Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Wednesday, July 18

WEWE NI BORA JINSI ULIVYO,

i mwanariadha maarufu wa afrika ya kusini,Oscar Pistorius
WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO....ULEMAVU NI FIKRA ZAKO .

Ni wakati mwingine wa kujitambua,sisi ni akina nani na tunakwenda wapi,na tunawezaje kwenda tuendako.....,Leo hii tukijadili kwa undani,uwezo tulionao,tusioutambua..Na mwisho tutatambua ya kuwa,ulemavu unaotambulika wa viungo si kitu,bali ulemavu mkubwa ni wa kukosa kutumia uwezo wetu tulionao wa kufikiri na wa kuumba vitu vipya tukiifanya dunia kuwa sehemu bora na kuishia kuishi kwa uoga na kulalamika,tukitegemea wengine kufikiri na kutenda kwa ajili yetu,tukiwa na macho yasiyo upeo wa kuona,tukiwa na akili,na tusiitumie.......(huu ukiwa ni ulemavu mkubwa)
SINA MIKONO,LAKINI HAIMAANISHI YA KUWA SINA UWEZO WA KUFIKIRI WALA KUTENDA (picha kwa hisani ya mtandao)
  Wewe ni kiumbe wa kipekee,uwe na miguu yote ,uwe umekosa miguu, ama mikono ,ama kiungo chochote cha mwili,bado unabaki kuwa kiumbe wa pekee aliyeumbwa,ukifanana na Muumba (asili yako) kwa uwezo wa kutenda na kuumba(wapo watakaohisi ya kuwa nafananisha moja kwa moja na Mungu,

Ni vema tukatambua ya kuwa Mungu anabaki kuwa Muumba kwa asili yake,na sisi tunabaki na ubora aliouumba,tukifanana na yeye aliye asili ya yote.....). Hivyo uwezo wa binadamu kuyatawala mazingira yake haupo kwenye nguvu za mwili(misuli),haupo kwenye miguu,haupo kwenye mikono bali upo kwenye fikra zake.

 Kwa kifupi,wewe ni bora jinsi ulivyo...uwe na miguu,uwe huna miguu,unabaki kuwa binadamu,unabaki kuwa kiumbe bora wa Mungu,...wewe ni bora jinsi ulivyo.....

 Kila tunapojitazama sisi,tusiishie kutazama sura tu,tusiishie kutazama rangi tu,tusiishie kutazama mvuto wa viungo vyetu tu, bali tujitazame ndani yetu ambako hutufanya tutambulike kwa wengine, kwani ndiko kunakoumba na kutufanya tuchague tutakuwa akina nani,tutaishi maisha yapi,na kutambua matokeo ya uchaguzi wetu kwa wengine...

Yupo kijana mmoja,anayetambulika kwa jina la Nick Vujicic,aliyezaliwa akiwa hana mikono na akiwa na miguu mifupi sana,akizaliwa katika familia isiyo na uwezo mkubwa,alifika wakati akajitambua kuwa jinsi alivyo ni bora sana. Kautambua uwezo wake ulio ndani mwake,akasoma na hata kumaliza chuo kikuu,akitenda mambo makubwa katika michezo,na hadi sasa ni mwenye mafanikio aliyoyakusudia, Anatambua kuwa nuru ya maisha yake haionekani tu kwa sura yake bali kwa uwezo ulio ndani mwake...akitenda kwa ajili ya wengine....Huyu anatufunza ya kuwa ,sisis ni bora jinsi tulivyo...na tunastahili ushindi wowote kadiri ya uchaguzi wetu
NICK VUJICIC AKIWA KATIKA MOJA YA MICHEZO AIPENDAYO,WEWE NI BORA JINSI ULIVYO
NINATAMBUA YA KUWA MIMI NI BORA JINSI NILIVYO,NIKICHAGUA MAISHA YANGU,NA NJIA YA KUISHI,NI KIYATIMIZA YOTE PASIPO KUJALI VIKWAZO VILIVYOPO,HATA PANAPOONEKANA HAPAWEZEKANI,MIMI NITAWEZA
nayafurahia maisha kwa kuwa mimi ni bora jinsi nilivyo
. KWA KUWA NINAJUA NA KUTAMBUA KUWA MIMI NI BORA JINSI NILIVYO,NIKIWA NINA UWEZO MKUBWA NDANI MWANGU...NINAFURAHIA MAISHA YANGU,NIKIFURAHI,NIKICHAGUA MAISHA NA KUYAISHI...WEWE JE
NINAFURAHIA MAISHA YANGU,NIKIFURAHI,NIKICHAGUA MAISHA NA KUYAISHI...WEWE JE
Hivyo basi,ulemavu ni tatizo la kifikra kuliko ilivyo kwamba,ulemavu ni kukosa viungo fulani vya mwili.Hii ni tafsiri yangu ya kimtazamo....kama nlivyoandika katika makala iliyopita yenye kichwa cha habari..NI JINSI GANI TUNAPATA TUWAZACHO...Soma hapa.

NIKIJITAMBUA,NITATAMBUA UWEZO WANGU ,NITAWEZA KUCHAGUA MAISHA YANGU NA KUYAFIKIA MAFANIKIO AHSANTENI SANA
Ni wakati sasa kuamka na kuondoa fikra zote za vikwazo ambavyo vinatufanya tusifanikiwe Ni wakati sasa wa kutambua kuwa sisi ni zaidi ya vile wengine wanavyotutazama,ama kudhani,na ni zaidi ya tunavyofikiri....sisi ni bora jinsi tulivyo na kila wakati tunapojitambua tunapata nafasi ya kuchagua maisha ambayo tunayapenda,tukiyaishi kwa furaha,na kuanzia sasa, hutasikiliza maneno ya wengine kuwa u mbaya,u kituko,ama hauvutii.....haya kwako si kitu,kwani wewe ni bora ukiwa na uwezo wa kuchagua na kuyaishi maisha yenye furaha..na hayo ndiyo mafanikio. PONGU JOSEPH

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com