Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Monday, January 7

WAKATI NI SASA


Ulishawahi kujiuliza ni lini unasubiri ,ama ni lini umeamua kuanza kutimiza yale ambayo umepangilia kuyafanya maishani?Umewahi pia kujiuliza  ni lini malengo yako yatatimia?
Kama unatambua kuna sababu ya wewe kuishi hapa duniani,unasubiri nini kutenda kadiri moyo wako unavyokutuma?Unasubiri kesho,kesho kutwa,mwisho wa mwezi ,ukihitimu masomo,ama unasubiri umri wako ufike miaka kadhaa?
Ipo siku hutakuwa na uwezo wa kutenda chochote,hutakuwa na nafasi ya kutenda kile ulichokuwa kutimiza,na wakati huo ndipo utakapokuwa na majuto ni kwa nini hukutenda pale ulipoweza.
Hakuna muda mwingine zaidi ya sasa.Matokeo ya mambo yote yajayo hufanywa na maamuzi ya wakati uliopo.AMUA sasa.Amua kuanza kuishi maisha uliyoyakusudia sasa.
Utatambua kila kitu juu ya maisha yako ukianza kuchimba ndani yako sasa.Anza kusikiliza sauti iliyopo ndani mwako sasa.Usisubiri mwisho,fanya kwa bidii sasa.Badili maisha yako na ndoto zako zote kuwa halisi sasa.Usisubiri hatari ya kusubiri kesho,baadae….Mavuno ya baadae ni matokeo ya kupanda sasa

Saturday, January 5

ATHARI ZA MSUKUMO WA WANAOKUZUNGUKA

Watu wanaotuzunguka hutusukuma kufikiri na kutenda kadiri ya kanuni  na imani zao na kutufanya kuwa watumwa wa fikra za kimitazamo(picha na www.nlm.nih.gov)

Nilikwisha kujadili ni namna gani mafanikio ya mtu yanaanza ndani mwako,   soma zaidi hapa
Katika makala hiyo,tunajifunza kuwa kila jambo huanza na wewe.Chochote kinachoanza na msukumo utokao ndani yako,ndilo linaloleta mafanikio.Kwa kifupi tu mafanikio ya mtu yanaanza na yeye mwenywe na si msukumo utokao nje yake yeye.

Leo tutajadili jinsi msukumo wa nje (toka kwa marafiki,ndugu na wote wanaokuzunguka unavyowezakuathiri upekee wako na maamuzi.

Tumejifunzapia kuwa kila mmoja ni wa kipekee kwa maana ya nafsi yake na atasimami katika maamuzi yake na ujenzi wa maisha yake.Lakini tunaishi katika jamii ambayo inatutia msukumo wa kuamua na kutenda kadiri ya mawazo na kawaida yao.
Kabla hujazaliwa walikwepo waliotutanguli,kwa maana ya babu zetu na wengine wengi waliopita.Hawa walitengeneza mfumo yao ya maisha  ambayo tunaweza kuuita mfumo wa jamii,ambao ulijenga matarajio mengi ya watu mmojammoja  na jamii nzima.Mfumo huu ni pamoja na kanuni,mila ,desturi,imani,dini,serikali,sherehe.Mfumo huu umejengwa na sheria na kanuni nyingi ambazo unapozaliwa tu,unakuwa umefungwa moja kwa moja na mfumo huo pasipo kupenda ukiamini ndio mfumo sahihi.Sheria na kanuni zilizopo katika mfumo huu ulioukuta zinapokuwa kawaida kwako,zinaufanya mfumo wako wa tafakari uwe na uelekeo na fikra zilizo ndani ya mfumo huo.
Fikra zenye mipaka huleta matokeo yasiyo huru (picha kwa hisani ya www.rfidgeneral.com)


