Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Friday, July 27

Tuachane Na Fikra Za Malalamiko, Upanuliwe Wigo Katika Ubunifu




Na: Meshack Maganga, Mjengwablog-Iringa.

Rais wa enzi hizo wa taifa la Marekani Theodore Roosevelt (Oktoba 27, 1858- Januari 6, 1919) alipata kusema, “What we need is more people who specialize in the impossible”, kwa tafsiri isiyo rasmi ya Kiswahili ni kwamba, “Tunachohitaji ni watu wengi zaidi ambao wamebobea katika kufanya mambo yanayoonekana ama kudhaniwa kuwa hayawezekani, (specialists)”.

Kauli ya Roosevelt inanikumbusha habari ya vijana wawili waliohitimu Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam. Vijana hawa walipokuwa chuoni muhula wa pili, mwaka wao wa kwanza wa masomo walibuni biashara ya usafiri wa bajaji. Walichanga shilingi laki nane kutoka fedha ya mkopo wanayopewa na bodi ya mikopo ya elimu ya juu, ndipo wakanunua gari hiyo ya miguu mitatu na kufanya biashara hiyo ambayo iliwasaidia sana kuwakwamua kiuchumi.

Kwa mujibu wa maelezo yao ni kuwa wakati wakitambulisha wazo lao kwa wenzao waliambiwa “hilo haliwezekani!”. Wanasema kuwa katika kauli ambayo hawataisahau ni ile waliyoambiwa hivi, “Hiki kitabu cha UDSM kitawapaje muda wa kusimamia hiyo biashara yenu? Labda kama mpo tayari kwa supp zisizokwisha zitakazofuatiwa na disco”. Maneno hayo hayakuwazuia, walianzisha biashara wakaendeleza na bado walifaulu masomo yao. Wakafanikisha kisichowezekana!

Miaka ya karibuni watanzania tumeshuhudia kuanzishwa kwa utaratibu wa kuchangia gharama katika elimu ya juu. Suala hili ndilo lililopelekea kuundwa kwa bodi ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Bodi hii hutoa mikopo kwa wanafunzi hao; katika viwango tofauti tofauti kutegemea na vigezo ambavyo imeweka kwa mujibu wa sheria na taratibu za uendeshaji wa bodi hiyo.

Mabadiliko ya mifumo ya gharama za elimu ya juu nchini Tanzania yanatupa somo muhimu sana kuhusu alama za nyakati. Ni suala la uhakika kuwa siku zijazo mchango wa moja kwa moja wa serikali katika kusomesha vijana wetu utafutika. Hapa naikumbuka kauli aliyopata kuisema Mkurugenzi wa shule ya Star International ya mjini Iringa, Madam Jessca, namnukuu, “Ninawekeza leo kwa kutoa sadaka na kuimarisha biashara zangu, ili siku Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, itakapokosekana, wanangu wasishindwe kupata elimu ya juu” mwisho wa kunukuu. Hakuna haja ya kupambana na nyakati kwa kuzililia zama za Mwalimu J.K Nyerere ambapo elimu ilitolewa bure, bali tukabili nyakati zilizopo na kujipanga kwa nyakati zijazo

Tangu kuundwa kwa bodi hii kumekuwepo na malalamiko mengi sana kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusiana na mfumo huu wa uchangiaji wa gharama pamoja na utaratibu na utendaji wa bodi hii katika kufanikisha lengo hili.

Kuna wadau ambao kwa asilimia mia moja wanapingana na utaratibu huu wa kuchangia elimu ya juu na kuna kundi ambalo linaunga mkono. Sehemu kubwa ya kundi la pili inakwazwa na namna bodi hii inavyotenda kazi zake na kupelekea, mikopo kuchelewa kuwafikia wanafunzi kwa wakati husika, kukosekana kwa mbinu sahihi katika kubaini wapi wanastahili madaraja gani, pamoja na upendeleo (ama uzembe?) katika kupanga madaraja haya ya mikopo.

