Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Monday, February 18

WANAWAKE AMKENI


MWANAMKE-FURAHA ITOKAYO MOYONI-CHIMBUKO LA UPENDO
                                 
Ni miaka mingi imepita toka palipoingia mfumo wa kundamizi kwa  wanawake.Mfumo huu umemfanya mwanamke kudharaulika ,matokeo yake wanawake wenyewe wamekubaliana na mfumo huo bila kutambua.Nilipata kueleza jinsi mazingira tunayoyaishi yanavyoweza kupelekea kubadili fikra za mtu,hasa pale akiwa hatambui kuwa yeye ndiye anayepaswa kuyatawala mazingira.Wanawake wamekumbwa na mfumo huo.Mtu binafsi anapoukubali mfumo Fulani,huuona ni wa kawaida na hata kuuishi na kuusifia,asijue athari zake katika ujenzi wa maisha yake.

Mfumo huu kandamizi,umeonekana kuwa ni usahihi.Dini pia zimeingia katika kuuchagiza mfumo huu.Mara kadhaa zikifundisha ama kuwajengea waamini wake fikra kuwa  kuwa mwanaume yupo juu ya mwanamke.Wanaume wanaamini kuwa kuwa  na nguvu ni kumtawala mwingine badala ya kuyatawala mazingira na hivyo maisha ,wanafikiri kuwatawala wanawake.Wanaume wamekuwa wakijisifia kwa kuzaliwa jinsia ya kiume.Wamekuwa wakitoa maneno ya kejeli na dhalili dhidi ya jinsia ya pili(mwanamke).Mfumo huu ukakua na ndipo jinsia ya kike ilipoanza kutazamwa kuwa si bora.Ukweli ni kwamba hakuna jinsia iliyo bora kuliko nyingine.Kila jinsia ni bora jinsi ilivyo pasipo  kusahau kuwa  kila jambo huwa lina upekee wake.

Miaka ya hivi karibuni umeingia mfumo wa utandawazi.Mfumo ambao mifumo ya ,mawazo,uchumi,utamaduni inalengwa kufanywa kuwa sawia.Ni mfumo shindani ambao wanaoweza kuyatawala mazingira yao,wanafaidika kuliko wale wasiojitambua.Mfumo huu umewaathiri pia wanawake.Tumeshihudia wanawake wakivaa mavazi yanayoonesha sehemu zao nyeti,wakicheza picha za ngono na kudhalilishwa.Wanawake wanaonekana kuwa ni chombo cha starehe na dhalili.Kwenu ninyi wanawake,mnapaswa kuchukua hatua,kujitazama upya,mnawaza nini kila mmoja dhidi yenu wenyewe? Je mpo tayari kutumika kama msio na thamani kwenye matangazo,sinema na kwenye mawazo ya wanadamu wote? Je mpo tayari kujenga dunia duni yenye dhiki,chuki na isiyo na uelekeo?Mpo tayari kuendelea kutazamwa kuwa hamuwezi?

Leo ningependa wanawake waamke na kuvumbua siri kubwa ndani mwao.Hakuna wa kuchukua hatua ni ninyi wanawake,kila mmoja kwa nafsi yake. Ninyi ni wa thamani.Ni zaidi ya sura zenu,zaidi ya maumbile yenu.Ni zaidi ya mavazi mnayovaa.Uzuri wa mwanamke ni nuru iliyopo ndani mwake inayoangaza dunia kwa upendo.Ni nuru anayosubiria itumike kuimulika dunia,kuifanya kuwa sehemu bora ya kuishi. 

Ni nuru hiyo iliyo ndani mwenu ambayo ikiruhusiwa kutolewa huzaa upendo,amani,usawa,haki na chemchem zote za upendo.Anayetambua ni yule aliye tayari kuchimba ndani mwake na kugundua kuwa kama mwanamke, anaijenga na kuibomoa dunia kadiri ya matumizi ya uwezo aliopewa.Uwezo wenu upo ndani yenu.uzuri wenu upo ndani mwenu na si kwenye mavazi na maumbile tu.Uzuri huo ulio ndani mwenu,unapotumika hutoa matokea yanayotoa picha ya uzuri wenu,yaani Upendo.Kichwani mwenu na moyoni mwenu mmebeba hazina kubwa.Ninyi ni bora,zaidi ya mwili unaoonekana,zaidi ya idadi ya namba,idadi ya nyota..
                             

Wanawake ni viumbe muhimu katika dunia hii.Ndio wazazi wa kila jambo katika dunia hii.  Ni chumbuko la wema na upendo hapa duniani.Kupitia mwanamke binadamu wanazaliwa.Wakombozi wa fikra,wapigania haki,wahimiza upendo,wapigania amani wote wametoka kwa mwanamke.

Mungu alimuumba mwanamke na kumuwekea uzuri wa kila namna ndani mwake,ali kila apitiaye tumboni mwa mwanamke aubebe uzuri huo na kuuishi  hapa duniani.Katika kipindi chote aishipo akikua tumboni mwa mwanamke,kiumbe anayetarajiwa kuzaliwa  hubewa chemchem ya kila kitokacho kwa mama.Hivyo mwanamke anahusika katika kuijenga dunia iliyo bora.Ule usemi wa kuwa ukimuelimisha mwanamke,umeielimisha jamii,ni sahihi..kinyume chake pia ni sahihi.

Dunia tuliyonayo sasa,mwonekano wake,matukio na kila tukipatacho,ni matokeo ya usanifu wetu wenyewe.Ni matokeo ya mwanamke na mwanamume,mwanamke akihusika kwa kiasi kikubwa.Chuki zilizopo,matabaka yaliyopo,visasi,mauaji ni matokeo ambayo yameanza katika dunia isiyoonekana iliyopo ndani mwetu,na kisha tumeijenga katika mwonekano uliopo.

Ukandamizaji wa wanawake ,na udhalilishaji unatoa matokeo ya jamii kandamizi na dhalili.
Wanawake mnayo nafasi ya kujenga dunia mpya.Inayoanza ndani mwenu.Ubikira wenu (ukamilifu ndani mwenu) utumike kuimulika dunia,kuwa sehemu bora.Mwanamke akiutambua ubikira ndani mwake,maajabu makubwa ya mabadiliko ya maisha yake huanza,Maisha mapya,bora hutokea.Wanawake amkeni.
Kila mmoja wenu akiamka,mtaamsha dunia mpya.Tuanze kuwafunza watoto wetu juu ya thamani yao.Waanze kuthamini hazina walio nayo ndani mwao.Washeni mishumaa iliyo ndani mwenu,iimulike dunia kwa upendo.Mulikeni muondoe mtazamo mbaya wa jamii juu ya mwanamke.Jukumu ni lenu.Nguvu mlionayo haijapotea,kinachohitajika ni kuiamsha.Licha ya magumu mtafika.

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 Comments:

Post a Comment

maoni yako hapa