Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Monday, December 31

UKWELI KUHUSU WEWE

Wewe ndiye mjenzi na mbomoaji wa maisha yako katika nyanja zote kwa fikra zako kwani fikra ndiyo mbegu ndani yako itoayo matokeo kadiri ya sababisho litokanalo na msukumo wa kimazingira. Hivyo mafanikio yako huja kwa kupanda fikra za mafanikio na kutofanikiwa huja kwa kupanda fikra za kushindwa,uma kwa kujua na kutojua. Wewe ni msanifu na mjenzi...

NURU NA GIZA

Bila shaka kila mmoja yu na furaha siku ya leo.Karibu tena katika somo jipya leo hii.Somo hili litakufanya utambue jinsi wewe ulivyo muendeshaji wa maisha yko,ni somo litakalokufanya ujue kuwa wewe ndiye mjenzi na ndiye unayebomoa maisha yako mwenyewe,iwe kwa kutambua ama kutotambua.Karibu tujifunze pamoja Ni mara nyingi tumekuwa tukikumbushana kuwa...

Friday, December 7

Kumbuka wimbo wako

Katika dunia hii ni vema kuyaishi maisha yako pasipo kuigiza,yawe yako halisi..Ukiyaishi kwa juhudi zako,hutapata kuwa na wasiwasi juu ya kifo na matokeo yake...Waheshimu wengine wote,heshimu imani zao,fikra zao na mitazamo yao.Yapende maisha yako,furahia maisha yako,heshimu maamuzi yako katika maisha,sikiliza hisia za moyo wako...Fikiri kuishi...

Tuesday, December 4

IAMBIE NAFSI YAKO

 Tumeumbwa na kupewa mamlaka juu ya maisha yetu na juu ya kila kilicho juu ya nchi,Hivyo tunapaswa kukumbuka kuwa kila kitu tunachokihitaji maishani mwetu kipo katika uwezo wetu tuliopewa na Muumba...mradi tu ulihitaji jambo hilo kwa dhati kabisa toka moyoni mwako.... Kwa kutambua hilo huna sababu ya kuwa na wasiwasi juu ya maisha na juu ya...

Wednesday, October 31

JIFUNZE KUFANYA MAAMUZI MAGUMU

Kuna faida kubbwa sana kwa mtu kujitambua.Utafahamu ni jinsi gani unaweza kuchukua maamuzi ya kugeuza maisha ambayo huyapendi na kuishi maisha mapya,n ndipo utakapokuwa tayari kuchukua hatua ya kufanya maamuzi magumu maishani...amua,kaa na kuandika kila jambo unalhitaji ulifanye kwa mwaka mzima,andika kila jamnbo kwa kina...kwa makini tafuta ...

ONDOA HOFU KWA WENGINE

 Dunia ina watu wengi ambao daima hukatisha wengine tamaa.,hukatisha tamaa ama kwa maneno yao,vitendo  vyao na kwa njia  nyingine mbalimbali....hawa hiufanya dunia kuwa sehemu ya hofu na mataraji yaliyojaa kukata tamaa.... Ni muhimu tukaitangaza dunia yenye matarajio mema kwa kila mmoja ,tunao uwezo huo,timiza wajibu wako kwa njia yeyote...

Monday, October 8

mwanzo wa mafanikio

Pale unapolihitaji jambo lolote kwa moyo wako wote,huwa ndio mwanzo wa mafanikio wa jambo lolote lile.....Msukumo utokao ndani yako ndio mwanzo wa mafanikio yako...kama msukumo ni mdogo utokao ndani mwako ndivyo utoavyo mafanikio madogo...kama ilivyo pia kwamba moto mdogo utoavyo joto dogo pia...Huwezi kupata maendeleo(mafanikio )katika jambo lolote...

Thursday, September 6

ujumbe 2

Ipo siku ambayo hutahesabu tena ni nini unamiliki ama umepoteza....... chuki,hasira na majaribu yote hayatakuwepo Haitajalisha kuwa ulikuwa na sura nzuri ya mvuto ama ulionekana wa sura mbaya wala ngozi,wala jina halitahesabika Ni NINI KITAHESABIKA.... KiTAHESAbika ulichotoa kwa wengine na si ulichopokea Kitahesabika ulichojenga ukiwa duniani,kilichowainua...

Sunday, September 2

UJUMBE

Wakati mwingine huhisi kuwa niandikayo hapotea tuu,hutazamwa tuu,na hata kutotiliwa maanani...hii hainikatishi tamaa...siuzi ujumbe...hutolewa bure...wakati mwingine nafikiri kurudia na kurudia Wakati mwingine nasoma kwa kurudia na kurudia,nami hupata faraja.Siandiki tu kujifurahisha....naandika nikilenga kubadili maisha ya wale walio katika huzuni,kuanguka...