Mfumo huu unakulazimu kujifunza na kufuata mengi kama ni nini unapaswa kufuata,kuamini,ni nini kinakubalika na nini hakikubaliki,kipi ni chema na kipi ni kibaya.MFUMO HUU WOTE UNAKUPELEKA KUFUATILIA KILA JAMBO KADIRI YA TARATIBU NA MAWAZO YA MFUMO.Maka unapokuwa unakuwa na fikra za kimfumo kuwa jambo fulani lipo hivi tu,na hivyo mara nyingi hujenga mpaka wa kufikiri na kuamua.Unakuwa huwezi kufanya jambo mpaka usikilize waanaokuzunguka wanasemaje.
Natoa mfano wa mjomba wanguambaye pale alipotakakuoa binti ambaye walikubaliana na kupendana,alibadilisha uamuzio baada ya kuambiwa tu eti dini anayoiamini binti huyo si nzuri.Hapo dini ikawa juu ya upendo.
Pia kuna rafiki yangu mmoja alikuwa akijadili na marafiki juu ya imani ya dini nyingine,akashawishiwa kuifuata imani mpya,akakiri kuridhika na imani hiyo lakini hofu yake ikwa je,wazazi watanionaje?,licha ya kuwa yeye ni mkubwa kiumri.

Hii ni baadhi tu ya mifano.Mwisho kbisa tunaanza kuitazama  dunia kama sehemu ya ushindani.Tunajifunza uchoyo,ubinafsi,usiri na visasi kwa sababu ya mfumo licha ya kuwa yapo mengi mazuri.

Ushindani huo unatufanye tufikiri na kutenda kwa kuangalia mitazamo ya jamii.Unakuwa huna fikra za kutafakari jambo nje ya mipaka ya jamii.HIVYO unakuwa si huru katika maamuzi juu ya maisha yako mwenyewe.Kwa kifupi unakuwa mtumwa wa mfumo huu wa jamii.,ukifikiri na kutenda katika uwanja wa fikra za jamii.Ukweli ni kwamba usipotoka katika mpaka huu na kuuvuka,kuwa huru,hutaishi kamwe maisha yako halisi.
Maisha yetu ni matokeo ya fikrazetu (picha kwa hisani ya mtandao)


Ninachotaka kukisema hapa ni kuwa ukitaka kuishi maisha unayoyachagua wewe ,na kufikia mafanikio ni lazima uchukue uamuzi wa kufikiri nje ya mipaka ya mawazo ya jamii.Ni lazima uvunje mipaka ya mazoea na ile ya sheria na kanuni za imani ya jamii.Ni lazima ujifunze kuwa huru.Naomba nieleweke vizuri hapa si kwamba nahamasisha watu wavunje sheria za nchi ama mahalia,laaah,kuvunja mazoea ni kufikiri kwa mapana bila kufungwa na mawazo yanayoaminika tu na jamii.


Imani ya jamii ina nguvu sana,na hujenga upotofu ya kuwa tunapaswa kufikiri hivi na si vile,fulani yupo hivi na vile na inamsukuma mtu kutenda kadiri ya fikra za jamii husika.Tunalazimika kuishi maisha ya bandia ili tuonekane kwa wengine(Amini nakwambia utakuwa mtumwa katika mawazo mpaka pale utakapopanua wigo /uwanja wako wa fikra).

Unakuta jamii inaamini juu ya ushirikina na uchawi katika kutafuta mafanikio,hivyo kunakuwa na imani kuwa huwezi kufanikiwa mpaka uende kwa mganga.Watoto wakiugua magonjwa mabayo ni matokeo ya maisha anayoishi basdi inaaminika amechezewa(amelogwa).Tukumbuke kuwa mtu hawezi kukutendea ubaya  kama wewe si kisababishi cha fikra za mtu huyo kukufanyia ubaya.Nakumbuka kuna rafiki yangu ambaye nilisoma pamoja nae,alikuwa namsukumo sana kwa wengine,akiwaaminisha kuwa ili uwe bora na rafiki yake ni lazima uwe unakunywa pombe ama kuzisifia.Hii yote ni matokeo ya imani na fikra za kimfumo.

