Wale
waliopitia ugumu ,milima na mabonde katika maisha yao ni walimu
bora,kwa sababu wanajua maana ya kila jambo walilolipitia,wanajua jinsi
gani ya kubomoa ukuta wa mipaka ya kufikiri,wanajua kuumizwa,wanajua
faraja,wanajua chuki,wanajua amani,wanajua upendo,wanajua kila jambo
walilolipitioa si kwa kusoma nukuu tu,bali kwa kuishi na kupambana na
vikwazo...wanatambua kuwa hakuna njia ya kupambana na woga zaidi ya
kuamua kutenda unachokiogopa,wanatambua jinsi ya kufungua minyororo
inayotuzuia kuyafikia mafanikio,hawa maisha yamewapa changamoto,maisha
pia yamewapatia baraka tele...wamepata majaribu,wakayapita,wamepata
maumivu,wakaendelea kusimama imara ,watu waliwakejeli,waliwaumiza na
wengine waliwapa faraja...waliamua kuacha yaliyopita na kusimama tena
kwa ushindi,wakachagua kuwa washindi,wakaishi maisha yao kwa ajili ya
wengine pia,woga wao ni kuogopa kutenda wanapotakiwa kutenda..wamekuwa
mifano bora katika jamii,wanatambua kujitolea ,hawa ni mashujaa ambao
nuru ya maisha yao itaishi milele.Ni wakati sasa wa sisis kutoogopa
kushindwa na kuamua kudiriki kutenda.
Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
Related Posts:
MY WISDOM
UPLIFT YOURSELF