Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Tuesday, July 31

UPENDO,NDOA NA SHERIA

Mwisho wa makala hii utapata kujifunza mambo yafuatayo

  1. ni nini na jinsi gani upendo wa dhati
  2. HOFU-ADUI MKUBWA WA UPENDO
  3. ndoa,furaha,na huzuni katika ndoa-sababu
  4. sheria katika upendo na kushindwa kwa sheria kulinda ndoa
  5. jinsi gani utaishi maisha ya furaha katika ndoa
  6. nafasi yako katika upendo,ndoa.
  7. jinsi ya kuifanya ndoa yako idumu na kuwa na mafanikio kila kukicha
  8. jinsi ya kutazama kila jambo katika mfumo chanya na kubadili maisha yako

                                  UPENDO
 


     Upendo ni mvuto wa asili(nguvu ya asili) usio na shuruti kati ya mtu mmoja na mwingine.Ni lugha ya pekeee ambayo kiziwi,kipofu,mtoto,mzee, na kila kabila huisikia.Ni lugha ya moyoni..Ni NGUVU PEKEE INAYOTIBU,INAYOWEZA KUAMSHA WASIO NA TUMAINI,INAYOONDOA CHUKI,(UPENDO HUSHINDA YOTE).Upendo ndio ishara kuu ya Mungu(MUUMBA-ASILI YA VIUMBE VYOTE),,ni faraja,amani,ni tumaini...Ndio maana katika maandiko toka katika biblia tunaelezwa ya kuwa Mungu ni upendo
       Mara nyingi tumekuwa tukigawa aina mbalimbali kutokana na mazingira yetu na fikra zetu na kupata upendo wa dhati,upendo wa kawaida,lakini ukweli ni kwamba upendo unabaki kuwa ni upendo(unapopungua huo si upendo) na kinyume chake (chuki) inabaki kuwa chuki.Huwezi kusema kuwa unao upendo pasipo kuuishi/kutenda mambo yanayodhihirisha upendo.Upendo ni kutazama kwa huruma,upendo ni kuinua walkio chini,upendo ni kujitolea pasipo kuhitaji malipo,upendo hushinda yote.  
       Kama tulivyyoona hapo juu,upendo ni msukumo wa kiasili kabisa.Hutokana na mvuto wa asili utokao moyoni kwa mtu,na ndio maana nikauita upendo kuwa ni lugha ya moyoni.Kwa sababu ni mvuto wa kiasili,upendo haujengwi wala kulindwa na vitu visivyo vya asili.Fikra zetu zimejengwa kuutazama upendo katika mtazamo wa vitu ama mali.Mvuto huu wa asili huwa haujali rangi,dini,tofauti ya kimawazo ama mtazamo,haujali tofauti za taifa,ukanda ama lugha,kabila,haujali mali wala hali.Ni ukweli usiopingika kuwa kila mtu huweza kumpenda ama kuvutiwa na mwingine si kwa sababu ya dini,ama rangi,ama kabila,ama utaifa fulani,ama mali.....fikra za dini,mali,kabila,taifa huja kwa msukumo wa fikra(zenye athari ya kimazingira) na tamaa.
      Kwa maana hiyo,sitakuwa nakosea nikisema kuwa,upendo (mvuto wa asili) kwa sababu ni asili ya moyo,basi ukitazamwa kwa mtazamo wa vitu visivyo asili(vitokanavyo na fikra za kimazingira) basi huwa si upendo tena bali huwa ni tamaa na udanganyifu.Upendo hauwezi kulindwa kwa sheria,hakuna sheria itakayotungwa kuulinda upendo kati ya watu wawili,na sheria hiyo ikashinda isipokuwa tu,upendo wa dhati hutoka moyoni mwa kila mmoja,nao hudumu na kutukuka toka moyoni mwa wawili hao na ndio maana,tutaona hapo mbele ya kuwa sheria imeshindwa kulinda ndoa na badala yake baada ya sheria kuwa ndio mlinzi wa upendo,ndoa nyingi zimekuwa zikivunjika(zipo sababu nyingine ndogo)
  Tumezaliwa tukiwa na upendo,lakini mitazamo yetu ya kifikra imefanya tuweke matabaka katika upendo,na hivyo hofu imetawala upendo,na kufanya hofu kuwa adui mkubwa wa upendo.
                                                Hofu,adui wa upendo(picha kwa hisani ya mtanzdao)
    Ni hofu ndiyo inayoleta chuki,hofu humfanya mtu kutojiamini na kuhisi wanaomzunguka ni maadui...Ni hofu ndiyo iliyosababisha viongozi wang'ang'anie madaraka,kufanya mauaji,kubagua..Ni hofu ndiyo  inayojenga uhasama.
                              