Hivyo tukumbuke kuwa kama tunaishi tukifikiri na kutenda kwa mipaka ya imani za wengine,basi sisi ni watumwa wa imani hizo mpaka pale tutakapotoka nje ya mipaka hiyo katika kufikiri na kutenda.Tunatafuta kukubaliwa na mawazo na mitazamo ya vikundi fulani.Tukumbuke kuwa picha halisi juu ya kinyago huwa sahihi kwa mchongaji,ambaye anachonga akiwa na picha yake katika fikra kuwa nataka awe hivi.Ukiwauliza wateja wanaonunua kinyago,kila mmoja atatafsiri kadiri ya fikra zake pia.
Mabadiliko katika fikra na maendeleo yako yanaanza pale unapoanza kufikiri nje ya mipaka ya wengine(picha kwa hisani ya mtandao)


Kwa nini uishi kwa mawazo ya wengine?Kwa nini uumie unapoambiwa una sura mbaya wakati hayo ni maoni ya msemaji tu.Ukitaka kupata majibu juu ya maisha yako,chimba ndani yako..Tafuta ndani yako.Ninaamini kila jambo huanza na wewe(mimi),Utajiri na mafanikio yote yanatoka ndani mwa muhusika.Zawadi kubwa juu ya maisha yako ni kuithamini nafsi yako  na kuisikiliza sauti kubwa itokayo moyoni mwako,ikuongozae juu ya kutenda,hii ni sauti ya Mungu iletayo mafanikio,furaha na kila lililo jema.Sauti hii inakupa nguvu ya kutenda miujiza kila wakati,ndiyo inayofanya nuru ya maisha yako ing'ae.

Jamii inakufanya ulazimike kuenenda kimawazo na fikra kadiri ya imani yake.Kwa nini usikuballi jinsi ulivyo na kuanza kuchimbandani yako palipo na siri kuu ya maisha yako?Mimi binafsi natambua jinsi ninavoonekana.Najikubali kwa kuwa mimi ni zaidi ya nilivyo.Ukiachilia mbali mazingira ninayoishi na sura yangu,mimi ni wa thamani,kama wengine.Wewe ni wa thamani jinsi ulivyo,na thamani yako ni sawa na binadamu wote.Unao uwezo wa kuwa na kuishi maisha ya furaha na mafanikio.Unastahili,wewe ni Matokeo ya kazi kubwa ya Mungu. 



Sasa anza kujikubali na kuepuka misukumo ya wale wanaokuzunguka.Anza kutazama uwezo ulio nao,tazama chemchem ya mafanikio iliyopo ndani mwako.Sisi sote ni bora .Sisi wote ni wamoja.
Huu ni wakati wa kujifunza kuwa wewe,kujikubali,kukua na kubadilika.Anzakujitambua wewe kisha utatambulika kwa wengine.Hongera kwa kujitambua

Ahsante. Joseph Pongu-0717903089,0765046644.Karibu tujadiliane na kuinuana.

HATUTAMUACHA HATA MMOJA 2013


Tumejifunza mambo mengi kwa mwaka 2012,ambayo yametufanya tutambue sisi ni akina nani na kwa nini tupo hapa duniani.Tumetambua kuwa sisi ndio wasanifu wa maisha yetu wenyewe.Tumejifunza kuwa kila jambo ni jema likitazamwa kwa mfumo chanya na kuwa mambo yote yatokeayo maishani mwetu ni matokeo ya fikra zetu na vitendo vyetu wenyewe...Tumejifunza kuwa upendo ndio silaha ya mafanikio ya kila jambo,upendo ni nuru.tumejifunza pia matokeo yake ambayo ni pamoja na furaha,amani,umoja,uvumilivu na ni mafanikio.Tukajifunza pia kuwa kinyume cha upendo ambayo ni chuki ndiyo matokeo ya maumivu,wivu,visasi,chuki,masengenyo na ndio matokeo ya kila jambo liletalo hasara katika maisha yetu
SISI NI WASANIFU WA MAISHA YETU WENYEWE
 

Leo hii tutajikumbusha kuhusu majukumu yetu …Mwaka mpya ulioanza tuuutazame kwa uchanya wake.Tuanze sasa kutimiza malengo yetu kila mmoja ya kuwepo hapa duniani.Kila mmoja wetu anayo majukumu yake.Kila mmoja ana wito unaomuita ndani mwake,ana sauti ya Mungu ndani yake inayomuita kutenda kwa ajili ya wengine na kuifanya dunia kuwa sehemu bora ya kuishi

