe ni kutoamini katika upendo...ni kukaribisha uadui wenye aibu mwishoni. Na zaidi ya hayo  ni kuwasha moto wa huzuni moyoni mwako,ni kufifisha uamsho wa mafanikio moyoni mwako

KUSAMEHE NI KUONDOA UCHUNGU,NA MAUMIVU YA MOYO {PICHA KWA HISANI YA MTANDAO)
 KUSAMEHE NI KUONDOA UCHUNGU,NA MAUMIVU YA MOYO...NI KUAMSHA UPYA NGUVU ZAKO ZA USHINDI JIFUNZE kusamehe..

Samehe nafsi yako kwa yote ambayo huwezi kujivunia ya kuwa yalikupa faida mbaya...fungua Moyo wako na kusahau yaliyopita.

1.Fungua mlango wa muujiza wa maisha yako....wote tunahitaji maisha yaliyo na nuru angavu,iletayo mafanikio kwa kuyaishi vyema maisha yetu, kwa kuchagua kutenda kwa upendo kwa wengine,kuwajali na kujali thamani ya kila mmoja...

 2.Kumbuka uwezo wetu mkubwa wa kuifanya dunia kuwa sehemu bora,upo katika kuyatazama maisha ya wengine hasa kwa kusamehe licha ya kuwa upo wakati ambao tuliumia sana

3.Tambua ya kuwa huruma,kupenda usawa,amani na kuyahubiri maisha yajayo na kuyahubiri maisha yetu yaifanyayo nuru ya Mungu ndani mwetu kung'aa ama kufifia, hupimwa na uwezo wa kusamehe...
si kwamba kuonesha udhaifu..bali ukomavu katika kutazama kwa ubinadamu na upendo uliotukuka,hasa kwa wale wanayoyaishi maisha ya ulimwengu usioonekana,lakini pale wengine wanapoweza kujifunza kwao ktk ulimwengu uonekanao..

KUSAMEHE NI KUFUNGUA MLANGO WAKO KWA MOYO WAKO,KUIFANYA SAUTI YAKO ISIYOSIKIKA,ISIKIKE HATA KWA WALE TUWAONAO KUWA NI MAADUI(PICHA NA unconditional love}
4.Kwa kutambua kuwa wenye hasira,jeuri,visasi,majivuno hawawezi kuijenga dunia,bali huibomoa...........twapaswa kujifunza kuijenga,kwani dunia bora huanza kujengwa ndani ya mioyo ya wale walio tayari kujitolea kwa wengine pasipo ghiliba wala majivuno...wala visasi...hivyo basi ni vema kusamehe na kuifanya dunia sehemu bora .

 KUSAMEHE NI KUFUNGUA MLANGO WAKO KWA MOYO WAKO,KUIFANYA SAUTI YAKO ISIYOSIKIKA,ISIKIKE HATA KWA WALE TUWAONAO KUWA NI MAADUI.

 Hili ni jambo kubwa sana kujifunza...pale unaposamehe,na kujisamehe mwenyewe...unafungua mlango wako kwa sauti iliyo ndani mwako,ambayo huanza kufanya kazi,kukufanya uwe wwe uliyo,ufungue mlango wa mawasiliano wewe ni Muumba wako...na ndipo hata sauti yako,ya upendo husikika na kusambaa,hata wale wakuonae adui,sasa huwa marafiki,wakikuthamini na kuutambua ukuu wa kiMungu ulio ndani mwako.........samehe...ufungue mlango wa furaha na mafanikio-

{picha zote kwa hisani ya unconditional love}

Saturday, July 7

UTANG'AA,UTAPAA LICHA YA VIKWAZO

NITAPAA,NITANG'AA KUFIKA KULE AMBAKO WENGI WANASEMA SITAFIKA
NITAPAA,NITANG'AA KUFIKA KULE AMBAKO WENGI WANASEMA SITAFIKA WEWE NI WA KIPEKEE,HUNA TOFAUTI NA WALIO NA MALI NYINGI,HUNA TOFAUTI NA WENYE ELIMU YA JUU YA DIGRII....

UTANGAAA,UTAPAA -Kuwa tayari kutambua ya kuwa wewe una uwezo mkubwa ndani yako....utapaa,kuwa tayari kutambua kuwa vipo vikwazo,milima na mabonde...lakini siri ni moja.....weka visheni yako juu ya jambo unalotaka kutimiza.....UTANG'AA,UTAPAA...

SIKILIZA HISIA ZA MOYO WAKO....SIKILIZA MOYO WAKO...TIMIZA MOYO WAKO UNAPOKUTUMA..UTANG'AA,UTAPAA...

