Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Thursday, July 12

DINI NA UUMBAJI WA WAAMINIO.

tazama Mungu umtafutae yupo ndani mwako
TAZAMA MUNGU UMTAFUTAE,YU NDANI MWAKO

Waimbaji huiwakilisha nuru ya Mungu kwa nyimbo.Waandishi pia hutufundisha yatokayo ndani mwao kwa kutumia maneno na kuyaandika.Wahubiri huifundisha nuru ya Mungu kupitia vipawa vya kuzungumza na kwa mifano mbalimbali hukumbusha uwezo wa Mungu ulio ndani mwetu.Mjasiriamali vivyohivyo hutenda kwa kutumia maneno yao ya kibiashara na bidhaa zenye kumjali mnunuzi.

Je wewe binafsi unaufundisha vipi utukufu wa Mungu?

Hakuna aliye hapa kwa bahati mbaya.Tuna sababu ya kuwepo duniani.
Nayo ni kufurahia uumbaji wa Mungu na kuitengeneza dunia bora.
Je,ni jinsi gani dini na imani ndani yake inatujenga kutambua sababu ya sisi kuwepo?

Nianze kwa kukusihi usome kuanzia mwanzo mpaka mwisho,ili uweze kuelewa ni nini nimekusudia kukifikisha kwako.....SI KAWAIDA KWANGU KUTAZAMA JAMBO KATIKA UPANDE HASI,lakini nitajadili upande hasi wa dini kwani ndicho kilichonisukuma kuandika kwa sasa,ninakusihi uchukulie hii kama elimu chanya ili ikusaidie kujadili na kujitambua.

 Dini inamaanisha jumla ya imani ya binadamu kadhaa pamoja na mafundisho wanayotoa kuhusu yale ambayo wanayazingatia ama kuyasadiki, yaani mambo ya roho, kama vile kuhusiana na Mungu, maisha na uumbaji-hii ndiyo maana ya kimtazamo kuhusu dini...Japo kimantiki hii si maana halisi.

Kila anayeingia katika imani hii,ama dini,matazamio yake huwa ni kwamba,dini itakuwa ni suluhisho la kila jambo kwa binadamu.....dini inatazamiwa kuwa ndio amani,ndiyo furaha,ndio umoja,ndio huruma,ndio usawa,ndio kila chimbuko la ubinadamu,na kikubwa kumfanya binadamu ajitambue yeye ni nani,anatoka wapi na anakwenda wapi......

Lakini kwa sasa imekuwa ikiwafanya binadamu kuwa tegemezi,wasio huru katika kila nyanja ikiwemo uhuru wa kufikiri usio na mipaka,uhuru wa kuchagua(simaanishi uchaguzi mbaya). Dini imekuwa kifungo cha kuwafanya wengi wasitumie vipawa walivyonavyo na hata wasisikilize sauti ya Mungu inayowatuma kutenda kwa ajili ya utukufu wake.(Unaweza kuuliza kivipi,jibu ni fupi...imani nyingi katika dini zimeweka mipaka ,inayomfanya muamini asifikiri juu ya hapo)NA KUWAFANYA wawe na maisha yasiyo na mwelekeo wa ushindi na hivyo kuamini kinyume na matarajio ya imani yenyewe.

1.KUMWOGOPA MUNGU
  Dini nyingi zimewafanya waumini wake wamwogope sana Mungu na kumuona kuwa ni adui.Wengi wamekuwa wakimuona Mungu ya kuwa yu mbali sana nao,asiye rahisi kufikika,asiye rahisi kuongea nae.

Wanasahau ya kuwa Mungu wamtafutao na kumwogopa yupo ndani mwao..Nae ni sauti iliyo kubwa kuliko utashi wa mtu mwenyewe,kuliko awazaye mtu,.Wanasahaulika ya kuwa yeye huzungumza na yeyote yule ,kwa wakati wowote pale kila mmoja awaye tayari kumsikiliza.

NAYE NI RAFIKI MKUBWA WA NAFSI YA KILA MMOJA WETU, Mungu ni mpole,mwenye huruma,asiyetazama tutazamavyo sisi,bali hutazama mawazo ya mioyo yetu,naye hujibu maombi ya mioyo yetu,na si maneno yatokayo kwa mtu..

 Hivyo kwa matokeo hayo dini hujenga jamii ya watu wenye kujiogopa wenyewe,wakimwogopa Mungu aliye rafiki mkuu,wakiishi maisha bandia ya kujionesha kwa wengine hasa wale wanaowaongoza,wawaone ya kuwa wamejaa nguvu za Mungu na matendo yaliyotukuka,huku wakifanya kinyume kwa siri(siri kwa binadamu wenzao,lakini Mungu ambaye tupo nae nafsini mwetu anatutazama kwa ubandia wetu)

2.KUISHI MAISHA YA WENGINE 
Dini zimekuwa zikiwafundisha na kuwafanya watu waishi maisha ya wengine na kuchagua maisha ya wengine waliopita na kuyaacha yetu yale tuliyoitiwa ili nuru yetu ing'ae kwa wengine....Hapa naomba nieleweke vizuri kuwa viongozi wengi wa dini wamekuwa wakiwafundisha watu kuishi kama fulani aliyepita(wapo wanaowaita watakatifu,wengine viongozi wao waliopita....)wakijitesa,wakijinyima pasipo sababu ya msingi,(SABABU ISIYO MSUKUMO WA MHUSIKA BALI MSUKUMO WA NJE}na matokeo yake kuishi maisha yasiyo ya furaha kwani mwisho hugundua ya kuwa furaha huja pale unapoishi maisha uliyoitiwa wewe mwenyewe,
Ukiyaishi kwa kujitolea si kwa ajili ya kuneemeka,bali ili wengine waitambue nuru ya Mungu aliyo ndani ya kila mmoja,na wale wasioamini ,wajitambue na kuiishi.