Hakuna hata mmoja wetu ambaye hatayapitia magumu,kwa sababu bila magumu kutokea hatuwezi kuendelea.Mwaka huu ni mwaka wa kusonga mbele ...tutasonga mbele,hatutamuacha hata mmoja nyuma
Ni mwaka ambao mwalimu anayeishi katika mazingira magumu yenye milima mingi,ataamka kila siku na kufundisha kwa bidii na kuwanyanyua wengine wengi.Anahitajika huyo ambaye hatalalamika na kusubiri serikali(kwani serikali ni kila mmoja wetu) bali atakuwa ni mfano wa kuigwa wa mbinu bora za kutatua matatizo.Mwalimu popote ulipo amka na kutenda kwa ajili ya wengine.Amka mwalimu.

Sauti ya upendo husikika kwa viumbe vyote.Huu ni mwaka wa kuwa nuru kwa wengine(picha toka helped by animals kwa msaada wa mtandao)


Ni mwaka ambao daktari ataamka mapema na kukumbuka jukumu lake ,ya kuwa hayupo tu kwa ajili ya kutazama idadi ya wagonjwa na kiasi cha fedha,bali yupo kwa ajili ya upendo,akijali utu wa wengine pasipo kubagua hali,kabila,rangi ama hali yeyote na daima atahesabu mafanikio yake kwa kuokoa wengine,kuwainua walio kata tamaa.....na hata akitokea mtoto akaulizwa upendo ni nini,basi amtazame daktari kwa ujasiri akisema......huu ndio upendo.

Ni mwaka ambao kila anayetoa huduma kwa wengine,atatoa akisukumwa na upendo.Kila atazamapo wengine,atambue kuwa anajitazama yeye,na kuwa thamani yake ni thamani ya wengine wote.Anapowatendea wengine akumbuke kuwa anaitendea nafsi yake.Ni mwaka ambao sisi tulio binadamu tutaonesha upendo uliotukuka,utakaofanya nuru ya Mungu iliyo ndani mwetu iwaangaze binadamu engine wasiotambua upendo,ili nao waishi maisha ya upendo.
Sisi ni wamoja,sisi wote ni wana wa Mungu,tofauti zetu zimejengwa na woga ,fikra zetu


Huu ni mwaka ambao tunapaswa kuifanya dunia kuwa sehemu bora,ili nasi tuwe malaika wa dunia hii.

Binafsi jiulize utamtendea nini yule Mungiu ambaye yupo ndani mwako?Je ukiwa katika nyakati za faragha na Muumba wako,utajivunia lipi ulilomtendea?Kumbuka kuwa kama huna malengo ya kutenda jambo lolote huwezi kutimiza lolote.Ni sawa na kusafiri safari isiyojulikana,mahali na hata uelekeo!Tukiweka malengo na kuamini katika kuyatekeleza,hakika yatatimia.

Mimi binafsi najisikia faraja sana kuhamasisha wengine na kuwasaidia wengine waweze kufikia mafanikio HASA PALE WANAPOKUWA NA MSUKUMO UTOKAO NDANI MWAO.Nimejitolea kwa ajiliya wengine na wakati wote najisikia faraja.Ninapokutana na magumu,ninayashinda kwa sababu naamini katika ushindi.Sisi  tumeumbwa kushinda.,na ushindi ni matokeo ya usanifu katika fikra za kila mmoja.

Ninapata faraja ninapoona kuwa yupo nesi ambaye licha ya kwamba anaumwa,anaamka na kwenda kazini kwa ajili ya wengine.Ninafarijika ninapoona kuwa yupo mtu ambaye licha ya kuwa na magumu mengi,anatenda ka ajili ya wengine pasipo kutegemea malipo.Nilikwenda kijijini nilipozaliwa,nikakutana na mama ambaye kipato chake ni kidogo,anaumwa kwa miaka mingi lakini anajitolea chakula na malazi kwa ajili ya wengine....anawafariji wengine,hata anapokuwa katika ugumu sana,hakati tamaa.Maisha yake ni nuru kwa wengi.Daima hamuachi jirani akiwa katika huzuni,nuru yake inaishi.Ni mwanga kwa waliokosa nuru.