Bodi hii hutoa mikopo kwa madaraja kwa upande wa ada, “tuition fees” pamoja na fedha ya mafunzo kwa vitendo. Kuhusu fedha za chakula na malazi wanafunzi hupewa kiwango kinacholingana bila kuzingatia madaraja waliyopata. Hadi wakati huu bodi hii inatoa shilingi, elfu tano kwa siku, ama laki moja na nusu kwa mwezi, kama gharama za chakula na malazi.


Kumekuwa na changamoto zinazobainishwa na wanafunzi hawa kwamba kiwango cha fedha wanazopewa hazitoshi katika kuwawezesha kusoma kwa uzuri. Ingawaje vyuo hivi vipo katika maeneo tofauti tofauti, changamoto zinazowakabili wanafunzi hawa nyingi zinashabihiana.

Wanafunzi wengi wanatoka katika familia za kimasikini ambazo pengine hata 70,000/= ya kulipia ada katika sekondari walizotoka zilikuwa zinawapiga chenga. Sasa chukulia kuwa huyu mwanafunzi anapewa mkopo wa asilimia themanini, na yupo katika chuo ambacho gharama ya shahada ya kwanza kwa mwaka wa masomo ni 1,800,000/= Hii ina maana kuwa bodi ya mikopo itamlipia ada shilingi milioni moja na laki mbili na itampa shilingi milioni moja na laki mbili ya malazi na chakula kwa mwaka.

Katika ada atakuwa anadaiwa shilingi laki sita, (600,000/=). Hizi laki sita anatakiwa azilipe kutoka katika ile fedha ya malazi na chakula. Akilipa hizo ina maana anabakiwa na shilingi laki sita tu kwa mwaka wa masomo. (Isisahaulike kuwa bodi ina ukomo wa viwango vya kuwalipia ada wanafunzi inaowadhamini, ukomo huo ni milioni moja na nusu kwa mwaka wa masomo.) Laki sita kwa miezi nane ya masomo, kulipia pango, kununua chakula na kujipatia mahitaji mengine ya msingi kiuhalisia haitoshi.

Tatizo la mikopo isiyotosha elimu ya juu ni la kimtambuka kwa maana kuwa linahusisha pembe nyingi. Kuna suala la ada kubwa katika baadhi ya vyuo, kiwango kisichotosheleza cha fedha inayotolewa na Bodi ya mikopo kwa siku kwa chakula na mavazi, mfumo wa utoaji wa elimu ya juu nchini pamoja na fikra zilizopo miongoni mwa wanafunzi wengi wanaosoma elimu za juu.

Mwanazuoni mmoja wa nchi za Magharibi, G.K Chesterton amewahi kuelezea shida inayowakumba watu kupata ufumbuzi kwa matatizo yanayowakabili, yeye anasema “It isn’t that they cant see the solution. It is that they can’t see the problem” (Sio kwamba hawaoni ufumbuzi wa tatizo, ila ni kuwa hawalioni tatizo). Kuwa na tatizo ni kitu kimoja na kulielewa tatizo (chanzo cha tatizo, lilipo na madhara yake ikiwa halitatatuliwa) ni kitu cha pili. Tuna tatizo la mikopo isiyotosheleza kwa wanafunzi wa elimu ya juu lakini ufumbuzi wake umeendelea kuwa suala la kufikirika na imebaki kulaumiana.

Wanafunzi wa elimu ya juu na baadhi ya wadau wanadhani kuwa suluhisho la tatizo hili ni kuongezwa kwa kiwango cha mikopo. Serikali inasikia lakini haitendi kwa mujibu wa matakwa haya. Tayari pande mbili husika hazijakubaliana na ufumbuzi wa tatizo hili; ina maana kuwa eidha upande mmoja haujalielewa tatizo vizuri ama pande zote hazijalielewa.

