Nuru Ndani Yako

Nuru Ndani Yako
Nuru Ndani Yako
Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.

KARIBU SANA

HONGERA KWA KUCHAGUA BLOG HII.MAISHA NI UCHAGUZI...NA KILA UCHAGUZI NI SAHIHI....KILA UCHAGUZI UNA MATOKEO YAKE.......KUCHAGUA KUSOMA YALIYO KATIKA BLOG HII KUTAKUFANYA UJITAMBUE,,UUJUE UWEZO MKUBWA ULIO NDANI MWAKO NA HIVYO KUFIKIA MAFANIKIO UNAYOYAKUSUDIA........WEWE NI ZAIDI YA UJIONAVYO,NI ZAIDI YA UJIPIMIAVYO.....UTATAMBUA YA KUWA MUNGU AMBAYE KILA UCHAO WATU WANAMTAFUTA...YU NDANI MWAKO.....UTATAMBUA KUWA U MWANGAZA.....NA UTATAMBUA JINSI YA KUUTUMIA KUWAMULIKA WENGINE...NA KUIFANYA NURU YA MUNGU ILIYO NDANI MWAKO IONEKANA KWA WENGINE-PONGU JOSEPH

Monday, July 9

NITAYASHINDA YOTE

nitapanda milima na mabonde,nikiyaishi vyema maisha niliyoyachagua,nitashinda
Nitapanda milima na mabonde,nikiyaishi vyema ambayo ni uchaguzi wa moyo wangu,nitashinda .
Sauti zote zinazonikatisha tamaa zitashindwa .
 Nitayashinda yote na kuvunja imani zote na kauli zote zinazoaminisha kushindwa,na kunifananisha mimi na wengine ambao wanaamini katika kushindwa, ama kushinda kwa kutazama mifano ya wachache na wengi walioshindwa.....Nitashinda kwa sababu katika kupambana kwangu....nautambua mwisho,ya kuwa  nitashinda licha ya changamoto zote,

Nitashinda....ninaongozwa na visheni ionayo mbali,isiyotazama tu hatua chache,bali itokanayo na uhuru usio na mipaka wa tafakari,na uhuru usio na mipaka wa kuchagua,,,,,Sitakuwa na chochote cha kupoteza hata nikipoteza maisha,kwani kuishi maisha yasiyo na mtazamo wala matokeo ya kuifanya dunia kuwa sehemu bora,kwangu ni hasara kubwa......sitajutia uamuzi wangu,kwani kwangu majuto ni kutofanya jambo kwa kuamini kuwa haliwezekani, Na kisha mwingine akalifanya... 

Sitasikiliza sauti zote ambazo zitanikatisha tamaa,zitokao kwa wale wanayoyatazama maisha katika mtazamo hasi,na wote watakao nifanya niishi maisha ya bandia,bali daima nitaisikiliza sauti iliyo moyoni mwangu,ile iliyo kubwa kuliko ile ya mawazo mengi,ile iletayo furaha..kwani natambua kuwa kila mmoja ana jukumu la kusikiliza muito wa moyo wake, .umuitaye kuifanya kazi ambayo hujengwa katika upendo na kuijtolea,ili Nuru ya MUNGU iliyo ndani mwetu ionekane...
natazama mbele daima nikiyafurahia maisha
Nitatumia nguvu zangu, akili zangu na uwezo wangu wote kuisikiliza sauti ya Mungu kutenda kadiri sauti huru ya Mungu initumapo,nikitekeleza kwa upendo,ili alama ya maisha yangu,iandikwe hapa duniani,na siku nitakapo yaanza maisha yangu baada ya maisha katika dunia hii,alama hii iwe ni nuru kwa wengine na kuwa ishara ya umoja,kujitolea,na ushindi dhidi ya wasioamini...

Nitafundisha upendo kwa kuuishi,nikitimiza malengo yangu na ndipo nitakapouvuta upendo wa wengine.
Nitafanya bila kumdhuru yeyote,nikisamehe na kuyakubali maisha na changamoto zake....na ndipo wengine watakapotambua sababu ya wao kuwepo duniani,waamke,wajitambue,watumie vipawa vyao ,wakiifanya dunia kuwa sehemu bora ... kwani kila mmoja anazo nguvu zisizoonekana..lakini zikiwe ni zaidi ya vile kila mmoja ajiwaziaye na kufikiri.....

Licha ya kuwa niendako ni mbali,nitashinda yote
 DUNIA INILILIE PALE NTAKAPOONDOKA NA KUYAENDEA MAISHA MAPYA,SIO TU KWA SABABU YA NILIKUWEPO,BALI KWA SABABU NILIYAISHE VYEMA MAISHA,PASIPO KUOGOPA MACHO YA WENGINE,BALI KWA KUTAMBUA KILE NIKIAMINICHO,AMBACHO HAKUNA AWEZAYE KUKIONA,ISIPOKUWA MWENYE MACHO YAONAYO MBALI,YALE YAUONAO MWISHO KABLA YA KUANZA KWA MWANZO EWE MUUMBA WA VYOTE NISAIDIE...AMINA.

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com