Nafarijika kuona wengi ambao wanakwenda mbali na familia zao,mbali na wapendwa wao kwa ajili ya wengine. 
Nafarijika pia kuona wengi ambao wanajinyima kwa ajili ya wengine.Wengi wao wanaishi maisha ya kawaida,(kwa maana ya kipato) lakini wanatambua maana ya thamani yao kwa wengine,wapo tayari kujitolea pasipo kutambuliwa na wengine.Hii inanipa faraja ya kusonga mbele.Hwa wanatambua kuwa sisi binadamu wote ni wamoja ,tofauti zetu ni juu ya fikra zetu wenyewe.

Daima umoja ni nguvu.Usisubiri wengine wachukue hatua.Anza wewe.Mimi nimepata nafasi hii kwa kuandika.Wewe pekeyako pia watosha,unaweza kubadili wengine kwa kusamehe,kuimba,kufundisha,kutoa nakala nyingi za mafunzo kwa wengine,kwa kuwahurumia wengine,kutembelea wagonjwa,yatima,wafungwa na matendo yote yenye kuleta thamani kwa wanaotuzungua.Mwaka 2013 hatutamuacha mtu hata mmoja katika umasikini,chuki,uvivu,visasi,magonjwa huzuni...nk.Mwaka huu hatutamuacha yeyote kwenye giza.Tunao uwezo wa kuyatenda haya yote.Chukua hatua,mabadiliko yanaanza ndani yako.
Wathamini wengine,hata usiowafahamu....

Tujenge mwili mmoja,moyo mmoja na kupambana mpaka mwisho kwa ajili ya dunia iliyo bora na mafanikio kwa ajili yetu na wengine.

kila mmoja wetu anapochukua hatua licha ya vikwazo,tutayafika mafanikio(picha kwa msaada wa mtandao)




Tuishi maisha yetu kwa dhati bila uoga,tuchimbe ndani ya mioyo yetu ambapochemchem ya kila ushindi ipo,Tujifunze thamani yetu ,tuwathamini wengine kwa kuwa wao ni wa thamani kama tulivyo,tusamehe na kutazama mbele,tujali mawazo ya wenginena imani zao tuziheshimu.


Kila mmoja apende nafsi yake,ayapende maisha yake,asanifu vyema vyote vinavyomzunguka,KILA MMOJA AYAFANYE MAISHA YAKE YA THAMANI KWA WENGINE.Tutimize malengo yetu,yanayotokana na sauti iliyopo ndani mwetu,ili ule muda wa kuishi katika dunia hii unapokwisha ,na kifo kukuita,uitike kwa furaha,kwamba uliyaishi vyema,usipate hata sababu ya kuomba upewe tena muda,bali nuru ya maisha yako iwe mfano wa kuigwa milele.Uiage dunia na kuondoka kishujaa,kuelekea katika maisha mengine mapya yenye majukumu mapya.


Tutapita katika magumu mengi lakini daima tutasonga mbele,hatutamuacha yeyote nyuma,tutainuana sisi kwa sisi,hatutatazama nyuma,wala kuogopa kusonga kwa woga wetu,hatutaogopa lolote kwani sisi ni wa thamani,tutakumbuka daima kuwa dunia si sehemu ya ushindani bali ni sehemu ya ushirikiano na umoja na hivyo daima tutafikia tuendako,kwa sababu Mungu yu ndani mwetu.
Ahsanteni sana

Monday, December 31

UKWELI KUHUSU WEWE

Wewe ndiye mjenzi na mbomoaji wa maisha yako katika nyanja zote kwa fikra zako kwani fikra ndiyo mbegu ndani yako itoayo matokeo kadiri ya sababisho litokanalo na msukumo wa kimazingira. Hivyo mafanikio yako huja kwa kupanda fikra za mafanikio na kutofanikiwa huja kwa kupanda fikra za kushindwa,uma kwa kujua na kutojua.
Wewe ni msanifu na mjenzi wa maisha yako(picha na cognitivesocialweb.com)




Wewe ndiye unayebomoa na kuangamiza maisha yako kwa fikra zako,kwa kujua ama pasipo kutambua(picha na hot100tips.com)

Kamwe huwezi kufanikiwa kama hujui unachokitaka,huwezi kuona mbele pasipoonekana kama hufahamu uendapo,ni mpaka pale utakapojua unataka kuwa nani,ndipo utakapokuwa.....ni sawa na kwenda safari isiyojulikana hata uelekeo.

