Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Saturday, September 1

YALIYOPITA YAMEPITA...SONGA MBELE

Wapo wanaotazama mambo ya jana,juzi na yote waliyoyapitia na kukata tamaa,Wakisikia jinsi marafiki wao wanavyowanenea mabaya,wakitazama kila pande na kuhisi hakuna anayewajali,wakiangalia pande zote wasione tumaini,hukata tamaa lakini ukijitambua hutakata tamaa kamwe,kwani utatambua kuwa ni Mungu na wewe ndiye uliyetumaini juu ya yote...Hutaweka matumaini kwa wengine tu,bali utajifunza kuwa wewe ndiye unayepaswa kuchukua hatua juu ya maisha yako.
Maumivu tuliyopitia hutupatia juhudi mpya na uwezo mpya.Yote wanayokunenea wengine hayatakufanya uwe vile wanavyotaka ama kudhani kuwa utakuwa hivyo,bali uamuzi wako utayainua ama kudidimiza maisha yako mwenyewe.Utaacha aibu na woga wa kufanya jambo kwa kuogopa kuwa wengine watakucheka ama kusema vibaya juu yako.Jibu kwao ni mafanikio utakayoyapata,ambayo yatawafunza wao pia.Hutajiona kuwa hustahili kuwa unavyopenda,bali sasa utaamua na kujipenda,ukiishi kwa ajili ya wengine pia
Kila jambo huwa na sababu ya kutokea,ukitazama yaliyopita kwa moyo mweupe,utafurahi kupita huko,kwani ndiko kunliko kuinua na kukufanya uwe imara zaidi..Ndipo sasa utakapoanza kujitazama upya na kujipenda jinsi ulivyo,jinsi ulivyoumbwa,na si jinsi wengine wanavyotaka uonekane....usiwaache wengine wakuchagulie maisha yako...usiache yaliyopita yakakuchagulia jinsi utakavyokua.
Tazama ulivoshinda vikwazo,kisha chukua nguvu ya ushindi wako na songa mbele.Unaweza na maisha yanaendelea.Amka...songa mbele

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com