Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Sunday, July 15

MWANAMKE-USHINDI ULIOFICHIKA

MWANAMKE HUSIKIA MLIO WA UA HATA UPITAPO UPEPO

 Lengo langu katika makala hii si kufananisha(kulinganisha )kati ya mwanamke na mwanamme,hii ni kwa sababu hakuna kilicho bora kuliko kingine....kila kitu kipo vile kilivyo na ubora huja na kukamilika pale mtu anapotumia uhuru wake wa kuchagua,kuchagua anavyotaka awe,aishi....na kila achaguapo huwa.

Lengo langu ni kutaka kufunua yale yaliyofichika kuhusu mwanamke......ni baada ya kujifunza kupitia wanawake wengi......nikapata hisia za kuandika kuhusu kiumbe hiki kilicho bora,ishara ya upendo,uaminifu,huruma na chemchem ionekanayo ya ubinadamu na uwezo wa Mungu kwa mwanadamu....hisia zinanituma kumuona mwanamke kuwa ni ukamilifu aliouumba Mungu baada ya mwanaume kuwa na mapungufu mengi.(nieleweke kuwa simaanishi mwanaume si bora)(kwa Mungu kila kitu ni bora kadiri alivyokiumba)...

yapo mambo mengi ambayo mwanaume alikuwa ameyakosa kuitimiliza dunia.....hivyo mwanamke akaumbwa akikamilisha yale ambayo yalikuwa ni muhimu(alikamilika yeye kama mwanamke katika dunia timilifu na si kwamba anautimiliza ukamilifu wa mwanaume,mwanaume anabaki kuwa bora jinsi alivyoumbwa,na mwanamke anabaki na ubora wake, wote wakiuishi utimilifu wao kwa ushirika wao
 .
 Maisha yetu huwa yapo katika mzunguko...yanaanza na maisha fulani,yakimalizika,huanza mengine,mfano tupo hapa duniani,baada ya kumaliza maisha yetu hapa,huenda kuanza maisha mengine mapya,kadiri tunavyochagua.......anayefahamu hili anathawabika kwa ufahamu wake...lakini anayeliishi...ana hekima na hufanikiwa...
 mwanamke huishi kwa kufuata mfumo huu....hata pasipo kutambua.,.mwanamke hukubali haraka maisha anayoyaishi..akiyaishi pasipo kuigiza...akitenda upendo...akiishi huruma,akiishi ubinadamu,akiishi kwa kila matarajio ya maisha ya baadae.....

Mwanamke huyaishi maisha yake kwa unyoofu wake...pale anapoamua kuishi kwa dhati,huishi kwa dhati..hulea kwa dhati,hukarimu kwa dhati,hufungua moyo wake kwa wengine kwa dhati....hushiriki na wengine katika kila jambo linalohitaji ushirikiano....huuguza kwa dhati,huvisha kwa dhati...na hii ni ishara ya kila mafanikio katika maisha...yaani kulichagua jambo na kulifanya kwa dhati...wanaume wachache huweza kuamua hivyo...wanaume hugusa hiki na kile,hufanya kwa muda tu,hutamani dunia bandia,huchelewa kukubali maisha yaliyo halisia.....

MWANAMKE ,UPENDO,UVUMILIVU ULIOTUKUKA....HATA PALE ANAPOONEKANA KUSHINDWA..HUSIMAMA-HUJITOLEA KWA DHATI HATA KATIKA NYAKATI AMBAZO YEYE HUHITAJI ZAID   
 Mwanamke huuona upendo usioonekana,hutambua wakati wa kulia,wa kucheka,anatambua wakati wa kulishika jambo (na kulishika kwa moyo wake wote,) na anafahamu wakati wa kuachana na jambo linalomuumiza na kuanza upya maisha.....huu ni mfano bora wa mafanikio katika maisha..................yaani kulishika jambo kwa dhati....na kuyaacha yale yanayoturudisha nyuma,kwani mara nyingi tunashindwa kwenda mbele kwa sababu tunashikilia mambo ambayo yanatuumiza na kutufanya tuhindwe kwenda mbele......mwanamke huweza kuyatambua mambo haya vema..........hata akitelekezwa,husimama na kuanza upya maisha...ishara ya uvumilivu na ishara ya kujikubali na kujiamini na kwenda mbele hata pale ambapo wale wanaomzunguka hawaamini ya kuwa....ATASIMAMA TENA
kwa mwanamke majaribu kwake ni mtaji wa ushindi
 Kwa mwanamke majaribu kwake ni mtaji wa ushindi......anapoonekana kuwa hatatoka,amechimbiwa.......yeye kwake ni sehemu anayejipika,anayojiandaa kunyanyuka na kupaa juu...huyu ni mwanamke ambaye jamii imemfanya aonekane dhaifu,tegemezi....lakini hakika mwanamke akijitambua na KUSIMAMA......ushindi kwake ni lazima
MWANAMKE HUFURAHIA MAISHA,NA KWENDA NA MDUNDO WA MAISHA
 MWANAMKE HUFURAHIA MAISHA,NA KWENDA NA MDUNDO WA MAISHA,AKIJALI,AKIISHI KWA UPENDO,AKIHUDUMIA NA KUAMSHA ARI YA KUANZA UPYA MAISHA KWA WALE WALIOKATA TAMAA

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com