Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Sunday, August 5

KILA JAMBO LITOKEALO LINA SABABU, KILA JAMBO HUTUFUNZA

     Ni  kweli kwamba kila changamoto itupatayo huwa na sababu...na huwa ni wakati wetu kujifunza mbinu mpya za kufikia pale tunapohitaji kufika...wakati mwingine tunajifunza kutoshikilia sana mambo ambayo yanatuchelewesha kufika tuendako....wakati mwingine tunakumbushwa kuwa kila mlango mmoja ufungwapo,basi hutoa nafasi kwa milango mingine mingi na madirisha kufunguliwa ,na hivyo,waweza kukata tamaa,kwa kutokewa na changamoto,kumbe changamoto hiyo ndiyo inayokupa njia mpya
    Si lengo langu kuandika mambo yanayonihusu mimi,ama watu fulani...kama ilivyo ada,blog hii ni mahali pa kukufanya ujitambue wewe ni nani,uweze kufungua minyororo ambayo inakuzuia kuyafikia mafanikio
    Wikiendi nilikutana na rafiki yangu ambaye ameumizwa sana katika masuala ya mahusiano...kuumizwa huko kumemfanya ajihisi kuwa hana thamani,ana matatizo.....hajiamini tena na daima anashuka moyo,amekata tamaa na kuapa kuwa hatapenda tena...baada ya kuongea naye sana,alitokea kukubali kuwa hayo yalitokea,yamebaki historia.....anasimama tena na kusamehe,akianza maisha mapya.Amekubali kuwa aliumizwa,lakini yote hayo hayatamfanya ashindwe kuishi maisha mapya,amaetambua kuwa yeye ana jukumu juu ya maisha yake,hakuna anayeweza kumpangia maisha yake yajayo,bali ni yeye,yaliyopita yamempa nguvu ya kusimama na kukimbia kwa kasi zaidi





  CHANGAMOTO ZINATUKUMBUSHA KUWA NI VEMA KUTAZAMA KILA JAMBO  KUWA NI KUFUNZI
    Lipo somo kubwa tunajifunza hapa......nakusihi usome kwa makini maneno haya chini,ambayo rafiki yangu huyo,aliyaandika baada ya kujitambua,toa pia maoni


Kuachana nawe kumenifunza jinsi ya kuwathamini watu wengine,kuwapenda hata pale panapoonekana ni vigumu, kumenifanya nijifunze kuwa mimi sipo tu kwa ajili yang u,bali kwa ajili ya wengi,hivyo,maisha yangu yana sababu kubwa hapa duniani,nimejifunza kuwajibika na kujitolea kwa wale wote ambao jamii haiwathamini—wafungwa,yatima,wajane na wote ambao hawana tumaini la kusimama tena,nimetambua kuwa sisi sote ni wamoja,uadui huletwa na wale wasiojitambua,wanaofikiri kuwa dunia
hii ni sehemu ya ushindani badala ya ushirikiano,wanaodhani kuwa wao ni bora kuliko wengine...nimejifunza kuwa ni furaha katika kutoa kuliko kupokea,nimejifunza kuwa hata kama binadamu atakuwa amekosa viungo vya mwili,sura nzuri,mavazi,fedha ama umaarufu,lakini bado ni binadamu mwenye thamani kubwa,kwani thamani ya binadamu ni zaidi ya sura,umbo,mali,umaarufu,hivyo nitawatazama binadamu wote kwa usawa na kujitolea kwao kwa usawa,nimejifunza kuwa sipaswi kutazama changamoto kwa upande hasi,bali nitazame daima kwa mtazamo chanya,na mwisho,nimejifunza kusimama mwenyewe,na kumshukuru Mungu,nikimsihi anitumie daima kwa ajili ya  w engine…Amina (Pongu)

  

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 Comments:

Post a Comment

maoni yako hapa