Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Saturday, July 28

AMUA KUBADILIKA AMA KUBAKI ULIVYO


 ni wewe unaeweza kuamua juu ya kubadilikakuyaendea mafanikio AMA kutobadilika na kubaki ulivyo(picha kwa hisani ya mtandao)
           
          Ni wazi kuwa unatambua kwamba nazungumzia kuhusu kufanya mabadilko ili kuyafikia mafanikio uliyoyakusudia.Mafanikio kwangu nina maana ya kutimiza jambo lolote lile ambalo umepanga kulifanya maishani mwako,ambalo linakuletea furaha moyoni mwak Kila mara tumekua tukisubiri kuchukua hatua ya kubadilika,tumekuwa tukitarajia tutabadilika baadae,kesho,wiki ijayo,mwezi ujao ama mwakani,lakini hakuna wakati zaidi ya sasa,yaani wakati uliopo.Usisubiri kesho ama mwakani,kila jambo lipo mikononi mwako,ni wewe tu kuamua.Na pale tu utakapotambua sababu ya wewe kuishi,ndipo utakapoanza hatua kubwa kuelekea mafanikio.
            Tunao pia uwezo wa kuamua kutofanya chochote,kuamua kubaki tulivyo,kubaki na umasikini wetu,kubaki na malalamiko yetu,kubaki na huzuni zetu...tunao uwezo huu.Tunaweza pia kujifanya tumeamua kubadilika,hasa pale ambapo hatujitambui...tutajifanya tumebadilika ili kuwafurahisha watu fulani,kwa uoga wetu...Tunaweza kuamua hili.Tunaweza kuamua kukaa tu pasipo kazi,tunaweza kuamua kuchagua ujinga badala ya kuelimika, tunaweza kuchagua kuamini uzushi  dhidi ya ukweli,,kuchagua woga dhidi ya kujiamini,yoote haya ni uchaguzi wetu.......Tunaweza kujikumbusha toka kwa Shakespear,ambaye alisema(kwa tafsiri isiyo rasmi)kwamba 'suluhisho la matatizo ytu na maamuzi yetu halipatikani juu,kwenye nyota,bali ndani yetu wenyewe 
          Tunayo jukumu na maamuzi juu ya uchaguzi wa maisha yetu wenyewe,ili kuandaa maisha bora kwa ajili yetu kesho na kwa ajili ya wengine.....na maamuzi haya yanaanza sasa.Anayetafuta mafanikio hatafuta miujiza wala maneno mengi,bali ni msukumo wa maamuzi unaotoka moyoni,kutenda kwa ukweli na kwa bidii,Anayehitaji mafanikio hatazami nyuma na kukata ytamaa,bali hutazama mbele kwa matumaini,akijitolea nafsi yake yote kutenda.Anatambua kuwa hakuna muda wa kujadili afanye nini,wa kujadili mambo yaliyopita,bali kwake,hutazama kufanya tofauti na mawazo ya wasio liona tumaini jipya,wasiouona ushindi mbele...
                  Kwa yeyote anayehitaji mabadiliko katika maisha yake,kama unaona unachokifanya hakibadili maisha yako,badlika ukitazama malengo yako...wewe si jiwe,una akili na uwezo,amua kubadilika sasa.


 ni maamuzi yako kuchukua hatua ama kubaki ulivyo(picha kwa hisani ya the rhododendron  walk,George Mark)
     
     Kama utazidi kuzamisha kichwa chako ndani ya maji,ukiwa huna kifaa chochote,basi tambua kuwa huwezi kutambua upo sehemu gani,unakwenda wapi na umefika hatua gani,mpaka pale utakapoamua kunyanyua kichwa na kutazama,..tunafundishwa kuchukua hatua juu ya kubadili maisha yetu wenyewe.Tambua kuwa ili kubadili maisha yetu ,tambua unataka kuwa nani,weka maleno,chukua hatua kutekeleza malengo,amini uwezo wakop na kuutumia,vumilia mpaka mwisho,...wale wote waliofanikiwa walifanya maamuzi,wakachukua hatua kuyatekeleza.Ukiamua,zipo nafasi zisizo na ukomo..chukua hatua ........kila ukitakacho kitakuwa chako.siku njema

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 Comments:

Post a Comment

maoni yako hapa