Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Saturday, January 5

ATHARI ZA MSUKUMO WA WANAOKUZUNGUKA

Watu wanaotuzunguka hutusukuma kufikiri na kutenda kadiri ya kanuni  na imani zao na kutufanya kuwa watumwa wa fikra za kimitazamo(picha na www.nlm.nih.gov)

Nilikwisha kujadili ni namna gani mafanikio ya mtu yanaanza ndani mwako,   soma zaidi hapa
Katika makala hiyo,tunajifunza kuwa kila jambo huanza na wewe.Chochote kinachoanza na msukumo utokao ndani yako,ndilo linaloleta mafanikio.Kwa kifupi tu mafanikio ya mtu yanaanza na yeye mwenywe na si msukumo utokao nje yake yeye.

Leo tutajadili jinsi msukumo wa nje (toka kwa marafiki,ndugu na wote wanaokuzunguka unavyowezakuathiri upekee wako na maamuzi.

Tumejifunzapia kuwa kila mmoja ni wa kipekee kwa maana ya nafsi yake na atasimami katika maamuzi yake na ujenzi wa maisha yake.Lakini tunaishi katika jamii ambayo inatutia msukumo wa kuamua na kutenda kadiri ya mawazo na kawaida yao.
Kabla hujazaliwa walikwepo waliotutanguli,kwa maana ya babu zetu na wengine wengi waliopita.Hawa walitengeneza mfumo yao ya maisha  ambayo tunaweza kuuita mfumo wa jamii,ambao ulijenga matarajio mengi ya watu mmojammoja  na jamii nzima.Mfumo huu ni pamoja na kanuni,mila ,desturi,imani,dini,serikali,sherehe.Mfumo huu umejengwa na sheria na kanuni nyingi ambazo unapozaliwa tu,unakuwa umefungwa moja kwa moja na mfumo huo pasipo kupenda ukiamini ndio mfumo sahihi.Sheria na kanuni zilizopo katika mfumo huu ulioukuta zinapokuwa kawaida kwako,zinaufanya mfumo wako wa tafakari uwe na uelekeo na fikra zilizo ndani ya mfumo huo.
Fikra zenye mipaka huleta matokeo yasiyo huru (picha kwa hisani ya www.rfidgeneral.com)


Mfumo huu unakulazimu kujifunza na kufuata mengi kama ni nini unapaswa kufuata,kuamini,ni nini kinakubalika na nini hakikubaliki,kipi ni chema na kipi ni kibaya.MFUMO HUU WOTE UNAKUPELEKA KUFUATILIA KILA JAMBO KADIRI YA TARATIBU NA MAWAZO YA MFUMO.Maka unapokuwa unakuwa na fikra za kimfumo kuwa jambo fulani lipo hivi tu,na hivyo mara nyingi hujenga mpaka wa kufikiri na kuamua.Unakuwa huwezi kufanya jambo mpaka usikilize waanaokuzunguka wanasemaje.
Natoa mfano wa mjomba wanguambaye pale alipotakakuoa binti ambaye walikubaliana na kupendana,alibadilisha uamuzio baada ya kuambiwa tu eti dini anayoiamini binti huyo si nzuri.Hapo dini ikawa juu ya upendo.
Pia kuna rafiki yangu mmoja alikuwa akijadili na marafiki juu ya imani ya dini nyingine,akashawishiwa kuifuata imani mpya,akakiri kuridhika na imani hiyo lakini hofu yake ikwa je,wazazi watanionaje?,licha ya kuwa yeye ni mkubwa kiumri.

Hii ni baadhi tu ya mifano.Mwisho kbisa tunaanza kuitazama  dunia kama sehemu ya ushindani.Tunajifunza uchoyo,ubinafsi,usiri na visasi kwa sababu ya mfumo licha ya kuwa yapo mengi mazuri.

Ushindani huo unatufanye tufikiri na kutenda kwa kuangalia mitazamo ya jamii.Unakuwa huna fikra za kutafakari jambo nje ya mipaka ya jamii.HIVYO unakuwa si huru katika maamuzi juu ya maisha yako mwenyewe.Kwa kifupi unakuwa mtumwa wa mfumo huu wa jamii.,ukifikiri na kutenda katika uwanja wa fikra za jamii.Ukweli ni kwamba usipotoka katika mpaka huu na kuuvuka,kuwa huru,hutaishi kamwe maisha yako halisi.
Maisha yetu ni matokeo ya fikrazetu (picha kwa hisani ya mtandao)


Ninachotaka kukisema hapa ni kuwa ukitaka kuishi maisha unayoyachagua wewe ,na kufikia mafanikio ni lazima uchukue uamuzi wa kufikiri nje ya mipaka ya mawazo ya jamii.Ni lazima uvunje mipaka ya mazoea na ile ya sheria na kanuni za imani ya jamii.Ni lazima ujifunze kuwa huru.Naomba nieleweke vizuri hapa si kwamba nahamasisha watu wavunje sheria za nchi ama mahalia,laaah,kuvunja mazoea ni kufikiri kwa mapana bila kufungwa na mawazo yanayoaminika tu na jamii.


