Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Wednesday, October 31

JIFUNZE KUFANYA MAAMUZI MAGUMU

Kuna faida kubbwa sana kwa mtu kujitambua.Utafahamu ni jinsi gani unaweza kuchukua maamuzi ya kugeuza maisha ambayo huyapendi na kuishi maisha mapya,n ndipo utakapokuwa tayari kuchukua hatua ya kufanya maamuzi magumu maishani...amua,kaa na kuandika kila jambo unalhitaji ulifanye kwa mwaka mzima,andika kila jamnbo kwa kina...kwa makini tafuta  picha ya jinsi gani unataka maisha yako kuwa...kisha chukua hatua kuanza maisha hay sasa,wakati ni sasa...mwaka wako unaanza sasa...na hakuna mwisho...kila mwisho wa jambo moja utaanzisha jambo jipya..... kumbuka kama huna malengo huwezi kufanya lolote..hivyo weka malengo yako sas..yafanye kuwa dura yako...chukua  hatua hata kama unahisi ni vigumu kusonga mbele...chukua hatua...narudia usiogope kuchukua hatua juu ya maisha yako mwenyewe

ONDOA HOFU KWA WENGINE

 Dunia ina watu wengi ambao daima hukatisha wengine tamaa.,hukatisha tamaa ama kwa maneno yao,vitendo  vyao na kwa njia  nyingine mbalimbali....hawa hiufanya dunia kuwa sehemu ya hofu na mataraji yaliyojaa kukata tamaa....
Ni muhimu tukaitangaza dunia yenye matarajio mema kwa kila mmoja ,tunao uwezo huo,timiza wajibu wako kwa njia yeyote ulionayo iitakayoifanya  dunia kuwa sehemu bora...fanya chochote kitakachoondoa hofu kwa wengine juu ya maisha yao wenyewe kuwafanya wawe jasiri miyoni mwao...washindi na mategemeo makubwa juu ya dunia bora...upendo ndio silaha pekee kufikia hapo.....upendo hushinda yote...........tumeumbwa kufanya maisha ya wengine na yetu kuwa mwanga wa dunia

Monday, October 8

mwanzo wa mafanikio


Pale unapolihitaji jambo lolote kwa moyo wako wote,huwa ndio mwanzo wa mafanikio wa jambo lolote lile.....Msukumo utokao ndani yako ndio mwanzo wa mafanikio yako...kama msukumo ni mdogo utokao ndani mwako ndivyo utoavyo mafanikio madogo...kama ilivyo pia kwamba moto mdogo utoavyo joto dogo pia...Huwezi kupata maendeleo(mafanikio )katika jambo lolote bila kuwa na hamu ya kweli ya kutenda jambo hilo,pasipo mwelekeo(mipango),pasipo kujitolea kwa dhati kulitenda jambo hilo,na wala huwezi kufanikiwa kama jambo ulilosukumwa kulitenda,halijawa sehemu ya fikra na tafakari ya moyo wako kila wakati.Kinachomfanya mtu atambulike ama kufanikiwa si wingi wa mali aliyonayo,bali ni maamuzi ya kweli yatokayo moyoni,ambayo anayehitaji,hujitoa kweli kutimiza lengo(malengo)ALOJIWEKEA.Si idadi ya vyeti alivyonavyo ama elimu aliyonayo...ni kile kilicho ndani mwako...kinachokusukuma kutenda.

Thursday, September 6

ujumbe 2

Ipo siku ambayo hutahesabu tena ni nini unamiliki ama umepoteza.......
chuki,hasira na majaribu yote hayatakuwepo
Haitajalisha kuwa ulikuwa na sura nzuri ya mvuto ama ulionekana wa sura mbaya
wala ngozi,wala jina halitahesabika
Ni NINI KITAHESABIKA....
KiTAHESAbika ulichotoa kwa wengine na si ulichopokea
Kitahesabika ulichojenga ukiwa duniani,kilichowainua wengine,,,na si kile cha kifahari ulichonunua
Ni kila upole,usawa,utu, na kuwanyanyua wote walio wahitaji,
nI vile ulivyo,wewe halisi,ulivyoyaishi maisha yako kwa ajili ya wengine
Si watu wangapi wanakufhamu,ama umaarufu wako bali ni kiasi gani wengine wataumia pale wanapokukosa
Ni ule umuhimu wako kwa wengine
Si kumbukumbu tu kwamba ulikwepo,bali ni kumbukumbu ya maisha ya wengine uliowabadilisha na kuwasaidia kufikia furaha.
Kitakachohesabika si ni muda gani utakmbukwa,bali ni nani na kwa nini unakumbukwa,ni kwa wema uliotenda
Katika maisha tuishio,ni muhimu kuishi maisha yenye faida kwa wengine....
jiulize ni nini kimekuleta duniani...ishi kilichokuleta

