Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Monday, December 31

UKWELI KUHUSU WEWE

Wewe ndiye mjenzi na mbomoaji wa maisha yako katika nyanja zote kwa fikra zako kwani fikra ndiyo mbegu ndani yako itoayo matokeo kadiri ya sababisho litokanalo na msukumo wa kimazingira. Hivyo mafanikio yako huja kwa kupanda fikra za mafanikio na kutofanikiwa huja kwa kupanda fikra za kushindwa,uma kwa kujua na kutojua.

Wewe ni msanifu na mjenzi wa maisha yako(picha na cognitivesocialweb.com)




Wewe ndiye unayebomoa na kuangamiza maisha yako kwa fikra zako,kwa kujua ama pasipo kutambua(picha na hot100tips.com)

Kamwe huwezi kufanikiwa kama hujui unachokitaka,huwezi kuona mbele pasipoonekana kama hufahamu uendapo,ni mpaka pale utakapojua unataka kuwa nani,ndipo utakapokuwa.....ni sawa na kwenda safari isiyojulikana hata uelekeo.

Mungu alipokuuumba alikupa nguvu na uwezo,akaifanya dunia na vyote vinavyokuzunguka vitii maagizo yako,hasa yale yanayotokana na msukumo wa moyo wako..hivyo wewe ni kiumbe bora jinsi ulivyoumbwa,wewe ni aidi ya ulivyo,wewe ni upendo,amani,faraja,chuki,visasi,wewe ni mwerevu,na msanifu wa maisha yako mwenyewe,hivyo hupaswi kumlaumu yeyote kuhusiana na jambo lolote linalohusu maisha yako,chukua hatua juu ya maisha yako mwenyewe.

Ndani yako ni chemchemi ya kila hali iletayo matokeo hasi ama chanya,ukifikiri kuhusu upendo utafute ndani yako,ukitaka kujua kuhusu uwezo ulio nao,utafute ndani yako,ukitaka kujua kuhusu mafanikio yako,tafuta ndani mwako...chemchemi yako haileti faida kama hujachukua maamuzi

Huna tofauti na binadamu mwingine kwa maana ya uwezo......anza kwanza kuuchunguza ubora wako uujue,ukiutambua,utambue kuwa wengine ni bora kama wewe,hivyo matendo yako yazingatie matokeo yake,fikra zako ziwe fikra njema juu yako na kwa wengine kwani kila utendalo kwa wengine,umejitendea mwenyewe.Maisha ni uchaguzi wako,na matokeo ya kila unachochagua ni juu yako.

Fikra zitokazo kwako ni sewa na bustani ama shamba,inaitaji kutazamwa na kupaliliwa...kuhakikisha kuwa unapanda mbegu bora,ukipanda mbegu isiyo bora (fikra mbaya dhidi yako na maisha yako) huleta matokeo sawia na mbegu uliyoipanda.

Maisha unayoyaishi hayatokei kwa kiitwacho bahati(nzuri ama mbaya) bali ni matokeo ya uchaguzi wako mwenyewe ama kwa kutambua na kutotambua.Umasikini,utajiri,furaha,huzuni,amani,chuki,upendo vyote ni matokeo ya uchaguzi wa maisha yako.Nguvu na uwezo wa kubadili matokeo hayo hutoka ndani mwako....Ni msukumo utokao ndani mwako pekee ndio utakaobadili maisha yako.

Kamwe wewe huvuti maishani vile vitu unavyovitamani ama maisha unayoyatamani,bali unavuta jinsi ya fikra zako.Fikra a ushindi huleta ushindi,fikra za kushindwa huleta kushindwa.

Mara nyingi unajaribu kubadili hali ama mazingira yanayokuzunguka pasipo kubadili fikra zako juu ya mambo hayo....Jinsi uvitazamavyo vitu huwa...ukilitazama jambo kwa uchanya wake,basi kila hali huwa ni nafasi,kama ni mtazamo hasi,basi matokeo yake huwa hasi na kwako huwa ni maumivu.

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com