               NDOA
        Kila unapofikiri kuhusu mwenzi wako,umefikiri kuhusu wewe,unapomtendea mwenzi wako unajitendea wewe,unapomjali mwenzi wako umejipenda mwenyewe,unapomfanya mwenzi wako afurahi umejitendea wewe,upendo hutoka ndani ya moyo wako mwenyewe...pale unapovutiwa na mwingine...pasipo shinikizo litokalo nje ya moyo wako...ukamchagua na kuonesha nguvu hii ya asili kwake,ukishirikiana nae kukua na kuyafikia matarajio ya kila mmoja wenu,hii huitwa ndoa.Ndoa si kupata mwenza ambaye atakufanya uwe kamili(kwa kuwa kila mmoja amekamilika vile alivyo), ni urafiki na upendo uendao mbele ya maumbile.Ndoa ni muumngano wa wawili kila mmoja kwa ukamilifu wake,kwa ajili ya kufanya nuru ya Mungu ambayo ipo kwa kila mmoja,ing'ae kwa kila mmoja ili kuwafanya wawili hao na wale wanaowazunguka waujue utukufu wa Mungu
 Nimetazama ndani yangu na kuuona ukamilifu wangu,nami naungana nawe ili mimi nawe tushirikiane ukamilifu wetu(tafakari kwa kina)
            muhimu:wengi hufikiri kuwa hawajakamilika,wamekosa kitu fulani,na hivyo huingia kwenye ndoa wakitazamia kukipata kitu fulani toka kwa wenzi wao,baadae hugundua kuwa wanachokitafuta hakipo kwa wenzi wao,hapo ndipo matatizo huanza kutokea kwenye ndoa....baada ya changamoto nyingi ,wengine huomba Mungu awabadili wenzi wao,hawatambui kuwa ni fikra zao ndio adui wa ndoa yao(fikra huleta hofu)-(kama wangetambua wangemuomba Mungu abadili fikra zao.-hata ndoa kuvunjika,hutambua kuwa kumbe furaha,amani,upendo,kujali..kunaanza ndani mwao.
               Ndoa ni mungano ambao kila mmoja katika wenza huhakikisha anatumia kila alichonacho kuhakikisha kuwa mwenzi wake anakua na kutimiza yale aliyoyakusudia katka maisha yake.Ni mahali ambapo chemchem ya amani ilipo,ndoa si kifungo...ndoa ni chimbuko la uhuru ,ndoa si hofu,bali ni chemchem ya upendo,umoja na amani,ni mbegu iletayo matunda bora,ndoa ni ishara ya kukubali majukumu,ni chimbuko la kuifanya dunia kuwa sehemu bora
              Kinyume chake katika dunia ya sasa,ndo imekuwa ni sehemu ya watu kukimbia majukumu,ni sehemu ya watu kukwepa kufikiri,kuamua na kutenda...ndoa imekuwa ni sehemu ya mmoja kuweka matarajio dhidi ya mwenzi wake......tamaa ya kupata mali,kupata sifa ndio imekuwa msukumo wa watu kuingia kwenye ndoa...na kwa sababu ya hofu ya kukosa matamanio ama matarajio haya......mwanadamu akabuni sheria mabyo inamuhakikishia kuwa\ anatimiza matamanio yake......na kutengeneza sheria.....ya kwamba kila anayeingia katika ndoa basi huweka kiapo cha lazima(na kuifanya ndoa kuwa shuruti ya kisheria).Swali ni je,upendo (usio na shuruti) unaweza kulindwa kwa shuruti(sheria)?