Imani ya jamii ina nguvu sana,na hujenga upotofu ya kuwa tunapaswa kufikiri hivi na si vile,fulani yupo hivi na vile na inamsukuma mtu kutenda kadiri ya fikra za jamii husika.Tunalazimika kuishi maisha ya bandia ili tuonekane kwa wengine(Amini nakwambia utakuwa mtumwa katika mawazo mpaka pale utakapopanua wigo /uwanja wako wa fikra).

Unakuta jamii inaamini juu ya ushirikina na uchawi katika kutafuta mafanikio,hivyo kunakuwa na imani kuwa huwezi kufanikiwa mpaka uende kwa mganga.Watoto wakiugua magonjwa mabayo ni matokeo ya maisha anayoishi basdi inaaminika amechezewa(amelogwa).Tukumbuke kuwa mtu hawezi kukutendea ubaya  kama wewe si kisababishi cha fikra za mtu huyo kukufanyia ubaya.Nakumbuka kuna rafiki yangu ambaye nilisoma pamoja nae,alikuwa namsukumo sana kwa wengine,akiwaaminisha kuwa ili uwe bora na rafiki yake ni lazima uwe unakunywa pombe ama kuzisifia.Hii yote ni matokeo ya imani na fikra za kimfumo.

Hivyo tukumbuke kuwa kama tunaishi tukifikiri na kutenda kwa mipaka ya imani za wengine,basi sisi ni watumwa wa imani hizo mpaka pale tutakapotoka nje ya mipaka hiyo katika kufikiri na kutenda.Tunatafuta kukubaliwa na mawazo na mitazamo ya vikundi fulani.Tukumbuke kuwa picha halisi juu ya kinyago huwa sahihi kwa mchongaji,ambaye anachonga akiwa na picha yake katika fikra kuwa nataka awe hivi.Ukiwauliza wateja wanaonunua kinyago,kila mmoja atatafsiri kadiri ya fikra zake pia.
Mabadiliko katika fikra na maendeleo yako yanaanza pale unapoanza kufikiri nje ya mipaka ya wengine(picha kwa hisani ya mtandao)


Kwa nini uishi kwa mawazo ya wengine?Kwa nini uumie unapoambiwa una sura mbaya wakati hayo ni maoni ya msemaji tu.Ukitaka kupata majibu juu ya maisha yako,chimba ndani yako..Tafuta ndani yako.Ninaamini kila jambo huanza na wewe(mimi),Utajiri na mafanikio yote yanatoka ndani mwa muhusika.Zawadi kubwa juu ya maisha yako ni kuithamini nafsi yako  na kuisikiliza sauti kubwa itokayo moyoni mwako,ikuongozae juu ya kutenda,hii ni sauti ya Mungu iletayo mafanikio,furaha na kila lililo jema.Sauti hii inakupa nguvu ya kutenda miujiza kila wakati,ndiyo inayofanya nuru ya maisha yako ing'ae.

Jamii inakufanya ulazimike kuenenda kimawazo na fikra kadiri ya imani yake.Kwa nini usikuballi jinsi ulivyo na kuanza kuchimbandani yako palipo na siri kuu ya maisha yako?Mimi binafsi natambua jinsi ninavoonekana.Najikubali kwa kuwa mimi ni zaidi ya nilivyo.Ukiachilia mbali mazingira ninayoishi na sura yangu,mimi ni wa thamani,kama wengine.Wewe ni wa thamani jinsi ulivyo,na thamani yako ni sawa na binadamu wote.Unao uwezo wa kuwa na kuishi maisha ya furaha na mafanikio.Unastahili,wewe ni Matokeo ya kazi kubwa ya Mungu. 



Sasa anza kujikubali na kuepuka misukumo ya wale wanaokuzunguka.Anza kutazama uwezo ulio nao,tazama chemchem ya mafanikio iliyopo ndani mwako.Sisi sote ni bora .Sisi wote ni wamoja.
Huu ni wakati wa kujifunza kuwa wewe,kujikubali,kukua na kubadilika.Anzakujitambua wewe kisha utatambulika kwa wengine.Hongera kwa kujitambua

Ahsante. Joseph Pongu-0717903089,0765046644.Karibu tujadiliane na kuinuana.

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com