Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Monday, February 4

RAFIKI WA KWELI

Rafiki wa kweli ni yule ambaye unaweza kumwamini,ni yule ambaye unaweza kumshirikisha furaha,huzuni na kila tamanio la moyo wako,ni yule ambaye hakuhukumu kwa kufikiri tu,ama kusikia toka kwa wengine,ni yule anayekubali na kuheshimu maamuzi yako,uchaguzi wako na uhuru wako,ni yule ambaye yupo tayari kutumia alichonacho kwa ajili yako,ni yule anayeweza kukukosoa na kukufanya utambue njia bora na kukua ukiendelea mbele daima,hutambua umuhimu wako na kukupa moyo,kukuamsha uwe bora zaidi na kufikia mafanikio,Hukusikiliza na kukushauri pale panapostahili na unapohitaji...daima huwa kwa ajili yako..rafiki wa kweli hawezi kuwa na ajenda za siri,hawezi kukuzunguka n A KUKUSALITI...rafiki wa kweli hufurahi pale unapofanikiwa na si kuweka kinyongo na kuumia pale unapofanikiwa,daima huwa pamoja nawe......na ni furaha kubwa pale unapogundua kuwa rafiki yako mkuu ni wewe mwenyewe....furaha pia ni kumpata rafiki wa kweli ..ni wachache....daima nafurahi kupata marafiki ambao wanathamini uwepo wangu,ambao hufurahi wakiona nasonga mbele.Ambao wako tayari kujitolea kwa ajili ya wengine,hasa kupitia blog hii .nitakuwa sina fadhila kama sitasema ahsante itokayo katika furaha ya moyo wangu

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 Comments:

Post a Comment

maoni yako hapa