               Kuingizwa kwa sheria(kiapo_katika ndoa ni dalili tosha ya kuwepo kwa hofu kati ya wawili waliopendana.Ni dalili ya kutoamini mioyo yao .Ni matokeo ya kutazama ndoa katikamisukumo ya hali na mali...gari,fedha,nyumba,ardhi,umaarufu...Matokeo yake ni kwamba mmoja kati yawenzi hawa huwa mtumwa na mwingine huwa mtwana...Hofu ndio msingi wa ndoa ya kisheria.....upendo hushinda yote..Mpendwa msomaji,jiulize ni kwa nini,watu wawili waliokutana wao wawili,wakathaminina na kupendana,huweka kiapo na kuandikishana kisheria.....je kiapo hiki huwasaidia kukua na kupendana pamoja? 
               Hivi majuzi nimesoma ripoti moja kuhusu ndoa duniani,ikionesha kuwa kuvunjika ndoa kumeongezeka sana toka katika karne ya kumi na tisa na sasa kasi ni kubwa sana..Sababu si ugumu wa maisha,sababu si utandawazi...sababu nimekwisha ieleza,ni fikra zetu na msukumo wa kuingia katka ndo kwa msukumo wa mali na hali,kwa matazamio ya kupata kuliko kutoa,sheria ikiwa ndio chimbuko lake
               KWA mtazamo wangu mimi upendo ,ni mvuto asilia...huvumilia,hujali,huthamini..na ndoa iliyojengwa katika upendo,hukua,tena pasipo kiapo kanisani ,msikitini,ama kwa mkuu wa wilaya,kila mmoja huishi kwa furaha ndani ya ndoa hii,kila mmoja huona fahari kuona mwenzi wake akikua nakutimiza ndoto zake....lakini ndoa itokanayo na msukumo wa kisheria...hujengwa katika tamaa,majivuno,hofu,kisasi...na kila mmoja hujitazama yeye anapata nini,mmoja huwa mtumwa na mwingine huwa mfalme.Hawa kinachowaunganisha ni sheria,(hofu) bali waliopendana kwa dhati upendo huwaunganisha.
 sisi twapendana kwa dhati.....kwetu thamani si magari,fedha,ufahari,umaarufu....sisi huvumilia,upendo hushinda yote
          Hivyo ,ni wazi kuwa ili uishi maisha ya furaha katika ndoa, unapaswa kufanya mabo yafuatayo
  1. Kubadili fikra zako,ya kuweka mategemeo ya kupata kitu fulani toka kwa mwenzi wako,kisha anza kutazama kwa mtazamo chanya,jitolee,timiza jukumu lako,daima kumbuka kuwa wewe una jukumu la kumfanya mwenzi wako akue na kutimiza malengo yake maishani,hivyo ni wakati wa kuacha kuomba tu Mungu ambadili mwenzi wako,bali muombe abadili fikra zako.
  2. Ondoa hofu,toa hofu juu ya mwenzi wako kuwa atakusaliti,atakuumiza,..anza kumtazama kwa wema,mfanye aamke na kutambua wajibu wake,hofu hupelekea kujaa wasiwasi na kufanya maamuzi yasiyo na manufaa.
  3. Zipo nyakati mbalimbali katika maisha,kuna wakati wa shida,raha......uvumilivu utokanao na upendo hurejesha matumaini..hivyo jipende wewe,kisha jifunze kumpenda mwenzi wako kama unavyojipenda wewe
  4. Tumezungukwa na jamii yenye maoni tofauti,sikiliza sauti ya moyo wako.....kama unaingia katika mahusiano kwa kusikiliza ushauri ama maoni tu ya wenginme pasipo kuchunguza na kusikia moyo wako,unatengeneza njia ya maangamizi yako mwenyewe,kama utambagua mytu kwa sura,umbo,rangi,kabila ama hali,basi umejibagua mwenyewe toka moyoni mwako
  5.  
       
