Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Friday, August 2

MUNGU KATI YETU

MUNGU KATI YETU


Hekima ipo katika kutambua tofauti iliyopo miongoni mwetu wanadamu.

“Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani,  alitwaa mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.Yakafumbuliwa macho yao,wakamtambua,Kisha akatoweka mbele yao.
Wakaambiana,Je mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?Luka 24:30-32


Nahitaji mwalimu!!
Nahitaji msaidizi!!!
Nahitaji mwombezi!!

"Kama nikipata mwalimu ama yeyote atakayeniongoza,Maisha yangu yatakuwa mazuri!!

Inawezekana haya ni baadhi ya maoni yako ambayo unahisi yanaweza kubadili maisha yako,pasipo kutambua kwamba mwalimu,msaidizi , yupo kati yetu.
Wakati Fulani unaweza kutoka Singida, kukitafuta kitu Dar es salaam, kumbe umekiacha Singida kikipatikana kwa wingi na bure.

Natoa mfano huu kuonesha kwamba zipo nyakati unaweza ukatafuta kitu Fulani na kukifuata mbali,kumbe kinapatikana katika mazingira unayoishi.

Utashangaa nitakaposema kwamba,kuna watu ambao wanakuzunguka na unaishi nao, ambao Mungu amewaweka makusudi katika kuifanya safari yako ya maisha kuwa rahisi,lakini upofu ulio ndani yako,unakufanya usitambue kabisa.

Nyakati zote unawatazama kama ni wa kawaida tu, hawana umuhimu kwako,na hivyo badala ya safari yako ya mafanikio kuwa  ni siku 40, inakuwa  ni miaka 40.

Wapo watu ambao wakati mwingi nawafuatilia.Na huwa najiuliza ni kwa nini sikupata kuwatambua mapema.Matendo yao,mienendo yao, maneno yao, mitazamo yao huweza kuamsha nguvu ndani yangu.

Tabia yangu hii ya kudadisi imenifanya nianze kuwatazama kila nnayekutana nae kwa jicho la kipekee,kwa sababu naamini,kila ninayekutana nae katika kazi,sala,mijadala,daladala,hawajatokea kwa bahati mbaya, bali Mungu ana makusudi.

Mara nyingi nafanya hivi pasipo hata wao kutambua kwamba nathamini kukutana nao.

Mungu yupo miongoni mwetu,na wakati mwingi hatutambui hilo.

Mara nyingi tunadhani Mungu yupo kanisani ama msikitini.

Tukiwaona wachungaji,mapadre na viongozi wa kiimani,tunadhani ndipo tunapoweza kumwona Mungu.

Mungu yupo miongoni mwetu.Kwa wadogo,wadhaifu, warefu,wafupi,weusi,wembamba. Mungu yupo miongoni mwetu.

Binadamu wengi hawapendi kutazama zaidi ya mwonekano wa mtu.Ukijifunza kutazama zaidi ya mwonekano wa nje,unaweza kuona kilicho ndani na thamani ya kisichoonekana kwa macho ya nyama.

Kwa wale wanaoishi na wenzi wenu,Mungu anaweza kuwa ndni ya mwenzi wakounayelala nae kwenye kitanda kimoja.Moyo wa kudhani/kutazama kwa kuhukumu unaweza kukufanya usitambue hilo.

Anaweza kukupa suluhisho juu ya jambo,lakini kwa sababu unamtazama kwa nje, na kwa mazoea basi huwezi ona kilicho ndani yake.

Lakini akisimama kiongozi wa kiimani, akiongea kwa sauti ya kukuvuta, akikupa ushaurinhata usiofaa, utapiga kelele na mwitikio mkubwa moyoni mwako.Ndio baba!!!

Hekima ipo katika uwezo wa kutambua kisichoonekana.

Mungu yupo kati yetu, picha uliyonayo kichwani mwako kuhusu Mungu inakufanya usimtambue.

Kitu unachokifuata maili nyingi,kipo kinakuzunguka katika mazingira yako

Naitwa Pongu Joseph



x

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

1 Comments:

  1. Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

    Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

    Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

    Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

    Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

    Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159

    dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete

maoni yako hapa