Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Tuesday, August 7

MWALIMU BORA

Wale waliopitia ugumu ,milima na mabonde katika maisha yao ni walimu bora,kwa sababu wanajua maana ya kila jambo walilolipitia,wanajua jinsi gani ya kubomoa ukuta wa mipaka ya kufikiri,wanajua kuumizwa,wanajua faraja,wanajua chuki,wanajua amani,wanajua upendo,wanajua kila jambo walilolipitioa si kwa kusoma nukuu tu,bali kwa kuishi na kupambana na vikwazo...wanatambua kuwa hakuna njia ya kupambana na woga zaidi ya kuamua kutenda unachokiogopa,wanatambua jinsi ya kufungua minyororo inayotuzuia kuyafikia mafanikio,hawa maisha yamewapa changamoto,maisha pia yamewapatia baraka tele...wamepata majaribu,wakayapita,wamepata maumivu,wakaendelea kusimama imara ,watu waliwakejeli,waliwaumiza na wengine waliwapa faraja...waliamua kuacha yaliyopita na kusimama tena kwa ushindi,wakachagua kuwa washindi,wakaishi maisha yao kwa ajili ya wengine pia,woga wao ni kuogopa kutenda wanapotakiwa kutenda..wamekuwa mifano bora katika jamii,wanatambua kujitolea ,hawa ni mashujaa ambao nuru ya maisha yao itaishi milele.Ni wakati sasa wa sisis kutoogopa kushindwa na kuamua kudiriki kutenda.

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com