Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Thursday, July 26

KUMBUKA YAFUATAYO UNAPOPATA HOFU NA KUVUNJIKA MOYO

 Upo wakati ambapo tumnapita katika magumu ,huwa tunafika wakati tunashindwa kujitambua,na wakati mwingine tunapatwa na msongo mkubwa wa mawazo hata tunakata tamaa.Kila wakati jitazame ndani mwako,usome uwezo wako ulio ndani mwako...utaondoa hofu,woga na kukata tamaa.Jikumbushe ya kuwa wewe u bora vile ulivyoumbwa.....wewe ni bora kwa sababu zifuatazo


   Wewe  ni wa pekee,unaipenda nafsi yako,hivyo unampenda Muumba wako na watu wote   pasipo kujali sura,rangi,kabila,dini , na hivyo upo katika uhuru na usalama pote ulipo

  • Unatambua kuwa furaha,amani havitoki nje yako na kwamba furaha ya kweli huanza ndani yako
  • Wakati wote katika maisha yako unaishi ukithamini wengine na kuhakikisha kuwa wewe ni sababu ya wengine kuamka na kufanikiwa,hivyo unapata marafiki na ndugu kwa maisha yako halisi,hivyo wote anaoutambua mchango wako,wanathamini maisha yako.
  • yote yaliyopita kwako,hayakufanyi uwe mnyonge bali yote hayo yalikuwa ni mwanzo wa wewe kuyaendea mafanikio,na hivyo daima utatazama sasa(wakati uliopo) na kuyaandaa maisha yako yajayo kwa kujali pia maisha ya wengine.
  • unatambua kuwa kuanguka(kushindwa) si mwisho wa maisha ,bali ni mwanzo wa kuuelekea ushindi na kadiri unavyoshindwa mara nyingi,ndivyo unavyokuwa mpya kupambana na huhesabu ni mara ngapi umeanguka,bali ni mara ngapi na namna gani umesimama na kushinda.
  • unatambua ya kuwa katika maisha hakuna jambo lililo baya kama kukata tamaa,hivyo magumu hayatakupoteza katika lengo uliloliweka,bali yatakupa mbinu mpya za kufika uendapo.
  • kwa kuwa kila jambo unalolitenda linasukumwa na upendo,na daima unafurahi kuona wengine wakifurahi,unajitolea,unatazama wengine kwa huruma,unawakumbuka wenye mahitaji,hivyo yote yaliyo mema unaowatendea wengine yatakuja kwako pasipo wewe kutegemea.
  • kwa sababu  unayo imani,unayo matumaini na upendo na daima unaepuka hasira,masengenyo,woga,choyo na visasi.
  • unatambua kuwa kutochukua hatua kwa kuogopa kufa ama kuumia ni usaliti wa nafsi yako mwenyewe.
  • moyo wako unawapenda wale ambao jamii imewasahau,unawatia moyo wale walioshuka moyo na wenye katika hali ya kukata tamaa,wwe ni rafiki wa waliotengwa,na  tumaini jipya kwa wasio na tumaini.
  • Daima upo tayari kusamehe,unatazama mbele kwa tumaini la maisha mapya,unaitika sauti ikuitayo kwa ajili ya yatima,wafungwa,wagonjwa,wajane na daima unasimama upya kuyafikia matazamio yako.
    • unapokuwa msaada kwa wanyonge,watima,wajane,wafungwa,matatizo yako yote hupata suluhisho(picha kwa msaada wa mtandao)
    • kwa kuwa unakiri na kutambua na kutumia nguvu na uwezo,akili na  uwezo usioonekana uliopewa na Muumba(Mungu)  kwa utukufu wa Muumba wako,na yote utayafanya kwa ajili ya binadamu wote,hivyo utaepuka kudhuru,kuumiza wengine.
    • kwa sababu unatambua tu kuwa,ili kuwa mkuu mbele ya wengine...ni lazima uwe mtumwa kwanza

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 Comments:

Post a Comment

maoni yako hapa