Saturday, September 1

YALIYOPITA YAMEPITA...SONGA MBELE

Wapo wanaotazama mambo ya jana,juzi na yote waliyoyapitia na kukata tamaa,Wakisikia jinsi marafiki wao wanavyowanenea mabaya,wakitazama kila pande na kuhisi hakuna anayewajali,wakiangalia pande zote wasione tumaini,hukata tamaa lakini ukijitambua hutakata tamaa kamwe,kwani utatambua kuwa ni Mungu na wewe ndiye uliyetumaini juu ya yote...Hutaweka matumaini...

AHSANTE WOTE

Rafiki wa kweli ni yule ambaye unaweza kumwamini,ni yule ambaye unaweza kumshirikisha furaha,huzuni na kila tamanio la moyo wako,ni yule ambaye hakuhukumu kwa kufikiri tu,ama kusikia toka kwa wengine,ni yule anayekubali na kuheshimu maamuzi yako,uchaguzi wako na uhuru wako,ni yule ambaye yupo tayari kutumia alichonacho kwa ajili yako,ni yule anayeweza...

Tuesday, August 28

TUNAENDELEA MBELE

KATIKA MAISHA TUNAPITIA MAGUMU.....tunapitia kuanguka mara nyingi...tunapitia kukatishwa tamaa,kusengenywa,kutengwa na hata kudaharauliwa.....tunapitiwa kuumizwa katika mahusiano,kuachwa,kudhulumiwa nk...haya yote hayana budi kutokea,jambo la muhimu ni kuwa tunavumilia yote na licha yakuwa tumeanguka mara nyingi,lakini pia tumesimama mara nyingi...

Monday, August 27

NAFASI YAKO HAPA DUNIANI NI YA MUHIMU SANA

Kwa sababu kila mmoja wetu anahitaji kuthaminiwa,kuheshimiwa na kila mmoja anahitaji kuona wengine wanamjali....mioyo yetu haiwezi kuwa na furaha ya kweli kama hatutakuwa sauti kwa wale ambao wanataka kusema lkn hawapati japo nafasi....kuwa faraja kwa wale wenye machozi,kuwa mwangaza kwa wale wanaohitaji nuru ya kuamsha mioyo yao na ari ya kuyaishi...

Saturday, August 25

WEKA JUHUDI KUJITAMBUA WEWE KWANZA

Wapo watu wanaofikiri kwamba yupo mtu ambaye anahusika juu ya uchaguzi wa wanataka kuwa nani,na kuishi maisha ya namna gani...Wapo wanaofikiri kuwa wenzao ni bora kuliko wao...Wapo wanaofikiri kuwa upo wakati utafika watabadilika tu katika kufikiri,kutafakari na kufanya maamuzi pasipo kuweka juhudi binafsi.Nikupe siri moja katika kutafuta mafanikio,jiulize...

Wednesday, August 22

TUNAPATA KILE TUTOACHO

Nakusihi usome kwa makini makala yenye kichwa cha habari.JINSI GANI TUNAPATA TUWAZACHO hapa http://pongujoseph.blogspot.com/2012/07/ni-jinsi-gani-tunapata-tuwazacho.html   kabla ya kusoma makala hii..    Kabla ya kueleza kanuni hii...nitoe mifano miwili           Kwanza kabisa...tafakari pale unapokuwa...

Saturday, August 18

simama kwa ajili ya wengine

Kila mmoja anacho kipaji chake...haijalishi mzee ama kijana...simama kwa ajili ya wengine..wapo wahitaji,wanyonge,walioshuka moyo..wapo waliokata tamaa,simama kwa ajili yao...unaweza kuhisi kuwa wewe si lolote ..lakini ukisimama kwa ajili ya wahitaji.....utapata furaha isiyo kifani.....natamani sana kuona maisha ya wengi ya kibadilika...ninaweza...

Friday, August 17

THAMINI WANAOKUZUNGUKA.

    Nimefanya utafiti na kupata matokeo kwamba katika Jamii nyingi za waafrika,wengi huwa hawapendi kuona wenzao wakifanikiwa..Mtu huchukia kuona mwenzake kaanzisha biashara,kapata ajira,kagundua kitu kipya,yaani kwa kifupi wengi huingiwa na chuki kuona wengine wakinyanyuka.Mfano,mpogoro yupo radhi kumfanyia fitina mpogoro mwenzake asiendelee,Mbena...

Monday, August 13

KUMRADHI

 Karibuni nyote mnaofuatilia blog hii.  Kwa siku kadhaa nilipata shida kuweza kuandika katika blog hii kutokana na tatizo la kiufundi,akaunti yangu ilipata hitilafu na kuingiliwa,nikapata changamoto katika kuandika......nilikuwa nikiumia kwa kuwa furaha yangu ni kuona kuwa kila mara tunajifunza jambo jipya,ni kuona waliokuwa wanakata tamaa...