Mungu alipokuuumba alikupa nguvu na uwezo,akaifanya dunia na vyote vinavyokuzunguka vitii maagizo yako,hasa yale yanayotokana na msukumo wa moyo wako..hivyo wewe ni kiumbe bora jinsi ulivyoumbwa,wewe ni aidi ya ulivyo,wewe ni upendo,amani,faraja,chuki,visasi,wewe ni mwerevu,na msanifu wa maisha yako mwenyewe,hivyo hupaswi kumlaumu yeyote kuhusiana na jambo lolote linalohusu maisha yako,chukua hatua juu ya maisha yako mwenyewe.

Ndani yako ni chemchemi ya kila hali iletayo matokeo hasi ama chanya,ukifikiri kuhusu upendo utafute ndani yako,ukitaka kujua kuhusu uwezo ulio nao,utafute ndani yako,ukitaka kujua kuhusu mafanikio yako,tafuta ndani mwako...chemchemi yako haileti faida kama hujachukua maamuzi

Huna tofauti na binadamu mwingine kwa maana ya uwezo......anza kwanza kuuchunguza ubora wako uujue,ukiutambua,utambue kuwa wengine ni bora kama wewe,hivyo matendo yako yazingatie matokeo yake,fikra zako ziwe fikra njema juu yako na kwa wengine kwani kila utendalo kwa wengine,umejitendea mwenyewe.Maisha ni uchaguzi wako,na matokeo ya kila unachochagua ni juu yako.

Fikra zitokazo kwako ni sewa na bustani ama shamba,inaitaji kutazamwa na kupaliliwa...kuhakikisha kuwa unapanda mbegu bora,ukipanda mbegu isiyo bora (fikra mbaya dhidi yako na maisha yako) huleta matokeo sawia na mbegu uliyoipanda.

Maisha unayoyaishi hayatokei kwa kiitwacho bahati(nzuri ama mbaya) bali ni matokeo ya uchaguzi wako mwenyewe ama kwa kutambua na kutotambua.Umasikini,utajiri,furaha,huzuni,amani,chuki,upendo vyote ni matokeo ya uchaguzi wa maisha yako.Nguvu na uwezo wa kubadili matokeo hayo hutoka ndani mwako....Ni msukumo utokao ndani mwako pekee ndio utakaobadili maisha yako.

Kamwe wewe huvuti maishani vile vitu unavyovitamani ama maisha unayoyatamani,bali unavuta jinsi ya fikra zako.Fikra a ushindi huleta ushindi,fikra za kushindwa huleta kushindwa.

Mara nyingi unajaribu kubadili hali ama mazingira yanayokuzunguka pasipo kubadili fikra zako juu ya mambo hayo....Jinsi uvitazamavyo vitu huwa...ukilitazama jambo kwa uchanya wake,basi kila hali huwa ni nafasi,kama ni mtazamo hasi,basi matokeo yake huwa hasi na kwako huwa ni maumivu.

NURU NA GIZA

Bila shaka kila mmoja yu na furaha siku ya leo.Karibu tena katika somo jipya leo hii.Somo hili litakufanya utambue jinsi wewe ulivyo muendeshaji wa maisha yko,ni somo litakalokufanya ujue kuwa wewe ndiye mjenzi na ndiye unayebomoa maisha yako mwenyewe,iwe kwa kutambua ama kutotambua.Karibu tujifunze pamoja

Ni mara nyingi tumekuwa tukikumbushana kuwa Mungu ametuumba kwa mfano wake,kwa kutupatia uwezo wa kutenda kama yeye.Naye hujidhihirisha kuwepo kwetu kwa njia ya upendo,ni sawa na kusema upendo ni Mungu ndani yetu.Upendo ni nuru ya Mungu iliyopo ndani yetu.Hivyo kila jambo litendwalo kwa msukumo wa upendo hufanya nuru ya Mungu iliyopo ndani yetu hung'aa.
Upendo ni nuru,kama nilivyoeleza hapo juu.Kinyume chake ni chuki,ama giza. Kila tutendapo jambo kwa chuki,basi nuru huzimika ndani yetu  na linabaki giza


