Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Monday, July 23

SHUKRANI

    SHUKRANI KWA KUJALI NA KUTHAMINI


Kila binadamu huhitaji kutambulika na kila mmoja wet u hufurahi kuona ya kuwa wengine wanamjali na kuthamini mchango wake.....kile anachokifanya,ama kukisema.......kwa kutambua hili,nachukua  nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa wale wote ambao wamekuwa wakitembelea blog hii.
  Shukrani yangu ya kwanza iende kwa Muumba wa vyote,ambaye ndiye aliye asili na chemchem ya elimu yote,kwa kuniweka salama na kunifanya mimi nijitambue ni nani,kisha kushiks kalam na karatasi na kuandika.......yale ambayo yanawaamsha wengi,na kuwafanya si tu wajitambue...bali wasimame na kuchukua hatua ya kuishi maisha wanayoyakusudia,wakijitolea kwa ajili ya wengine.
  Pili kwenu ninyi mnaoingia katika blog hii na kushiriki katika kusoma,na hata kuwaeklimisha wengine.Mnapoonesha kujali na kutaka tufike mbali zaidi na kuwaamsha wengi.Shukrani yangu kwangu ni kuendelea kujitolea zaidi,kuandika kwa sababu najua kila wakati yatupasa kutazama ni jninsi gani tutashinda.Si kwamba mimi ni mwalimu,bali ninyi mnaoingia na kushiriki kutoa maoni...mmekuwa walimu wangu...najifunza mengi kupitia wote wanaotuma maoni na wengine wengi.Rai yangu kwenu ni kwamba waalikeni wengine wengi tujifunze.....kama unao uwezo print pasipo kuathiri umiliki,wape wengine wasioweza kufikia huduma hii .....kuwa nuru kwa vitendo...amsha walio wahitaji..jitolee kwa dhati.
                                        

   chagua kuwa chemchem ya wengine kuamka

    Haikuwa  rahisi kuanza kufanya kazi hii ya uandishi....auonae mwisho husukumwa na upendo ,kutenda pasipo kukata tamaa,kuna furaha katika kutoa kuliko kupokea,na ndio maana tunaendelea mbele........Zipo blog nyingi sana,zinazofahamika sana na zenye kutembelewa na maelfu wa watu.......sisi tumeanza ....tutafika huko.Kwa ushirikiano wetu tutafika,lengo likiwa kuwafanya wengi wajitambue,na kuamsha upya matumaini ya wengi......tutafika,kwani katika mapambano(ushindani),wapo wenye kasi,wapo walio nanguvu...lakini anayeshinda ni yule anayeamini katiaka ushindi.....Tutashinda kuwafanya watu wajitambue,tutashinda kuamsha matumaini,tutashinda na kufundisha upendo....
    Natambua ya kuwa  mimi na wewe tunayo sababu ya kuwepo hapa duniani,nikitambua hilo,nitaishi kwa upendo,nitafundisha upendo na kuufundisha  kwawengine si kwa kuusema tu bali kwa kuuishi.Nitajiamini na kutenda kwa upendo..nikijitolea kwa ajili ya wengine pasipo kujali malipo ,ama dharau na kejeli.,kwa sababu hivi havitabadili ukweli ya kuwa mimi ni nani ....nitajitolea na kushiriki kuwaamsha waale wote walio wahitaji..nimejifunza kuwa mimi si chochote pasipo wengine,hivyo matendo yangu na majitoleo yangu yatatazama furaha ya wengine,nikiwapenda na kuwajali kama ninavyoitendea nafsi yangu....nina imani ya kuwa nitakua na kufikia mafanikio hata pale panapoonekana kuwa hapawezekani...kwa pamoja tutaweza
    Shukrani ziende kwa familia yangu,kwa wote waliokuwa tayari kujitolea ili blog hii ifanikishe lengo lake..Ahsante Mtaki R Muyenjwa Gamba kwa ushauri wa kiufundi  nilipohitaji,Lazaro Mafie,Faith Kassano,na wote walioshiriki kwa kila namna.

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 Comments:

Post a Comment

maoni yako hapa