KUWA NA VISHENI MWANANGU......HUTAKATA TAMAA KAMWE KWANI UNAJUA MWISHO WA PALE UNAPOTAKA KUFIKA,HIVYO VIKWAZO ,MILIMA NA MABONDE,HAVITAKUDONDOSHA KAMWE KWANI WAIJUA NJIA,WAUONA MWISHO...

.UTANG'AA,UTAPAA....UMEPEWA UHURU USIO NA KIKOMO WA KUCHAGUA...UMEPEWA UHURU WA KUTUMIA FIKRA ZAKO PASIPO UKOMO...UTANG'AA,UTAPAA...UTAPAMBANA NA WENYE NGUVU,WENYE KASI YA KUTISHA ,LAKINI WEWE UTASHINDA NA SABABU NI MOJA,,,WEWE UNAAMINI KATIKA USHINDI...WEWE WATAZAMA MBALI,HATA ZAIDI YA MAWINGU...MBELE YA BAHARI,NDANI ZAIDI YA MIAMBA..

UTASHINDAWEWE UNA NURU...NURU NDANI YAKO...NURU IKUONGOZAE HATA KATIKA MWISHO WA UPEO WAKO......UTAPAA...WAO WANAVUTA OKSIJENI ...NAWE PIA...KWA NINI WEWE USISHINDE?HAUMTEGEMEI MGANGA,WALA MIUJIZA YA KUFIKIRIKA...BALI WAUTAMBUA UWEZO WAKO WA KIPEKEE ALIYEKUPA MUUMBA..... UTADONDOKA MARA NYINGI,UTAUMIA,UTACHOKA SANA LAKINI WAITAMBUA FARAJA YAKO...PALE UFIKIAPO MWISHO...HIVYO KWAKO HIVI NI VIGEZO MUHIMU KWENDA MBELE, KWENDA JUU ZAIDI.

NJIANI KATIKA MAGUMU UTAGUNDUA MBINU  MBINU MPYA NA DAIMA HUTAPOTEZA MWELEKEO-UTANG'AA,UTAPAA...

TAZAMA WATAKUCHEKA...WATASEMA HUNA LOLOTE,WENGI WALISHASHINDWA...LAKINI WAONA MBALI,NAWE WAUJUA MWISHO,NAO MOYO WAKO UMEJAA NGUVU,ISIYO KIFANI....WATAFIKIRI YA KUWA HUTATOKA ULIPO...LAKINI TAZAMA WANAPOKUJA WATAKUKUTA UKIWA JUU....JUUU...NAO WATAPEWA TAARIFA YA KUWA...HAYUPO...KATANGULIA .... MTAMKUTA....KAMA ALIVYOSEMA
simama mwanangu......usikumbuke maumivu...kumbuka faraja iliyobaki......allow your wing to fly to greater


ruhusu mabawa ya uwezo Uliopewa ,kuruka juu na kuyafikia mafanikio makubwa,,...
UMESHAJITAMBUA NAWE WAUONA MWISHO..........ruka kwa nguvu zote,usisikilize maneno ya wengine ya kukukatisha tamaa,fanya yote ukisukumwa na upendo...hutakatishwa tamaa na milima wala mabonde.....changamoto hazitakufanya utepoze mwelekeo...kuwa imara kwani M UNGU YU NDANI MWAKO.... simama mwanangu......usikumbuke maumivu...kumbuka faraja iliyobaki......allow your wing to fly to greater height
NITAPAA KUYAFIKIA MAFANIKIO LICHA YA KUWA WENGINE HAWAAMINI
NITAPAA KUYAFIKIA MAFANIKIO LICHA YA KUWA WENGINE HAWAAMINI MWANANGU,CHUKUA KILA KIKWAZO KATIKA MINAJILI CHANYA,IWE NDIO SABABU YA WEWE KUFIKIA MAFANIKIO,WAKATI WAO WANASEMA HAIFAI,HAITAWEZEKANA,HAITATOKEA KAMWE...WEWE UTAWEZA KWA SABABU TU UMEAMINI NA KUCHUKUA HATUA...KUTUMIA NGUVU ZOTE NA UWEZO WAKO WOTE..TAZAMA UTAFIKA-TAFAKARI

MAHUSIANO,MAUMIVU,UPENDO UNAANZA NA WEWE

KWA NINI UMEINGIA KWENYE MAHUSIANO?
JE ILI UPENDWE>?JE UMEINGIA KWENYE MAHUSIANO ILI KUJAZA PENGO AMBALO LI WAZI? UMEINGIA KWENYE MAHUSIANO ILI UFANANE NA WENGINE WALIO KWENYE MAHUSIANO? JE UMEINGIA KATIKA MAHUSIANO ILI KUUMALIZA UPWEKE ULIOKUA NAO?UMEINGIA ILI UWEZE KUWA NA MTU UNAYEWEZA KUMUITA MPENZI?

