Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Wednesday, August 14

Nafsi huru

Kuna nyakati maishani mwetu ambapo vitu na watu walio karibu nasi watatutoka na kuwa mbali nasi, hii inatokea ili kutukumbusha kuwa tumetumwa kila mmoja kama nafsi huru yenye kazi maalum .Kila nafsi ni rafiki wa kweli wa nafsi yake . Inatukumbusha kuwa tusiishi maisha ya wengine bali kila nafsi ijenge maisha yake iliyoitiwa.Maisha na matukio yatutokeayo yanatukumbusha kutazama ndani mwetu palipo na nuru na sauti ya Muumba.Tunakumbushwa kurudi ndani yetu kila wakati tunaposukumwa na vitu vinavyotusahaulisha sababu ya kuwepo duniani.Yapo mengi yanayotugawa, kutupoteza na kutusahaulisha kuwa ss ni malaika tuliobeba miili kuiangaza nuru duniani kote.
Kila nafsi ipo sehemu muafaka kwa wakati na nafasi muafaka.
3Pia kila nafsi hutoka sehemu kwa wakati muafaka ili kuipa nafasi nafsi nyingine nafasi muafaka.
Nafsi isiyotumia nafasi ni nafsi isiyotambua sababu ya kuwepo-Katika ulimwengu halisi hakuna kufa,bali kubadilika kwa nafasi na kazi mpya.Nafsi itendayo jukumu lake huishi milele .Zikutanapo nafsi zitendazo wajibu huunda umoja uundwao kutoka ndani ya kila nafsi.Ni muungano takatifu ambapo dunia mpya huundwa na kisha matokeo yake kuonekana katika ulimwengu unaoonekana.Je wewe ni mmoja wa umoja huo?.Ishi maisha yako halisi.

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 Comments:

Post a Comment

maoni yako hapa