Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Tuesday, December 4

IAMBIE NAFSI YAKO

 Tumeumbwa na kupewa mamlaka juu ya maisha yetu na juu ya kila kilicho juu ya nchi,Hivyo tunapaswa kukumbuka kuwa kila kitu tunachokihitaji maishani mwetu kipo katika uwezo wetu tuliopewa na Muumba...mradi tu ulihitaji jambo hilo kwa dhati kabisa toka moyoni mwako....
Kwa kutambua hilo huna sababu ya kuwa na wasiwasi juu ya maisha na juu ya kesho....iambie nafsi yako kwa dhati kabisa toka moyoni yakuwa Unaweza.
Unaweza kuwa imara kuliko hofu uliyonayo,
Unaweza kabisa kuwa na afya bora,furaha na amani,
Unaweza pia kuwa sababu ya vyote hivyo kwa wengine,
Unaweza kuwafanya wengine watambue kuwa wao ni nuru,nao wanapaswa kuifanya nuru hiyo iangaze wengine
Kuafanya wayatazame maisha katika upande wa mwangaza

Iambie nafsi yako kuwa,
Unaweza kubadili maisha yako na kuyafanya kuwa nuru,
Unaweza kufikiri chanya na kutenda kwa uwezo wako wote
Kuwa chachu ya mabadiliko chanya duniani,na kuwa mfano wa kuigwa

Iambie nafsi yako yakuwa unaweza kusahau yaliyopita,
ambayo yalikusababishia maumivu,na kuishi maisha yenye furaha na matumaini,ukianza upya bila woga,
Unaweza kuwapenda na kuwajali wengine pasipo kutazama maumivu ama mabaya waliyokutendea
Unaweza kusimama imara hata katika nyakati za magumu mengi
        furaha ni pale unapotumia maisha yako kuwa furaha kwa wengine-unaweza kuwa chachu ya upendo na anani


Sema kwa nafsi yako kuwa unaweza
Kuishi bila kusengenya na kuwanenea wengine kwa ubaya,bali unaweza kuwa faraja kwa watu wote,
Iambie nafsi yako kuwa wewe ,ukiwa kama nafsi huru,
Una jukumu la kutenda hapa duniani,
Iambie nafsi yako itazame kwa kina,
Ichunguze umuhimu wa maisha yako hapa duniani
Na kisha kuamua kufanya dunia kuwa sehemu ya upendo

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 Comments:

Post a Comment

maoni yako hapa