Je ili kumaliza mgandamizo wa kuachika ama mawazo yeyote?ILI kumkomoa yeyote uliyekuwa nae kwenye mahusiano?ili uolewe?...........................................................?

Kama hizi ni sababu za kuingia katika mahusiano,basi tambua kuwa mahusiano hayo yatakusumbua sana,na itafika wakati utatoa maana mbaya ya mahusiano.....na kumbe wewe ndiye muanzilishi mkuu wa kuteswa,kuumizwa,kupigwa,kudhalilishwa,kutothaminika...na wewe ndiye unayetoa ruhusa ya yote hayo...

 Kila mmoja wetu ana uhuru wa kuchagua...usio na mipaka.Na kila unachokichagua ni chema.....ni chema kwako....lakini ukumbuke kila uchaguzi unaoufanya una madhara yake(yenye faida na yasiyo na faida kwako.........  

Kabla ya kuingia kwenye mahusiano yeyote,hakikisha unaingia si tu ukitegemea kuwa mwenzi wako atakupa kitu fulani,furaha ama amani,atakufanyia nini,atakujali kiasi gani,atafuata taratibu unazoziweka wewe kwa kiasi gani,atakupenda kwa kiwango gani,atakufariji kwa kiwango gani............bali jiulize wewe utakuwaje chanzo cha upendo katika mahusiano yenu,wewe utakuwaje chanzo cha uhuru usio na mipaka kwa mwenzi wako,utakuwaje ni tunu ya mwenzi wako kukua na kufikia malengo aliyoyapanga,je,wewe utakuwa ni chanzo cha mwenzi wako? kuiona na kuiishi nuru ya Mungu iliyo kwa kila mmoja wenu.....na je ni kwa kiasi gani wewe hauchukui uhusiano kuwa kifungo cha kisheria kati yenu wawili,bali zaidi kuwa ni chachu ya uhuru na msukumo wa mwenzi wako kukua?

Upendo ni kutoa/kujitolea
 Jiulize hivi ni kweli unaingia katika mahusiano kwa ajili ya kutimiliza ukamilifu(kwa kuhisi wewe hujakamilika) badala ya kuingia katiaka mahusiano kuuishi utimilifu ulionao ili kwa pamoja ninyi mkue na kuufanya upendo ndio utimilifu wenu?

Jiulize upendo ni msukumo utokao moyoni kwenda kwa mwingine pasipo kujali chochote jiulize,je unaingia katika mahusiano ili tu utimize matamanio yako ama raha ya mapenzi....?  

Upendo wa kweli ni ule ambao hutoka kwa anayejipenda yeye kwa dhati na kuwafikiri wengine juu ya upendo alio nao.....upendo huu huwa juu ya rangi,juu ya ukabila,juu ya dini ,juu ya itikadi, juu ya tofauti za kimtazamo na kifikra......na upendo huu hushinda yote!!!!!!!1

UPENDO NI KUMJALI MWENZAKO LICHA YA TOFAUTI ZENU
 Ni ajabu kuona dini zikitenganisha watu,dini kuwa juu ya ubinadamu na upendo,...zikifundisha wengi kuingia katiaka mahusiano kwa misikumo ya vitu nlivyoviutaja awali...vikitazama imani sawia,fikra sawia,mfumo dume,na ndio maana mahusiano mengi na ndoa nyingi zimeshindwa kudumu na matokeo yake ni manyanyaso,dharau,vitisho na huzuni .

Mahusiano ya kweli yenye afya kwa pande zote mbili huanza na upendo unaotoaka ndani mwa kila mmoja,kwenda kwa mwingine pasipo kuhesabu faida,rangi,kabila, ama tofauti yeyote,bali husaidia kila mmoja aliye ndani ya mahusiano hayo kukua,kutimiza ndoto za kila mmoja ...na kwao hao upendo hushinda yote....

Hivyo basi,ni vema ukajipenda na kutambua maana ya kupenda,ni vema ukasukumwa na upendo ambao ni kitu halisi na si vitu visivyo na mashiko katika mahusiano...ni vema ukatambua kuwa mahusiano ama ndoa,ikijengwa katika minajili ya kila mmoja kuhakikisha anaheshimu mawazo,uhuru wa mwenzi na kuhakikisha kuwa anamsaidia mwenzi wake kuendelea na kukua hata kutimiza malengo yake na hisia zake....upendo ukiwa msukumo mkuu....hushinda yote