      unapomsikiliza,kumthamini na kumjali mwenzi wako licha ya mapungufu ya kimaamuzi,hujenga ndoa imara na yenye furaha
     upendo hautazami nini mimi ninapata,bali mwenzangu anafanikiwa vipi kwa uwepo wangu



  Kuna rafiki  yangu alikataliwa kuoa kwa sababu ya kabila lake,akiambiwa kuwa 'mtoto wetu hawezi kuolewa na kakabila hako,labda ungekuwa umesoma sana maana sisi kabila letu ni wasomi,yupo ambaye aliwekewa pingamizi eti kwa sababu ya tofauti ya dini,....waliofanya hivi husukumwa na mali na hali.....upendo haujali dini,kabila wala hali........Kama hatujajitambua,basi migogoro katika ndoa haitakwisha kabisa....tafakari njema
 
     
   
      

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

1 Comments:

  1. Mimi ni hapa ili kushiriki uzoefu wangu na wote wa wewe. Kuhusu jinsi mimi akarudi mume wangu, sisi got ndoa kwa zaidi ya miaka 9 na got watoto wawili. Akaenda vizuri na sisi na sisi ni daima furaha. Hadi siku moja mume wangu alianza kuishi maisha kama hakuweza kuelewa, mimi alikuwa amechanganyikiwa sana kwa njia yeye kutibiwa mimi na watoto. Baadaye mwezi huo huo hakurudi nyumbani na kuniita kuwa alitaka talaka, Mimi aliuliza nini nalikosea stahili hii kutoka kwake, kila kitu alikuwa akisema anataka talaka anachukia mimi na hataki Kuona mimi tena katika maisha yake, nilikuwa mambo na pia kuchanganyikiwa kutokana sijui nini cha kufanya, nilikuwa mgonjwa kwa zaidi ya wiki 2 kutokana na talaka. Nampenda sana kuwa yeye ni kila kitu kwangu bila yeye maisha yangu si kamili. Kumwambia dada yangu kuhusu hali yangu ya sasa na aliniambia kuhusu daktari chamberc, I kuwasiliana naye kwa kurudi kwa mume wangu nyuma yangu, yeye aliniambia kuwa mume wangu imechukuliwa na mwanamke mwingine, ambayo Mke yameandikwa naye nje, hii ndiyo sababu yeye anachukia yangu na anataka sisi kupata talaka. Kisha pia alinipa uhakika kwamba katika saa 48 zijazo mume wangu atarudi kwangu na watoto, baada ya kumaliza akitoa Spell katika saa 48 zijazo mume wangu aliniita msamaha kwangu kwenye simu na kusema yeye bado anapenda mimi sana yeye hajui nini kilichotokea kwake. Lakini leo mume wangu na familia yangu yote ni furaha tena. Asante Dr.chamberc kwa nini alifanya. Ingekuwa kitu leo ​​lakini kwa msaada wako. Wasiliana naye kupitia barua pepe chamberc564@yahoo.com
      (1) wanataka wako wa zamani nyuma.
    (2) Daima kuwa jinamizi.
    (3) Kwa kukuzwa katika ofisi yako
    (4) Je, unataka mtoto.
    (5) Unataka kuwa tajiri.
    (6) ambayo unataka kuweka mume wako / mke kwa ajili yenu peke yake milele.
    (7) haja ya msaada wa kifedha.
    8) Je, unataka kuwa katika udhibiti wa ndoa hiyo
    9) Je, unataka kuwa na kuvutia kwa watu
    10) na ukosefu wa watoto
    11) inahitaji mume / mke
    13) JINSI YA KUPATA bahati nasibu yako
    14) uendelezaji SPELL
    15) SPELL ULINZI
    16) BUSINESS SPELL
    17) GOOD JOB Hechizo
    18) tiba ya ugonjwa wowote.
    (19) E.T.C kesi azimio
    Kuwasiliana nao katika barua pepe yako hekalu chamberc564@yahoo.com na kupata matatizo yako yote kutatuliwa.

    ReplyDelete

maoni yako hapa