Unapoanza
kumuona Mungu katika kila kiumbe kinachokuzunguka unatambua kuwa sasa
umezaliwa upya.Sauti yake inakuwa ikiongea nawe ndani mwako toka ndani
yako.Unatambua kuwa Mungu hayupo mbali nawe bali yupo ndani mwako wakati
wote.
Unaruhusu nguvu na chemchem ya kila ushindi kufanya kazi ndani
yako na kukupa nafasi ya kugundua nguvu hii iliyo ndani mwako na
kuitumia kuifanya dunia kuwa sehemu bora kwa
viumbe wote.
Mungu ametupatia uwezo mkubwa wa kuyafanya maisha yetu kuwa
yenye faida kwa wengine,na husubiri maamuzi yetu ili kutuonesha
njia.
Tunapokuwa tayari anatufundisha maana ya kuwa hapa na thamani ya
maisha yetu . Ndipo unapomjua tena si kama kiumbe cha kutisha ama
kisichoonekana lakini kama sehemu muhimu ndani mwako.Kisichoonekana
ndani mwetu kinazaliwa upya na kuonekana kwa kila anayekuzunguka.
Kisha
hutupatia kila uwezo na kuingia ndani ya kila kilicho mwilini mwetu kwa
maelfu,tayari kwa kumtumikia kwa njia mbalimbali.Unitambua kuwa maisha yako ni ya thamani kwako
na kwa wengine,unafungua ndani ya moyo wako kuishi kwa dhati.Sauti
ndani mwako inaanza kusikika kwa viumbe wengine.Unapata thamani zaidi
kupita vito vya thamani na zaidi ya fedha.
Maisha yako yanakuwa mwanga kwa
viumbe wote.Unaanza kutumia kila kipawa na nafasi unayopewa na Muumba
kwa ajili ya wote kwa utukufu wake yeye.Maisha yako yanaongea — Tunajenga dunia mpya
yenye matumaini na furaha-Jumapili njema
KARIBU SANA
HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH
Sunday, August 25
UJUMBE WA JUMAPILI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Comments:
Post a Comment
maoni yako hapa