Hata hivyo mwathirika mkubwa ni huyu mwanafunzi anayesomeshwa na bodi ya mikopo katika taasisi hizi.Hakuna namna zaidi ya mwanafunzi huyu kupanua wigo wa fikra zake na kuona ni namna gani ataishinda changamoto hii kwa mbinu na njia zilizo halali. Daima ufahamu uliopanuliwa katika njia mpya za kupata majibu ya changamoto, haurudi kamwe katika mipaka yake ya mwanzo. Zikomeshwe fikra za malalamiko, wigo upanuliwe katika ubunifu, badala ya mawazo ya kuilaani Bodi ya mikopo na serikali kwa mikopo isiyotosheleza ni vema kupanua fikra katika kujitegemea

Huu ni wakati ambao vijana wetu wanatakiwa kushusha chini vidole vyao vilivyoielekea serikali na kutazama ni nini kinaweza kufanyika kujikwamua. Mwanaharakati wa kweli hupambana kwa ajili yake na kwa ajili ya vizazi vyake vijavyo. Tujiulize, maswali yafuatayo. Je, vizazi vijavyo vitaishije pindi mchango wa serikali kwa elimu zao utakapofutika, ikiwa hatuweki misingi ya kujitegemea sasa? Vilio vyetu vimesikilizwa kwa kiasi gani? Je, tuendelee kulia ama tufute machozi, tujifunge mikanda tutazame tatizo kwa namna tofauti?

Hakuna maana ya kuweka nadhiri za chuki zitakazoliangamiza taifa kutokana na yale yanayopitiwa kwa sasa. Nafahamu wapo vijana wetu ambao kutokana na adha wanazozipata katika utaratibu huu wa mikopo, wananadhiri kuja kulipiza kisasi. Nao wanaweka nia za kuja kupukutisha rasilimali za taifa ili kunufaisha matumbo yao na ya ndugu zao. Vijana wetu wa vyuo vikuu lazima watambue jambo hili, ya kuwa uovu wa baadhi ya viongozi waliopo madarakani haupaswi kuhalalisha wengine kutenda maovu. Msomi ni lazima awe na ndoto za kuubadili ulimwengu wake kutoka hatua moja kwenda nyingine iliyobora zaidi.

Ipo haja kubwa sana kwa wanafunzi wa elimu ya juu kujijengea utamaduni wa kijasiriamali ili kwa fedha kidogo wanayokopeshwa waweze kuzalisha na kufidia upungufu unaojitokeza katika gharama za masomo yao. Nikigusia suala la ujasiriamali inawezekana kuwepo na vikwazo vingi, ikiwemo muda na mazingira ya kufanya huo ujasiriamali, ukosefu wa rasilimali (mitaji) na mengine mengi upendayo kuorodhesha. Anayevuka na kutatua vikwazo hivyo, huyo ndiye “specialist” wa yasiyowezekana!

Wanafunzi wengi waliopo katika taasisi zetu si wenye juhudi katika kufikiria, ubunifu na kufanya kazi kwa kujituma. Waangalie wanafunzi hawa jinsi wanavyoutumia muda wa likizo zao ndefu na fupi, mara nyingi hawafanyi kazi eidha za kulipwa ama za kujitolea. Mara nyingi hutoa sababu zinazosema na kuonesha kuwa hakuna kazi. Wananata, hawataki kukaa vijijini hata kama kuna fursa nyingi, wanataka kumalizia likizo zao Dar es Salaam.

Kuna wakati unaweza kudhani kuwa vyuo vya elimu ya juu hupendelea kufanya udahiri wa kimikoa, kwa sababu wengi wanataka kutambulika kama wakazi wa majiji hasa Dar es Salaam. Miezi mitatu ama mine ya likizo mtu yupo jijini kwa mjomba, binamu au kwa wa kutoka kijiji kimoja kule Songea, hana kazi zaidi ya kula, kulala, kuoga na kuangalia TV. Wakati mwingine analala sebuleni, na kulala kwake ni mpaka wote waende kulala! Kama mwanafunzi huyu angeenda hata kijijini kwenye kata ya nyumbani kwao akajitolea kufundisha shule ya kata kwa miezi minne angekuwa amezalisha angalau laki mbili!