Upendo ni nuru iliyo ndani ya mioyo yetu,kila tutendapo kwa upendo maisha yetu huwa nuru kwa wengine (picha kwa msaada wa mtandao)


 Giza ndani ya mioyo yetu hutokana na kutoweka kwa mwanga,yaani kutenda pasipo upendo.Inamaanisha visasi,migogoro,ugomvi....yote hii huipoteza nuru iliyopo kwako.Ama kwa kutambua na kutotambua,unayajenga maisha yako kwa uchaguzi wako mwenyewe,ambao hutokana na kutenda kwa upendo ama kinyume chake (giza).Ni sawa na kusema tunayafanya maisha yetu kung'ara ama kufifia kwa maamuzi yetu wenyewe.
Atandaye kwa upendo hulipwa upendo.Moyo wake hujawa furaha na hivyo hufungua njia ya mafanikio katika kila jambo alipendalo.Huamsha mwili wenye uchangamfu na uso uliojawa bna furaha na amani.Nuru yake hung'aa daima.Hata siku zake za kuishi hapa duniani zinapokwisha,huenda kwa amani.Nuru yake huendelea kung'aa vizazi hata vizazi.Mifano ipo mingi
Mfano wa kwanza ni ule wa Yesu,Kristu (mnazareti).Huyu alifanya kila jambo kwa kusukumwa na upendo.Alitoa maisha yake kwa ajili ya wengine.Alifundisha upendo kwa kutenda na kuuishi.Akawa faraja kwa wote ambao walikuwa hawathaminiki katika jamii.Hata alipoondoka,wengi wa wafuasi wake na wasio wafuasi wamezidi kumkumbuka,na hata sasa wanaozaliwa baada yake hukumbuka na kumtambua kwa kupitia matokeo ya upendo .Wengine ni wengi ambao tumekuwa tukiwasikia ama kupata kuwaona katika jamii yetu.
Kutenda kwa upendo humaanisha kujali,kuthamini wengine.
Sisi ni wa thamani kwa sababu Mungu yupo ndani yetu.Hivyo kila unapojitazama na kujikumbusha thamani yako,kumbuka ya kuwa kila anayekuzunguka ana thamani sawia na ile uliyonayo,hivyo kila utendalo kwa wengine,umejitendea wewe.Unapotenda kwa upendo kwa wengine,umejitendea wewe,vivyo hivyo,unapotenda kwa wenako kwa chuki,basi umejitendea mwenyewe.
Upendo ndio lugha ya pekee inayounganisha viumbe wote duniani(picha kwa msaada wa mtandao)
 

Hivyo kwa maelezo hayo juu,tunajifunza kuwa sisi tunajenga ama kubomoa maisha wetu wenyewe kwa uchaguzi tunaoufanya wenyewe.Katika kila huduma unayoitoa,iwe ni elimu,biashara..ukitenda kwa upendo unafanikiwa.Ukitoa huduma kwa chuki unadidimiza mafanikio yako mwenyewe,iwe kwa kutambua hilo ama kutotambua.Chukua mfano unafanya biashara;wanapokuja wateja unawachangamkia kwa furaha na upendo..ukiwahudumia vema na kuwapa ushauri mzuri na ukatenda kinyume chake,ni lipi kati ya matendo hayo juu itakuletea mafanikio?

Nuru ya Mungu iliyopo ndani mwetu haifichiki kamwe,viumbe vyote duniani huvutiwa na nuru hiyo
Tunapokianza kipindi kipya katika mpangili wa miaka,tukumbuke kuwa tutahesabu mafanikio ama kutofanikiwa katika malengo yetu kwa  kuchagua wenyewe,nuru ama giza

Kuna furaha kubwa kwa wale wanaouchagua upendo,furaha huwa daima maishani mwao,na daima nuru ya Mungu iliyo ndani mwao hung'aa daima na kuwafanya wengine wajifunze toka kwao.Heri ya maandalizi ya kipindi kipya cha mwaka 2013.


