Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Monday, January 7

WAKATI NI SASA


Ulishawahi kujiuliza ni lini unasubiri ,ama ni lini umeamua kuanza kutimiza yale ambayo umepangilia kuyafanya maishani?Umewahi pia kujiuliza  ni lini malengo yako yatatimia?
Kama unatambua kuna sababu ya wewe kuishi hapa duniani,unasubiri nini kutenda kadiri moyo wako unavyokutuma?Unasubiri kesho,kesho kutwa,mwisho wa mwezi ,ukihitimu masomo,ama unasubiri umri wako ufike miaka kadhaa?
Ipo siku hutakuwa na uwezo wa kutenda chochote,hutakuwa na nafasi ya kutenda kile ulichokuwa kutimiza,na wakati huo ndipo utakapokuwa na majuto ni kwa nini hukutenda pale ulipoweza.
Hakuna muda mwingine zaidi ya sasa.Matokeo ya mambo yote yajayo hufanywa na maamuzi ya wakati uliopo.AMUA sasa.Amua kuanza kuishi maisha uliyoyakusudia sasa.
Utatambua kila kitu juu ya maisha yako ukianza kuchimba ndani yako sasa.Anza kusikiliza sauti iliyopo ndani mwako sasa.Usisubiri mwisho,fanya kwa bidii sasa.Badili maisha yako na ndoto zako zote kuwa halisi sasa.Usisubiri hatari ya kusubiri kesho,baadae….Mavuno ya baadae ni matokeo ya kupanda sasa

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com