Ninao mfano wa rafiki yangu mmoja ambaye ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Mzumbe, ambaye amekuwa mbunifu na alishaupiga teke ulimbukeni wa kujiona kuwa eti “wa elimu ya juu” kuna kazi hatakiwi kuzifanya hata kama zinamwingizia kipato. Huyu kila likizo huwa anarudi kijijini kwao na huko huutumia muda wote katika kufanya biashara ya alizeti. Huzunguka vijiji mbalimbali akikusanya na kisha kusafirisha alizeti hizo kwenda mjini. Katika moja ya likizo yake ya miezi minne, aliingiza mtaji wa shilingi laki tatu (fedha za bodi ya mikopo) na kuzalisha jumla ya shilingi milioni moja na laki sita.

Hawa wanafunzi wa vyuo vya juu, imewapasa kuwa na macho ya ndani yenye uwezo wa kuvumbua na kuzitumia fursa. Kuna kuwekeza kwa aina nyingi ambako wakati mwingine mtu si lazima awepo muda wote katika kusimamia alivyowekeza. Inawezekana kumiliki hisa katika makampuni, kuingia ushirika wa kibiashara (partnership) ama kuitumia jamii ya wanafunzi wanaowazunguka, kubuni biashara ama miradi itakayowaingizia vipato.

Pale juu katika makala haya nilitaja pembe zinazochangia mtambuka wa tatizo hili. Ingawa niliacha pembe zingine tatu, ni dhahiri kuwa zinachangia sana katika kufanikisha ufunguzi wa hizi fikra  za hawa wanafunzi wa elimu ya juu. Nitachambua pembe hizi katika makala mengine, lakini itoshe tu kusema, ukiwa na tatizo ni lazima ujikague na kujirekebisha vizuri kabla hujamvaa anaechangia kukua kwa tatizo lako.

Leo hata kama wanafunzi hawa wakaongezewa fedha na kulipwa 20000/= kwa siku, bado watagundua kuwa fedha hiyo haiwatoshi. Suluhisho sio kuililia serikali pekee wakati tumekaa na kubweteka. Tutalala, tutaamka, tutaandamana na kujikuta bado tuko pale pale. Badala ya kuwaza ukahaba, wizi na ujanja ujanja wa kukopeshana na kudhulumiana hebu wasomi wetu waanze kutumia taalveuma zao kufanya ubunifu na kujikwamua. Hii inawezekana ila kwa wale watakaojitolea ku-specialize katika yasiyowezekana.
 Na kila mwanafunzi wa elimu ya juu anayeguswa na hili analazimika kuwa specialist wa yasiyowezekana!

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

1 Comments:

  1. Je! Unahitaji mkopo wa haraka ili uondole deni lako au unahitaji mkopo wa usawa ili kuboresha biashara yako? Umekataliwa na mabenki na mashirika mengine ya kifedha? Je! Unahitaji uimarishaji wa mkopo au mikopo? Utafute tena kama tuko hapa kufanya matatizo yako yote ya kifedha kitu cha zamani.

    Hii ni kampuni rahisi ya mkopo. Tunatoa mikopo kwa wale wanaopenda kiwango cha riba cha 2%. Mipangilio mbalimbali kutoka $ 5,000.00 hadi dola za dola 100,000,000.00.

    Mikopo yetu ni bima nzuri kama usalama wa juu ni kipaumbele chetu.

    Wasiliana nasi kwa barua pepe: oceanfmortgages@gmail.com


    Uzidi
    Max Bent
    oceanfmortgages@gmail.com
     
    Mikopo ya 2% ya awali na dhamana
    oceanfmortgages@gmail.com

    ReplyDelete

maoni yako hapa