Tuesday, August 7

MWALIMU BORA

Wale waliopitia ugumu ,milima na mabonde katika maisha yao ni walimu bora,kwa sababu wanajua maana ya kila jambo walilolipitia,wanajua jinsi gani ya kubomoa ukuta wa mipaka ya kufikiri,wanajua kuumizwa,wanajua faraja,wanajua chuki,wanajua amani,wanajua upendo,wanajua kila jambo walilolipitioa si kwa kusoma nukuu tu,bali kwa kuishi na kupambana...

Sunday, August 5

KILA JAMBO LITOKEALO LINA SABABU, KILA JAMBO HUTUFUNZA

     Ni  kweli kwamba kila changamoto itupatayo huwa na sababu...na huwa ni wakati wetu kujifunza mbinu mpya za kufikia pale tunapohitaji kufika...wakati mwingine tunajifunza kutoshikilia sana mambo ambayo yanatuchelewesha kufika tuendako....wakati mwingine tunakumbushwa kuwa kila mlango mmoja ufungwapo,basi hutoa nafasi kwa...

Saturday, August 4

TUJIKUMBUSHE SISI NI NANI.

     Kwa kipindi hiki cha mwisho wa wiki,ningependa tujikumbushe sisi ni nani,anza na wewe,  Kaa sehemu tulivu,kisha funga macho,vuta pumzi taratibu ,sikiliza na kufuatilia mapigo ya moyo wako,kisha jiuliza maswali yafuatayo  mimi ni nani? kwa nini nipo hapa duniani je ni kwa kiasi gani nimetimiza jukumu langu la kuwepo...

Tuesday, July 31

UPENDO,NDOA NA SHERIA

Mwisho wa makala hii utapata kujifunza mambo yafuatayo ni nini na jinsi gani upendo wa dhati HOFU-ADUI MKUBWA WA UPENDO ndoa,furaha,na huzuni katika ndoa-sababu sheria katika upendo na kushindwa kwa sheria kulinda ndoa jinsi gani utaishi maisha ya furaha katika ndoa nafasi yako katika upendo,ndoa. jinsi ya kuifanya ndoa yako idumu na kuwa na mafanikio...

DUNIA INAKUHITAJI

 dunia inakuhitaji uwatazame wenzako kwa huruma,ukijali mahitaji yao,ukiwainua na kuwafanya wajitambue na kujikwamua(picha kwa hisani ya www.viewtz.com) DUNIA HAIITAJI WATU WENYE FEDHA NYINGI,MAGARI,NYUMBA,NGUO NYINGI AMA WENYE UMAARUFU MKUBWA..DUNIA INAHITAJI WATU WENYE KUJITOLEA KWA WENGINE,WENYE UTAJIRI WA UPENDO,WENYE KUUGUZA,KUPONYA,KUAMSHA...

SONGA MBELE.

 KAMA HUWEZI KUPAA,USILALAMIKE,...KIMBIA,  KAMA HUWEZI KUKIMBIE USIKATE TAMAA,TEMBEA......KAMA HUWEZI KUTEMBEA USIBAKI TU UNALALAMA, TAMBAA,ILI MRADI TU KILA SIKU UNASONGA MBE...

Saturday, July 28

AMUA KUBADILIKA AMA KUBAKI ULIVYO

 ni wewe unaeweza kuamua juu ya kubadilikakuyaendea mafanikio AMA kutobadilika na kubaki ulivyo(picha kwa hisani ya mtandao)                       Ni wazi kuwa unatambua kwamba nazungumzia kuhusu kufanya mabadilko ili kuyafikia mafanikio uliyoyakusudia.Mafanikio...

Friday, July 27

UTAMBUE UHURU WA KUCHAGUA USIO NA MIPAKA

Je wewe unafahamu nini kuhusu uhuru alionao binadamu katika kuchagua,?Je binadamu amewekewa mipaka katika kuchagua maisha(aina ya maisha na jinsi atakavyoishi)?Mazingira yana athari gani kwa binadamu katika kufanya uchaguzi?  BINADAMU TUMEPEWA UHURU WA KUCHAGUA NA UHURU WA MAWAZO USIO NA MIPAKA    ...

...

Tuachane Na Fikra Za Malalamiko, Upanuliwe Wigo Katika Ubunifu Na: Meshack Maganga, Mjengwablog-Iringa. Rais wa enzi hizo wa taifa la Marekani Theodore Roosevelt (Oktoba 27, 1858- Januari 6, 1919) alipata kusema, “What we need is more people who specialize in the impossible”, kwa tafsiri isiyo rasmi ya Kiswahili ni kwamba,...