Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Thursday, September 6

ujumbe 2

Ipo siku ambayo hutahesabu tena ni nini unamiliki ama umepoteza.......
chuki,hasira na majaribu yote hayatakuwepo
Haitajalisha kuwa ulikuwa na sura nzuri ya mvuto ama ulionekana wa sura mbaya
wala ngozi,wala jina halitahesabika
Ni NINI KITAHESABIKA....
KiTAHESAbika ulichotoa kwa wengine na si ulichopokea
Kitahesabika ulichojenga ukiwa duniani,kilichowainua wengine,,,na si kile cha kifahari ulichonunua
Ni kila upole,usawa,utu, na kuwanyanyua wote walio wahitaji,
nI vile ulivyo,wewe halisi,ulivyoyaishi maisha yako kwa ajili ya wengine
Si watu wangapi wanakufhamu,ama umaarufu wako bali ni kiasi gani wengine wataumia pale wanapokukosa
Ni ule umuhimu wako kwa wengine
Si kumbukumbu tu kwamba ulikwepo,bali ni kumbukumbu ya maisha ya wengine uliowabadilisha na kuwasaidia kufikia furaha.
Kitakachohesabika si ni muda gani utakmbukwa,bali ni nani na kwa nini unakumbukwa,ni kwa wema uliotenda
Katika maisha tuishio,ni muhimu kuishi maisha yenye faida kwa wengine....
jiulize ni nini kimekuleta duniani...ishi kilichokuleta

Sunday, September 2

UJUMBE

Wakati mwingine huhisi kuwa niandikayo hapotea tuu,hutazamwa tuu,na hata kutotiliwa maanani...hii hainikatishi tamaa...siuzi ujumbe...hutolewa bure...wakati mwingine nafikiri kurudia na kurudia
Wakati mwingine nasoma kwa kurudia na kurudia,nami hupata faraja.Siandiki tu kujifurahisha....naandika nikilenga kubadili maisha ya wale walio katika huzuni,kuanguka na wote wanaohitaji maneno tu kusimama na kuanza tena maisha yenye mafanikio...naweza nikawa sijaridhisha wengi,lakini ukweli ni kwamba nitaweza kuinua wachache...kwa yule ambaye huguswa na hata machache ,huu ni upendo wangu uende0 kwa wote....naamini siku moja nitakuwa sababu ya furaha kwa wengi...Ni tamaa yangu kuona ujumbe unafika mbali...kuwaamsha wengi....naamini ipo siku mlango mkubwa utafunguka...kwa ajili ya wengi..nami nitajitolea daima,kusimama pale Mungu atakaponituma.

Saturday, September 1

YALIYOPITA YAMEPITA...SONGA MBELE

Wapo wanaotazama mambo ya jana,juzi na yote waliyoyapitia na kukata tamaa,Wakisikia jinsi marafiki wao wanavyowanenea mabaya,wakitazama kila pande na kuhisi hakuna anayewajali,wakiangalia pande zote wasione tumaini,hukata tamaa lakini ukijitambua hutakata tamaa kamwe,kwani utatambua kuwa ni Mungu na wewe ndiye uliyetumaini juu ya yote...Hutaweka matumaini kwa wengine tu,bali utajifunza kuwa wewe ndiye unayepaswa kuchukua hatua juu ya maisha yako.
Maumivu tuliyopitia hutupatia juhudi mpya na uwezo mpya.Yote wanayokunenea wengine hayatakufanya uwe vile wanavyotaka ama kudhani kuwa utakuwa hivyo,bali uamuzi wako utayainua ama kudidimiza maisha yako mwenyewe.Utaacha aibu na woga wa kufanya jambo kwa kuogopa kuwa wengine watakucheka ama kusema vibaya juu yako.Jibu kwao ni mafanikio utakayoyapata,ambayo yatawafunza wao pia.Hutajiona kuwa hustahili kuwa unavyopenda,bali sasa utaamua na kujipenda,ukiishi kwa ajili ya wengine pia
Kila jambo huwa na sababu ya kutokea,ukitazama yaliyopita kwa moyo mweupe,utafurahi kupita huko,kwani ndiko kunliko kuinua na kukufanya uwe imara zaidi..Ndipo sasa utakapoanza kujitazama upya na kujipenda jinsi ulivyo,jinsi ulivyoumbwa,na si jinsi wengine wanavyotaka uonekane....usiwaache wengine wakuchagulie maisha yako...usiache yaliyopita yakakuchagulia jinsi utakavyokua.
Tazama ulivoshinda vikwazo,kisha chukua nguvu ya ushindi wako na songa mbele.Unaweza na maisha yanaendelea.Amka...songa mbele