Sunday, September 2

UJUMBE

Wakati mwingine huhisi kuwa niandikayo hapotea tuu,hutazamwa tuu,na hata kutotiliwa maanani...hii hainikatishi tamaa...siuzi ujumbe...hutolewa bure...wakati mwingine nafikiri kurudia na kurudia
Wakati mwingine nasoma kwa kurudia na kurudia,nami hupata faraja.Siandiki tu kujifurahisha....naandika nikilenga kubadili maisha ya wale walio katika huzuni,kuanguka na wote wanaohitaji maneno tu kusimama na kuanza tena maisha yenye mafanikio...naweza nikawa sijaridhisha wengi,lakini ukweli ni kwamba nitaweza kuinua wachache...kwa yule ambaye huguswa na hata machache ,huu ni upendo wangu uende0 kwa wote....naamini siku moja nitakuwa sababu ya furaha kwa wengi...Ni tamaa yangu kuona ujumbe unafika mbali...kuwaamsha wengi....naamini ipo siku mlango mkubwa utafunguka...kwa ajili ya wengi..nami nitajitolea daima,kusimama pale Mungu atakaponituma.

Saturday, September 1

YALIYOPITA YAMEPITA...SONGA MBELE

Wapo wanaotazama mambo ya jana,juzi na yote waliyoyapitia na kukata tamaa,Wakisikia jinsi marafiki wao wanavyowanenea mabaya,wakitazama kila pande na kuhisi hakuna anayewajali,wakiangalia pande zote wasione tumaini,hukata tamaa lakini ukijitambua hutakata tamaa kamwe,kwani utatambua kuwa ni Mungu na wewe ndiye uliyetumaini juu ya yote...Hutaweka matumaini kwa wengine tu,bali utajifunza kuwa wewe ndiye unayepaswa kuchukua hatua juu ya maisha yako.
Maumivu tuliyopitia hutupatia juhudi mpya na uwezo mpya.Yote wanayokunenea wengine hayatakufanya uwe vile wanavyotaka ama kudhani kuwa utakuwa hivyo,bali uamuzi wako utayainua ama kudidimiza maisha yako mwenyewe.Utaacha aibu na woga wa kufanya jambo kwa kuogopa kuwa wengine watakucheka ama kusema vibaya juu yako.Jibu kwao ni mafanikio utakayoyapata,ambayo yatawafunza wao pia.Hutajiona kuwa hustahili kuwa unavyopenda,bali sasa utaamua na kujipenda,ukiishi kwa ajili ya wengine pia
Kila jambo huwa na sababu ya kutokea,ukitazama yaliyopita kwa moyo mweupe,utafurahi kupita huko,kwani ndiko kunliko kuinua na kukufanya uwe imara zaidi..Ndipo sasa utakapoanza kujitazama upya na kujipenda jinsi ulivyo,jinsi ulivyoumbwa,na si jinsi wengine wanavyotaka uonekane....usiwaache wengine wakuchagulie maisha yako...usiache yaliyopita yakakuchagulia jinsi utakavyokua.
Tazama ulivoshinda vikwazo,kisha chukua nguvu ya ushindi wako na songa mbele.Unaweza na maisha yanaendelea.Amka...songa mbele

AHSANTE WOTE


Rafiki wa kweli ni yule ambaye unaweza kumwamini,ni yule ambaye unaweza kumshirikisha furaha,huzuni na kila tamanio la moyo wako,ni yule ambaye hakuhukumu kwa kufikiri tu,ama kusikia toka kwa wengine,ni yule anayekubali na kuheshimu maamuzi yako,uchaguzi wako na uhuru wako,ni yule ambaye yupo tayari kutumia alichonacho kwa ajili yako,ni yule anayeweza kukukosoa na kukufanya utambue njia bora na kukua ukiendelea mbele daima,hutambua umuhimu wako na kukupa moyo,kukuamsha uwe bora zaidi na kufikia mafanikio,Hukusikiliza na kukushauri pale panapostahili na unapohitaji...daima huwa kwa ajili yako..rafiki wa kweli hawezi kuwa na ajenda za siri,hawezi kukuzunguka n A KUKUSALITI...rafiki wa kweli hufurahi pale unapofanikiwa na si kuweka kinyongo na kuumia pale unapofanikiwa,daima huwa pamoja nawe......na ni furaha kubwa pale unapogundua kuwa rafiki yako mkuu ni wewe mwenyewe....furaha pia ni kumpata rafiki wa kweli ..ni wachache....daima nafurahi kupata marafiki wa namna hii..nitakuwa sina fadhila kama sitasema ahsante itokayo katika furaha ya moyo wangu