Friday, December 7

Kumbuka wimbo wako




Katika dunia hii ni vema kuyaishi maisha yako pasipo kuigiza,yawe yako halisi..Ukiyaishi kwa juhudi zako,hutapata kuwa na wasiwasi juu ya kifo na matokeo yake...Waheshimu wengine wote,heshimu imani zao,fikra zao na mitazamo yao.Yapende maisha yako,furahia maisha yako,heshimu maamuzi yako katika maisha,sikiliza hisia za moyo wako...Fikiri kuishi maisha marefu yenye thamani kwa wengine.Kila ukutanapo na watu,wafanye watambuae nuru ya Mungu iliyo ndani mwako...ing'ae kwao,nao wajifunze kutoka katika nuru hiyo,na kuwafanya nao pia waishi maisha yao halisi yenye thamani kwa wengine....Wathamini wote,wageni kwa wenyeji...Kila uamkapo tafakari thamani yako na nafasi uliyonayo kutenda makubwa zaidi..shukuru kwa siku mpya,Kama hutaona sababu ya kushukuru,basi ndani yako hujautambua mwanga,na utaidanganya nafsi yako mwenyewe..: Na pale wakati wako wa kuyaendea maisha mengine mapya hutapatwa na woga,wala wasiwasi juu ya yajayo.....usiogope kama wale ambao kifo kikiwajia hujaa hofu na kuomba muda kidogo wa kutekeleza yale ambayo hawakuyatilia maanani pale waliposukumwa na mioyo yao kutenda...Kumbuka wimbo wako...wa kumkaribisha rafiki yako,atakayekupokea katika maisha mapya,kifo...kisha aga dunia kwa furaha,kwa sababu uliishi vema..kishujaa.

Tuesday, December 4

IAMBIE NAFSI YAKO

 Tumeumbwa na kupewa mamlaka juu ya maisha yetu na juu ya kila kilicho juu ya nchi,Hivyo tunapaswa kukumbuka kuwa kila kitu tunachokihitaji maishani mwetu kipo katika uwezo wetu tuliopewa na Muumba...mradi tu ulihitaji jambo hilo kwa dhati kabisa toka moyoni mwako....
Kwa kutambua hilo huna sababu ya kuwa na wasiwasi juu ya maisha na juu ya kesho....iambie nafsi yako kwa dhati kabisa toka moyoni yakuwa Unaweza.
Unaweza kuwa imara kuliko hofu uliyonayo,
Unaweza kabisa kuwa na afya bora,furaha na amani,
Unaweza pia kuwa sababu ya vyote hivyo kwa wengine,
Unaweza kuwafanya wengine watambue kuwa wao ni nuru,nao wanapaswa kuifanya nuru hiyo iangaze wengine
Kuafanya wayatazame maisha katika upande wa mwangaza

Iambie nafsi yako kuwa,
Unaweza kubadili maisha yako na kuyafanya kuwa nuru,
Unaweza kufikiri chanya na kutenda kwa uwezo wako wote
Kuwa chachu ya mabadiliko chanya duniani,na kuwa mfano wa kuigwa

Iambie nafsi yako yakuwa unaweza kusahau yaliyopita,
ambayo yalikusababishia maumivu,na kuishi maisha yenye furaha na matumaini,ukianza upya bila woga,
Unaweza kuwapenda na kuwajali wengine pasipo kutazama maumivu ama mabaya waliyokutendea
Unaweza kusimama imara hata katika nyakati za magumu mengi
        furaha ni pale unapotumia maisha yako kuwa furaha kwa wengine-unaweza kuwa chachu ya upendo na anani


Sema kwa nafsi yako kuwa unaweza
Kuishi bila kusengenya na kuwanenea wengine kwa ubaya,bali unaweza kuwa faraja kwa watu wote,
Iambie nafsi yako kuwa wewe ,ukiwa kama nafsi huru,
Una jukumu la kutenda hapa duniani,
Iambie nafsi yako itazame kwa kina,
Ichunguze umuhimu wa maisha yako hapa duniani
Na kisha kuamua kufanya dunia kuwa sehemu ya upendo