Rafiki
wa kweli ni yule ambaye unaweza kumwamini,ni yule ambaye unaweza
kumshirikisha furaha,huzuni na kila tamanio la moyo wako,ni yule ambaye
hakuhukumu kwa kufikiri tu,ama kusikia toka kwa wengine,ni yule
anayekubali na kuheshimu maamuzi yako,uchaguzi wako na uhuru wako,ni
yule ambaye yupo tayari kutumia alichonacho kwa ajili yako,ni yule
anayeweza kukukosoa na kukufanya utambue njia bora na kukua ukiendelea
mbele daima,hutambua umuhimu wako na kukupa moyo,kukuamsha uwe bora
zaidi na kufikia mafanikio,Hukusikiliza na kukushauri pale panapostahili
na unapohitaji...daima huwa kwa ajili yako..rafiki wa kweli hawezi kuwa
na ajenda za siri,hawezi kukuzunguka n A KUKUSALITI...rafiki wa kweli
hufurahi pale unapofanikiwa na si kuweka kinyongo na kuumia pale
unapofanikiwa,daima huwa pamoja nawe......na ni furaha kubwa pale
unapogundua kuwa rafiki yako mkuu ni wewe mwenyewe....furaha pia ni
kumpata rafiki wa kweli ..ni wachache....daima nafurahi kupata marafiki ambao wanathamini uwepo wangu,ambao hufurahi wakiona nasonga mbele.Ambao wako tayari kujitolea kwa ajili ya wengine,hasa kupitia blog hii .nitakuwa sina fadhila kama sitasema ahsante itokayo katika
furaha ya moyo wangu
Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
Related Posts:
MY WISDOM
WAY TO SUCCESS
0 Comments:
Post a Comment
maoni yako hapa