Dini zitakufundisha kuishi maisha ya wengine na matokeo ya wengine lakini ROHO WA MUNGU aliye ndani mwetu hutufundisha kuishi maisha yetu halisi ili tufikie katika matokeo mapya,yamtangazaye Mungu na utukufu wake.
Wengi wameingia kwenye mkumbo kwa kufuata tu imani ,kwa sababu ni za wazazi wao

3.DINI NA WATEULE

Dini hutoa picha ya matabaka,ya walio wakuu kuliko wengine,na wale wanyonge(watawaliwa) wanaosubiri pia kupewa ukuu na Mungu.inatokeaje? Viongozi wengi wa dini wamekuwa wakijipa ukuu na kuwaaminisha wengine kuwa ukuu huo umetoka kwa Mungu.Viongozi hawa wamejitangazia utawala,wakichuma kutoka kwa wengine ambao daima huwaogopa na kuhisi labda,Mungu kateua baadhi,na kwamba wao si wateule.

UKWELI NI KWAMBA,KILA MMOJA YU SAWIA KWA 
MUNGU,Yu bora akiwa na uwezo na nguvu za kuponya,kuamsha upya ari ya kila kitu,kulea,kuwanyanyua wanyonge badala ya kuwakandamiza,na ukweli ni kwamba,kwa sababu tuu mfano wa Mungu(tukifanana katika nguvu )tunauwezo wa kufanya chochote kile,kuyafikia mafanikio makubwa,kuvumbua vitu vipya,mradi tu tumetambua uwezo huu na kuchagua kuutumia  

aliye mkuu yu ndani mwetu,sote tu bora
kila mmoja akitumia kipawa chake vyema,basi huwa mkuu..tukumbuke aliye mkuu ni yule atendaye yote kwa ajili ya wengine pasipo kutegemea malipo,aliye tayari kuona wengine wakinyanyuka na kuendelea mbele,asiyetengeneza matabaka,ambaye kwake kila mmoja ni sawa,na katika yote,upendo humsukuma kutenda

Tunaweza kuyaona matokeo ya dini,ni jinsi gani inaumba mustakabali wa waamini wake dini zimekuwa ni chanzo kikuu cha matabaka na ubaguzi duniani hasa kutoka kwenye imani na mafundisho ya msingi ya imani husika,dini moja hujiona ni bora kuliko nyingine...tena zinawafanya baadhi kujiona wao ni wateule na kutengeneza tabaka la wanyonge tofautti kabisa na makusudio ya MUngu.mf. mkatoliki anajiona ni bora na ni mteule ukijilinganisha ma mlutheri,mkristo anajitazama kama ni mteule akijilinganisha na mwislamu.mlokole anajipa sifa ya kuwa mteule pekee wa mungu akijilinganisha na wengine...hili ni kinyume kabisa na malengo ya Muumba ya kumuumba kila binadamu na kumfanya kuwa sawa na mwingine..dini zimeleta imani iliyopelekea matabaka..choyo,majivuno,utengano na hata kutowasaidia wengine kwa kuwaona si wa darajasawia... tukirejea vita na vurugu nyingi ni zile ziletwazo na dini...rejea ireland,nigeria,sudan,uturuki zamani.....tena hizi ni vita kati ya dini kubwa zinazofundisha usawa na upendo lkn zikishindwa kuonesha matokeo bora... dini pia zimekuwa ni chanzo cha kumfanya binadamu kuwa mtumwa wa mawazo yake naa mazingira yake...zinafundisha kinyume cha makusudio ya MUumba ya kumfanya binadamu kuwa huru na kuyatawala mazingira yake...zinafundisha utegemezi huku viongozi wakuu wakiwatumia waumini wao kama daraja la kujipatia utajiri na utawala...

Mbele za Mungu hakuna aliye mkuu na wala mtawala...kila mmoja amepewa nguvu na uwezo na anapaswa kuzitumia kama nuru ya utukufu wake MUNGU hapa duniani... Ni WAKATI SASA KUTAMBUA YA KUWA DINI ya kweli ya kila mmoja,ipo ndani mwake...na kuwa ukitambua hilo,utakuwa huru,mawazo huru yasiyo na mipaka,kila jambo litawezekana na li ndani ya uwezo wako kwani Mungu aliye suluhisho la yoote,yu ndani mwako.

Lengo langu si kupinga uwepo wa dini,lengo langu ni kukufanya ujitambue na unyanyuke,uwe na hofu ya kweli,hofu ya kuona unamaliza uwepo wako hapa duniani pasipo kuifanya nuru ya Mungu iliyo ndani mako,ing'ae......hofu ambayo itakufanya utumie maisha yako yote kuwainua wengine.....walio wahitaji,walio wanyonge,walio wafungwa na kila mmoja ambaye upendo tu,huwaamsha

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com