Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Monday, August 27

NAFASI YAKO HAPA DUNIANI NI YA MUHIMU SANA

Kwa sababu kila mmoja wetu anahitaji kuthaminiwa,kuheshimiwa na kila mmoja anahitaji kuona wengine wanamjali....mioyo yetu haiwezi kuwa na furaha ya kweli kama hatutakuwa sauti kwa wale ambao wanataka kusema lkn hawapati japo nafasi....kuwa faraja kwa wale wenye machozi,kuwa mwangaza kwa wale wanaohitaji nuru ya kuamsha mioyo yao na ari ya kuyaishi maisha yao....tutakapokuwa nguvu kwa wanyonge,na zaidi..kuishi kwa ajili ya wengine

Haujatokea duniani kama bahati mbaya,ama pasipo lengo,lipo lengo....nalo ni kuishi lengo hilo ili nuru ya Mungu iliyopo ndani mwako ionekane ,Bila wewe kuwepo na kuishi maisha yako,lipo jambo ambalo halitakuwa vile linatakiwa liwe,upo kwa ajili ya kuiangaza dunia...wewe ni mwanga...wewe ni chachu ya maendeleo ya dunia hii....si nyota,wala jua,wala miti,wala majani ,wanyama kila uoto ambao unakukosa pale unapokuwa upo duniani pasipo kutenda jambo lililokuleta.....nafasi yako wewe haijazwi na mtu yeyote mwingine,ndio maana umeletwa hapa duniani....amua kutimiza lengo lililo kuleta,viumbe wote wanakuhitaji....ishi kwa ajili ya wengine,wauone upendo,waione amani,waijue faraja,wafahamu kujitolea...na haya yote yanatoka kwako wewe..wewe ni wa pekee


 

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 Comments:

Post a Comment

maoni yako hapa