AHSANTE WOTE


Rafiki wa kweli ni yule ambaye unaweza kumwamini,ni yule ambaye unaweza kumshirikisha furaha,huzuni na kila tamanio la moyo wako,ni yule ambaye hakuhukumu kwa kufikiri tu,ama kusikia toka kwa wengine,ni yule anayekubali na kuheshimu maamuzi yako,uchaguzi wako na uhuru wako,ni yule ambaye yupo tayari kutumia alichonacho kwa ajili yako,ni yule anayeweza kukukosoa na kukufanya utambue njia bora na kukua ukiendelea mbele daima,hutambua umuhimu wako na kukupa moyo,kukuamsha uwe bora zaidi na kufikia mafanikio,Hukusikiliza na kukushauri pale panapostahili na unapohitaji...daima huwa kwa ajili yako..rafiki wa kweli hawezi kuwa na ajenda za siri,hawezi kukuzunguka n A KUKUSALITI...rafiki wa kweli hufurahi pale unapofanikiwa na si kuweka kinyongo na kuumia pale unapofanikiwa,daima huwa pamoja nawe......na ni furaha kubwa pale unapogundua kuwa rafiki yako mkuu ni wewe mwenyewe....furaha pia ni kumpata rafiki wa kweli ..ni wachache....daima nafurahi kupata marafiki wa namna hii..nitakuwa sina fadhila kama sitasema ahsante itokayo katika furaha ya moyo wangu

Tuesday, August 28

TUNAENDELEA MBELE

KATIKA MAISHA TUNAPITIA MAGUMU.....tunapitia kuanguka mara nyingi...tunapitia kukatishwa tamaa,kusengenywa,kutengwa na hata kudaharauliwa.....tunapitiwa kuumizwa katika mahusiano,kuachwa,kudhulumiwa nk...haya yote hayana budi kutokea,jambo la muhimu ni kuwa tunavumilia yote na licha yakuwa tumeanguka mara nyingi,lakini pia tumesimama mara nyingi zaidi...na ndio maana tunaendelea na maisha kama ili

vyo kawaida,tunaendelea kuandika,kuwaelimisha wengine,kuwaburudisha wengine na kuwafariji wengi....tunayafahamu maisha,tunajua kuwa kama tutakata tamaa tutakuwa tumejidharau wenyewe,tumejiangusha wenyewe,tumejisengenya wenyewe na tumejidhulumu wenyewe.....
Hatukati tamaa kamwe
“Tunasikiliza mioyo yetu,kwa sababu hutupatia mwongozo wa maisha kila kukicha,hutukumbusha kuwa haklisi...hutukumbusha kuwa tupo kwa ajili ya wengine....hutukumbusha kuwa dunia inatuhitaji....hutukumbusha kuwa sisi ni zaidi ya tujifikiriavyo...sisi ni bora kama tulivyoumbwa

Monday, August 27

NAFASI YAKO HAPA DUNIANI NI YA MUHIMU SANA

Kwa sababu kila mmoja wetu anahitaji kuthaminiwa,kuheshimiwa na kila mmoja anahitaji kuona wengine wanamjali....mioyo yetu haiwezi kuwa na furaha ya kweli kama hatutakuwa sauti kwa wale ambao wanataka kusema lkn hawapati japo nafasi....kuwa faraja kwa wale wenye machozi,kuwa mwangaza kwa wale wanaohitaji nuru ya kuamsha mioyo yao na ari ya kuyaishi maisha yao....tutakapokuwa nguvu kwa wanyonge,na zaidi..kuishi kwa ajili ya wengine

Haujatokea duniani kama bahati mbaya,ama pasipo lengo,lipo lengo....nalo ni kuishi lengo hilo ili nuru ya Mungu iliyopo ndani mwako ionekane ,Bila wewe kuwepo na kuishi maisha yako,lipo jambo ambalo halitakuwa vile linatakiwa liwe,upo kwa ajili ya kuiangaza dunia...wewe ni mwanga...wewe ni chachu ya maendeleo ya dunia hii....si nyota,wala jua,wala miti,wala majani ,wanyama kila uoto ambao unakukosa pale unapokuwa upo duniani pasipo kutenda jambo lililokuleta.....nafasi yako wewe haijazwi na mtu yeyote mwingine,ndio maana umeletwa hapa duniani....amua kutimiza lengo lililo kuleta,viumbe wote wanakuhitaji....ishi kwa ajili ya wengine,wauone upendo,waione amani,waijue faraja,wafahamu kujitolea...na haya yote yanatoka kwako wewe..wewe ni wa pekee


 

Saturday, August 25

WEKA JUHUDI KUJITAMBUA WEWE KWANZA

Wapo watu wanaofikiri kwamba yupo mtu ambaye anahusika juu ya uchaguzi wa wanataka kuwa nani,na kuishi maisha ya namna gani...Wapo wanaofikiri kuwa wenzao ni bora kuliko wao...Wapo wanaofikiri kuwa upo wakati utafika watabadilika tu katika kufikiri,kutafakari na kufanya maamuzi pasipo kuweka juhudi binafsi.Nikupe siri moja katika kutafuta mafanikio,jiulize unataka maisha ya namna gani,uishi vipi maishani....jiulize kila mara kabla ya kulala,na baada ya kuamka,jikumbushe ....kila siku mpaka pale moyo wako na nafsi yako itakapofanya kuwa kanuni ya msingi,kisha chukua hatua pasipo kutazama pembeni ama wanaokutazama....Acha uiga wengine...wewe ni wa pekee na nafsi yako...maisha ni mwanga,fuata mwanga wako..acha uoga...chagua ujasiri ....amka ,chimba ndani ya moyo wako,chimba ujitambue wewe ni nani.